DC Hapi atembelea hospitali, eneo la Uwanja wa fisi Tandale

Egnecious

JF-Expert Member
Jul 8, 2015
875
960
49873e37fcec27bb1edc3e63f401b43f.jpg


Akiwa na siku 85 tangu kuchaguliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni 21/April/2016 Ally Salum Hapi ameendelea kutekeleza kwa vitendo majukumu aliyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais John Pombe Magufuli.

Licha ya kusimamia suala la watumishi hewa katika wilaya yake ambao walikuwa 34 na kufikia 101, huku akisimamia vyema na Kulimaliza suala la upatikanaji wa madawati katika wilaya yake ambapo imekuwa changamoto kubwa tangu kutangazwa kwa Elimu bure.
Mkuu wa Wilaya Ally Salum Hapi ameelendelea na kasi hiyo ya HAPA KAZI TU ambapo siku ya leo ametembelea maeneo ya Tandale Hospitali, Uwanja wa Fisi na Soko la Tandale kwa ajili ya kusikiliza kero za wakazi wa maeneo hayo.

Akizungumza na wakazi hao amewataka kuzingatia suala la usafi na kuhakikisha wanakuwa na vifaa vya kuwekea uchafu katika maeneo yao huku akiwasisitiza wale wenye sehemu za kuegeshea magari katika maeneo yao kuyaweka katika mazingira ambayo hayataleta athari

c034c85f7547d25e9eda56b304affa79.jpg

855295581f01e920f358f48a4c4aad8c.jpg

4b273c0a95d92a764370956230fe9df8.jpg
 
Hii imekaa vizuri sio unafika hospitali unaanza kutoa matamko ya kukatisha tamaa watumishi
 
Hivi vyeo vya UDC hanina umuhimu wowote kabisa JPM alitakiwa
kubana matumizi kwa kuvifutilia mbali kabisa.
 
Hongera zake, uongozi ni kuzitafuta shida za wananchi wako na kuangalia namna ya kuzitatua. Badala tu ya kukaa ofisini na kula kiyoyozi. Safi sana
 
Ukuu wa mkoa, Ukuu wa Wilaya...ni mzigo tu kwa taifa inatakiwa vifutwe ni matumizi mabaya ya kodi za Wananchi
 
Back
Top Bottom