David Alaba ajiunga real Madrid

tc_edo

Senior Member
Apr 9, 2021
123
98
Akiwa kaichezea Bayern Munich mechi 448, magoli 47, pasi za mwisho 35 na kubeba makombe 27, beki huyo wa kati amesaini mkataba wa miaka mitano kujiunga na klabu ya Real Madrid. Alaba ataondoka Bayern Munich akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba msimu huu.

Alaba alijiunga na Bayern munich mwaka 2010 akiwa na miaka 17 chini ya kocha Greuther Furth kumfanya mchezaji mdogo kuichezea bayern ila kwasasa record yake imevunjwa na Jamal Musiala. Alaba ameshinda taji la Bundesliga mara 10 na ubingwa wa UEFA champions league mara mbili.

Kwenye ukarasa wake wa twitter Alaba amesema, " Naondoka timu bora kujiunga na timu bora nyingine. Nafuraha kwa kweli kujiunga na Real Madrid. Baada ya miaka mingi jijini Munich naenda kukutana na changamoto mpya hivyo ntaendelea kujitoa ili kutunza historia nzuri ya timu."
IMG_20210528_215308.jpg
 
Kimafanikio ni real madrid.. Kiutajir nadhani kwa sasa itakua bayern maana wimbi la corona limeitesa Madrid kiuchumi
Hata kipesa ni Real madtid buyern hajawahi kigusa hata top three kimshiko kaka

Ni Real,Manchester united na Barcelona,

Mwaka Jana ilikua Barcelona , Real, Manchester united

Ila takwimu zimetoka Real karudi juu tena na hii nafasi hua anashikilia kitambo tangu Perez hajashika madaraka
 
Back
Top Bottom