Analogia Malenga
Platinum Member
- Feb 24, 2012
- 5,292
- 10,842
UKOLONI MAMBOLEO UNAISUMBUA AFRIKA TUDenmark imesema Alhamisi kwamba itaanza kuondoa vikosi vyake nchini Mali baada ya utawala wa kijeshi uliofanya mapinduzi nchini humo mapema wiki hii kuitisha kuondoka kwao likionekana kuwa pigo kwa Ufransa ambayo inaongoza operesheni ya pamoja dhidi wanamgambo wa kiislamu nchini humo.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, hatua hiyo imekuja wakati utawala huo wa kijeshi ukizozana na washirika wa kimataifa pamoja na kieneo ukiwemo Umoja wa Ulaya ambao imewekea taifa hilo vikwazo kutokana na kutoitisha uchaguzi mwezi ujao kama ilivyokubaliwa.
Hali ya taharuki pia imetanda kutokana na madai kwamba serikali hiyo imeitisha mamluki wa kijeshi kutoka kampuni ya Wagner ya Russia, suala ambalo baadhi ya mataifa ya EU yamesema haliendeni mikataba ya kimataifa.
Denmark Januari 18 ilituma wanajeshi wake 105 nchini Mali ili kujiunga na kisosi maalum cha Ulaya kwa jina Takuba kilichobuniwa ili kukabiliana na wanamgambo wa kiislamu nchini humo. Denmark inasema kwamba ilileta kikosi hicho maalum kwa mwaliko wa Mali.
VOA
Kwa sababu magaidi ni zao la haohao wanaojifanya kuja kulindaSasa hao Mali mbona wenyewe wanashindwa kuwaangamiza hao magaidi. Hizi nchi za kiafrika ni shida sana.
Hawa majambazi wa kirusi wameshaingia Mali?....wataigeuza Libya nyingine.Hali ya taharuki pia imetanda kutokana na madai kwamba serikali hiyo imeitisha mamluki wa kijeshi kutoka kampuni ya Wagner ya Russia, suala ambalo baadhi ya mataifa ya EU yamesema haliendeni mikataba ya kimataifa.
Libya walihusika warusi?Hawa majambazi wa kirusi wameshaingia Mali?....wataigeuza Libya nyingine.
Ndio wanahusika kikamilifu sasa....ndio wanaomsaidia Jenerali HaftarLibya walihusika warusi?
Kumbe sasa ila hawakuhusika kwenye kuiharibu hio nchi,,,,,,yeye anaendeleza tu walipoanza wale wengineNdio wanahusika kikamilifu sasa....ndio wanaomsaidia Jenerali Haftar
Sio kweli, ingekuwa hivyo waislam wasingekubali wazungu wawatumie kama magaidi. Ugaidi ni zao la imani potofu kwamba kuna kitu kinaitwa "Global Jihad".Kwa sababu magaidi ni zao la haohao wanaojifanya kuja kulinda
Michezo ya akili tuSio kweli, ingekuwa hivyo waislam wasingekubali wazungu wawatumie kama magaidi. Ugaidi ni zao la imani potofu kwamba kuna kitu kinaitwa "Global Jihad".