ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 79,080
- 84,967
Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Festo Kiswaga, ametangaza rasmi nia yake ya kugombea ubunge katika Jimbo la Isimani, mkoani Iringa, katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Lumilo Hotel, Manispaa ya Iringa, Kiswaga amesema kuwa uamuzi huo umetokana na wito wa wananchi wa Isimani na nafasi iliyojitokeza baada ya Mbunge wa sasa, Mhe. William Lukuvi, kutangaza mwaka 2020 kuwa hatogombea tena ifikapo uchaguzi wa mwaka huu.
“Nina dhamira ya dhati kulitumikia Jimbo la Isimani. Mheshimiwa Lukuvi mwenyewe alitangaza kuwa hatagombea tena mwaka 2025, na ninasimama kwa ujasiri mkubwa kuchukua kijiti na kuendeleza maendeleo,” alisema Kiswaga mbele ya waandishi wa habari.
Akiendelea kufafanua, Kiswaga alisema kuwa mwaka 2022 aliitwa na Lukuvi jijini Dodoma, ambapo walizungumza kwa kina, na Lukuvi alimueleza kuwa amehudumu kwa zaidi ya miaka 30 na hatakuwa tena kwenye kinyang’anyiro cha ubunge.
“Kama ni kweli kwamba anapenda maendeleo ya Jimbo hili, basi kwa maslahi mapana ya wananchi wa Isimani, ni vyema akaheshimu kauli yake na kustaafu kwa hiari. Vinginevyo, wananchi wamesema wako tayari kumstaafisha kwa lazima kupitia sanduku la kura,” aliongeza Kiswaga.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Lumilo Hotel, Manispaa ya Iringa, Kiswaga amesema kuwa uamuzi huo umetokana na wito wa wananchi wa Isimani na nafasi iliyojitokeza baada ya Mbunge wa sasa, Mhe. William Lukuvi, kutangaza mwaka 2020 kuwa hatogombea tena ifikapo uchaguzi wa mwaka huu.
“Nina dhamira ya dhati kulitumikia Jimbo la Isimani. Mheshimiwa Lukuvi mwenyewe alitangaza kuwa hatagombea tena mwaka 2025, na ninasimama kwa ujasiri mkubwa kuchukua kijiti na kuendeleza maendeleo,” alisema Kiswaga mbele ya waandishi wa habari.
Akiendelea kufafanua, Kiswaga alisema kuwa mwaka 2022 aliitwa na Lukuvi jijini Dodoma, ambapo walizungumza kwa kina, na Lukuvi alimueleza kuwa amehudumu kwa zaidi ya miaka 30 na hatakuwa tena kwenye kinyang’anyiro cha ubunge.
“Kama ni kweli kwamba anapenda maendeleo ya Jimbo hili, basi kwa maslahi mapana ya wananchi wa Isimani, ni vyema akaheshimu kauli yake na kustaafu kwa hiari. Vinginevyo, wananchi wamesema wako tayari kumstaafisha kwa lazima kupitia sanduku la kura,” aliongeza Kiswaga.