Demokrasia Tanzania, Ghorofa linalojengwa juu ya puto?

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1572069583784.png
Declaration of interest; mleta mada ni muumini wa demokrasia. Anaamini kuwa pamoja na changamoto za demokrasia; bado ndio mfumo bora zaidi wa kuendesha mataifa yote duniani ukilinganisha na mifumo mingine.

Lengo la mada hii, nikueleza kwa uchache, ni kwa nini demokrasia haijaweza na haitarajiwi kuwa na matunda ya kuridhisha Tanzania katika siku za karibuni?

Wakuu, Mtaji mkuu wa demokrasia ni watu kwa maana kwamba mawazo ya walio wengi yaongoze wakati mawazo ya walio wachache yakiheshimiwa.

Sasa tatizo linalojitokeza kwenye demokrasia ni kwamba, si lazima mawazo ya walio wengi yawe ndio sahihi. Kuna wakati unaweza kukuta waliowengi wanaunga mkono kitu ambacho sio tu kwamba si sahihi bali ni hatari. Hii inasababishwa amma na jamii husika kutokuwa na elimu ya uraia, kutokuwa na taarifa za kutosha kuhusu wanachokiunga mkono au kukikataa au kuwa na taarifa zisizo sahihi au mtizamo/ mzuka hasi.

Tatizo hili ni kubwa sana Tanzania.Tuna watu wengi sana ambao wanaunga mkono au kupinga vitu; ukiwauliza ni kwa nini hawana majibu. Kuna watu wengi sana wanaopenda vitu visivyo na faida kwa jamii kuliko vyenye faida. Pia kuna watu wengi sana wanaotamani kusikia taarifa za watu wengine kufeli au kupata matatizo kuliko wanavyopenda mafanikio yao wenyewe. Jaribu kufikiri demokrasia kamili katika mazingira kama hayo; matokeo yake yanaweza kuwa nini?

Ili hoja hii ieleweke vyema, tutajaribu kutoa mifano miwili.

Jaribu kufikia mkutano wa siasa wenye wagombea wawili. Mmoja akasimama akaongea hoja za msingi sana kwa nusu saa. Mwenzake akasimama na asiongee kitu, akaenda akafungua mziki akaanza kuzungusha kiuno kwa muda wa robo saa tu, kisha akaenda zake kukaa, Unadhani nani atakayeungwa mkono zaidi? Anyway, tuachane na mfano huu labda unaweza ukaleta matokeo mchanganyiko.

Jaribu kufuatilia mijadala hapa JF, kati ya mijadala yenye hoja muhimu ambazo zinaweza kuwa na manufaa makubwa kwa taifa, au mijadala inayojadili watu, ni ipi yenyewafuatiliaji wengi? Bila shaka utabaini kuwa walio wengi wanafuatilia zaidi mijadala inayohusu ubaya wa watu wengine hasa inayolenga kuwadhalilisha wahusika. Hebu fikiria matokeo ya demokrasia kamili katika mazingira hayo!

Kwa mantiki hiyo, demokrasia ni kitu kizuri lakini inaweza kuwa na faida ikiwa tu jamii husika inajitambua, ina uelewa wa kutosha juu ya uraia na mtizamo chanya juu ya vitu ‘Positive altitude’. Vinginevyo demokrasia sio tu kwamba haitakuwa na mafanikio ya maana kwenye nchi husika, bali pia inaweza kuwa hatari kuliko tunavyofikiria kwa sababu inaweza kuwaingiza madarakani watu wa ajabu sana.

Ndio maana baadhi yetu tunafikiri kwamba, kujenga uelewa na mtizamo chanya kwa jamii ndilo jambo la msingi kabla ya demokrasia yenyewe na tukilifanikisha hilo, demokrasia itajiweka mahala pake yenyewe. Tunaweza kusema uelwa wa jamii na mtizamo chanya juu ya vitu ni ‘Major’ na kisha ‘Demokrasia ni ‘Minor’.Vinginevyo ni sawa na kukazana kujenga ghorofa juu ya puto?
 
