Dawa ya kumpata mwanamke nimtakae

Dawa ya kumpata mwanamke nimtakae

Steven Masele

Member
Joined
Jun 15, 2025
Posts
6
Reaction score
12
Wadau habarini,

Mimi nilioa mke akafuata ya Dunia starehe nilimtoa kijijini alitoka na vitu ving ikiwemo mimi kupata hasara na kuathirika kisaikolojia kwa muda mrefu. Nilirudi nyuma kimaendeleo.

Nimekaa miaka miwili kamili nikapata mwenza mwingine na kuamua kumwoa.

Mwenza huyu wa pili yaani mke alinidanganya kuwa aliolewa mara moja pia ana watoto wawili kumbe ndani ya ndoa alirekebisha usemi huo na kudai ana watoto watatu na aliolewa mara mbili.

Changamoto ni kwamba anapenda kulalamika muda wote, hana aibu kwa watu anaongea sauti ya juu na kupanic mara kwa mara yaani karibia kila siku lazima maudhi.
Niliondoka kwenda safari kidogo mwezi huu uliopita June akahama nyumbn kwangu na vitu vya ndani vyombo sola betri ya sola n.k

Mwenye nyumba akamfuma na kutia koful kabla hajamaliza kila kitu.
Kinaniuma sana kitendo hicho cha kuchukua vitu ndani bila sababu za msingi Naombeni mniambie mnaojua dawa kali ya kienyeji ambayo mwanamke nimtakae lazima akubali na asiweze kunitoka labda nimwache mimi.
 
Una Roho ya kukataliwa...

Ivunje kwanza hii...

Ukitumia uganga utazidi kupotea
 
Hama kijijini uje daslam….wa huku wanakwangua kila kitu
 
Mkuu achana na ayo mambo ,baadae njoo kitambaa cheupe karibu na Dj upande wa kulia.
 
Una Roho ya kukataliwa...

Ivunje kwanza hii...

Ukitumia uganga utazidi kupotea
Kweli inabidi nifanye hivyo, ila sasa walionitoka wote walikuwa washika dawa, wanaota hadi ndoto za kuchukuliwa kwenda kwa wachawi baadae wanarudishwa mimi waliniona story hizo haswa yule mke wangu wa kwanza ninapokuwa nae usingizini anaweza kuwa kama kapanda mizimu anakuambia huyo anabisha hodi usimfungulie anadhani ananiweza haniwezi, usiku wa manane hapo akipata ufahamu anaanza kukueleza alikuja mtu fulani kichawi.

Huyu wa pili kwa kusali unaweza kudhani kwamba huyu ndiye mke safi kabisa kumbe kitu kidogo anaenda kwa wifi yake ambaye ni mganga wa kienyeji na mm alikuwa ananishauri mikataba ila sikumwambia live kwamba nimekataa nilikuwa namchenga tu.
Ninachtamani nipate mke anamjua Mungu cyo mambo ya waganga au kuchukuliwa vitu kumbuka maisha ni magumu
 
Mkuuu Polee sana nitafute in box nikupe hio kitu
 
Dah! Duniani kweli kuna shida lakini za mleta uzi ni konkota/ngumu.Fumba macho uombewe dua njema.
 
Back
Top Bottom