Hapa nchini kuna ujinga mmoja unaendelea yaani watu 100,000 wana access na media na wapo huru kisa tu wanaimba ngonjera za kusifia uongozi uliopo hata kama ni madudu ila watu 1,000,000 wenye mawazo kinzani wamefungiwa chumbani hawaruhusu kuongea mawazo yao na iwapo wakithubutu tu kuropoka wanajikuta wamedakwa na kesi wanazofunguliwa ni uhujumu uchumi na utakatishaji pesa hivyo watu wamejawa na jazba ila uhuru wa kuongea hawana.
 
Nakubaliana na wewe. Kuna wakati watu wanapenda watu wengine wafanyiwe ubabe tuu. Wakiulizwa nitumbue nisitumbue wanasema Tumbuaaaa. Yaani kuhalalisha ubabe ni sifa ya watu wasiofikiri sawasawa!
 
Hapa nchini kuna ujinga mmoja unaendelea yaani watu 100,000 wana access na media na wapo huru kisa tu wanaimba ngonjera za kusifia uongozi uliopo hata kama ni madudu ila watu 1,000,000 wenye mawazo kinzani wamefungiwa chumbani hawaruhusu kuongea mawazo yao na iwapo wakithubutu tu kuropoka wanajikuta wamedakwa na kesi wanazofunguliwa ni uhujumu uchumi na utakatishaji pesa hivyo watu wamejawa na jazba ila uhuru wa kuongea hawana.
Ila kwa mfano hapa jukwaani tuna uhuru wa kutoa maoni kama hivi, sio kwamba kwa kuanzia, tunaweza kutumia jukwaa hili kujadili mawazo tunayoamini ni muhimu? Kupitia jukwaa kama hili, kwa mfano, mtu anaweza kufikia watu 10, 000 ndani ya saa moja na wakati hakuna mtu ambaye ana uwezo wa kukusanya idadi hiyo ya watu mahali pengine popote? huoni kwamba tatizo la Tanzania sio jukwaa la kutolea maoni bali fikra za watu?

Any way hata hata hivyo nadhani mjadala huu ni nje ya mada. ukisoma vizuri mada utaelewa inazungumzia nini.
 
Sasa mtu anaamini yeye ni always right kuliko wengine,hapana simkubali jiwe.
Nalog off
 
Ni vigumu kuwa na demokrasia ya maana katika nchi yenye masikini wajinga wengi.

Utawapa watu haki ya kuchagua, lakini hawajui wachague nini, kwa sababu hawana habari za kutosha, wamedanganywa, hawana muda wa kufuatilia mambo kwa kina etc.

Utaishia kuwa na kivuli cha demokrasia kinaitwa "electocracy". Utawala unaojinadi kuwa wa demokrasia kwa sababu kuna chaguzi tu, tena chaguzi zenyewe zinachakachuliwa

Sitetei ukandamizi wa watawala usiofuata demokrasia, naeleezea tu changamoto za demokrasia.
 
Declaration of interest; mleta mada ni muumini wa demokrasia. Anaamini kuwa pamoja na changamoto za demokrasia; bado ndio mfumo bora zaidi wa kuendesha mataifa yote duniani ukilinganisha na mifumo mingine.

Lengo la mada hii, nikueleza kwa uchache, ni kwa nini demokrasia haijaweza na haitarajiwi kuwa na matunda ya kuridhisha Tanzania katika siku za karibuni?

Wakuu, Mtaji mkuu wa demokrasia ni watu kwa maana kwamba mawazo ya walio wengi yaongoze wakati mawazo ya walio wachache yakiheshimiwa.

Sasa tatizo linalojitokeza kwenye demokrasia ni kwamba, si lazima mawazo ya walio wengi yawe ndio sahihi. Kuna wakati unaweza kukuta waliowengi wanaunga mkono kitu ambacho sio tu kwamba si sahihi bali ni hatari. Hii inasababishwa amma na jamii husika kutokuwa na elimu ya uraia, kutokuwa na taarifa za kutosha kuhusu wanachokiunga mkono au kukikataa au kuwa na taarifa zisizo sahihi au mtizamo/ mzuka hasi.

Tatizo hili ni kubwa sana Tanzania.Tuna watu wengi sana ambao wanaunga mkono au kupinga vitu; ukiwauliza ni kwa nini hawana majibu. Kuna watu wengi sana wanaopenda vitu visivyo na faida kwa jamii kuliko vyenye faida. Pia kuna watu wengi sana wanaotamani kusikia taarifa za watu wengine kufeli au kupata matatizo kuliko wanavyopenda mafanikio yao wenyewe. Jaribu kufikiri demokrasia kamili katika mazingira kama hayo; matokeo yake yanaweza kuwa nini?

Ili hoja hii ieleweke vyema, tutajaribu kutoa mifano miwili.

Jaribu kufikia mkutano wa siasa wenye wagombea wawili. Mmoja akasimama akaongea hoja za msingi sana kwa nusu saa. Mwenzake akasimama na asiongee kitu, akaenda akafungua mziki akaanza kuzungusha kiuno kwa muda wa robo saa tu, kisha akaenda zake kukaa, Unadhani nani atakayeungwa mkono zaidi? Anyway, tuachane na mfano huu labda unaweza ukaleta matokeo mchanganyiko.

Jaribu kufuatilia mijadala hapa JF, kati ya mijadala yenye hoja muhimu ambazo zinaweza kuwa na manufaa makubwa kwa taifa, au mijadala inayojadili watu, ni ipi yenyewafuatiliaji wengi? Bila shaka utabaini kuwa walio wengi wanafuatilia zaidi mijadala inayohusu ubaya wa watu wengine hasa inayolenga kuwadhalilisha wahusika. Hebu fikiria matokeo ya demokrasia kamili katika mazingira hayo!

Kwa mantiki hiyo, demokrasia ni kitu kizuri lakini inaweza kuwa na faida ikiwa tu jamii husika inajitambua, ina uelewa wa kutosha juu ya uraia na mtizamo chanya juu ya vitu ‘Positive altitude’. Vinginevyo demokrasia sio tu kwamba haitakuwa na mafanikio ya maana kwenye nchi husika, bali pia inaweza kuwa hatari kuliko tunavyofikiria kwa sababu inaweza kuwaingiza madarakani watu wa ajabu sana.

Ndio maana baadhi yetu tunafikiri kwamba, kujenga uelewa na mtizamo chanya kwa jamii ndilo jambo la msingi kabla ya demokrasia yenyewe na tukilifanikisha hilo, demokrasia itajiweka mahala pake yenyewe. Tunaweza kusema uelwa wa jamii na mtizamo chanya juu ya vitu ni ‘Major’ na kisha ‘Demokrasia ni ‘Minor’.Vinginevyo ni sawa na kukazana kujenga ghorofa juu ya puto?
Rubbish.Vuvuzera la Lumumba
 
Ni vigumu kuwa na demokrasia ya maana katika nchi yenye masikini wajinga wengi.

Utawapa watu haki ya kuchagua, lakini hawajui wachague nini, kwa sababu hawana habari za kutosha, wamedanganywa, hawana muda wa kufuatilia mambo kwa kina etc.

Utaishia kuwa na kivuli cha demokrasia kinaitwa "electocracy". Utawala unaojinadi kuwa wa demokrasia kwa sababu kuna chaguzi tu, tena chaguzi zenyewe zinachakachuliwa

Sitetei ukandamizi wa watawala usiofuata demokrasia, naeleezea tu changamoto za demokrasia.
Wapinzani tuliwategemea wawe mfano lakini nao demokrasia imewashinda. Kila unapowadia uchaguzi wa mwenyekiti wa chadema ndipo tunapoona sarakasi za viongozi wanaojitanabaisha kuwa chama chao ni cha kidemokrasia. Vyama vingine vya upinzani navyo hali ni ileile tu, kwa mfano sijawahi kusikia mkuu wa chama cha ACT Wazalendo akichaguliwa kwenye uchaguzi wowote ule tangu chama kianzishwe yaani hivi vyama vya upinzani vimejaa usanii tupu.
 
Wapinzani tuliwategemea wawe mfano lakini nao demokrasia imewashinda. Kila unapowadia uchaguzi wa mwenyekiti wa chadema ndipo tunapoona sarakasi za viongozi wanaojitanabaisha kuwa chama chao ni cha kidemokrasia. Vyama vingine vya upinzani navyo hali ni ileile tu, kwa mfano sijawahi kusikia mkuu wa chama cha ACT Wazalendo akichaguliwa kwenye uchaguzi wowote ule tangu chama kianzishwe yaani hivi vyama vya upinzani vimejaa usanii tupu.
Hatuwezi kuwa na demokrasia katika siasa kama hata familia tu zinaendeshwa kimabavu.

Mtu kalelewa katika mfumo wa kumuogopa baba kama Simba, anachosema Baba hakina mjadala.

Halafu amekuwa mkubwa wa nchi umwambie afanye mambo kwa demokrasia, atakuelewa kweli?

Tuna matatizo makubwa katika utamaduni.

Ndiyo maana unaona matatizo ya demokrasia yametamalaki kuanzia chama tawala mpaka upinzani.

Wote wamelelewa katika utamaduni wa mabavu, sasa utategemeaje wawe na tofauti kwenye demokrasia?
 
Wapinzani tuliwategemea wawe mfano lakini nao demokrasia imewashinda. Kila unapowadia uchaguzi wa mwenyekiti wa chadema ndipo tunapoona sarakasi za viongozi wanaojitanabaisha kuwa chama chao ni cha kidemokrasia. Vyama vingine vya upinzani navyo hali ni ileile tu, kwa mfano sijawahi kusikia mkuu wa chama cha ACT Wazalendo akichaguliwa kwenye uchaguzi wowote ule tangu chama kianzishwe yaani hivi vyama vya upinzani vimejaa usanii tupu.

Mkuu, hata mimi kuna kipindi nilidhani kuwa tatiizo ni chama cha siasa ila baada ya tafiti kadhaa, sasa nina uhakika tatizo ni watu na ndio maana unaona hata vikianzishwa vyama vipya matatizo ni yale yale na hata wewe ukisema uanzishe cha kwako shida zitakuwa ni zile zile.

Haitajalisha kwamba wewe una mtizamo chanya kiasi gani au ni mtu mzuri kiasi gani, kwa sababu mwisho wa siku chama ni watu na watu ndio hawa hawa wenye tabia na uelewa huu tunaouzungumizia.

Kwa hiyo kama kweli tunapenda siku tono demokrasia yenye faida, tunatakiwa kushungulika na kujengea uelewa mtu mmoja mmoja kwanza.
 
Hatuwezi kuwa na demokrmrasia katika siasa kama hata familia tu zinaendeshwa kimabavu.

Mtu kalelewa katika mfumo wa kumuogooa baba kama Simba, anachisema Baba hakina mjadala.

Halafu amekuwa mkubwa wa nchi umwambie afanye mambo kwa demokrasia, atakuelewa kweli?

Tuna matatizo makubwa katika utamaduni.

Ndiyo maana unaona matatizo ya demokrasia yametamalaki kuanzia chama tawala mpaka upinzani.

Wote wamelelewa katika utamaduni wa mabavu, sasa utategemeaje wawe na tofauti kwenye demokrasia?
mkuu nakufuatilia kwa karibu sana. kuna wakati unatoa hoja nzito kwelikweli.
 
Back
Top Bottom