Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 2,563
- 7,321
Mahakama ya Wilaya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam, Mei 29, 2025 imetoa hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela kwa mtuhumiwa Dotto Adinani Makando mwenye umri wa Miaka 34, Mkazi wa Yombo Kilakala baada ya kupatikana na hatia ya kosa la shambulio la aibu ambapo alimfanyia mwanafunzi wake wa kiume mwenye umri wa miaka 14.
Mnamo Januari, 2025 kwa nyakati tofauti majira ya usiku Mtuhumiwa ambaye ni mwalimu wa madrasa alikuwa anamwambia kijana huyo amnyonye uume wake, mpaka atakapotoa manii ayameze na kisha kumruhusu aondoke nyumbani.
Ilielezwa Mahakamani kuwa muda wa kutoka madrasa ukifika Mtuhumiwa alikuwa anawaruhusu wanafunzi wengine kutoka madrasa majira ya usiku na kumuamuru kijana huyo abakie ili amnyonye uume wake na humtishia kwamba endapo ataondoka atampa adhabu ya viboko.
Akisoma hukumu hiyo Mhe. Catherine Madili amesema kuwa Mahakama imeridhika na ushahidi uliowasilishwa Mahakamani hapo ambao pasi na shaka umeweza kumuunganisha mtuhumiwa kutenda kosa hilo.
Mnamo Januari, 2025 kwa nyakati tofauti majira ya usiku Mtuhumiwa ambaye ni mwalimu wa madrasa alikuwa anamwambia kijana huyo amnyonye uume wake, mpaka atakapotoa manii ayameze na kisha kumruhusu aondoke nyumbani.
Ilielezwa Mahakamani kuwa muda wa kutoka madrasa ukifika Mtuhumiwa alikuwa anawaruhusu wanafunzi wengine kutoka madrasa majira ya usiku na kumuamuru kijana huyo abakie ili amnyonye uume wake na humtishia kwamba endapo ataondoka atampa adhabu ya viboko.
Akisoma hukumu hiyo Mhe. Catherine Madili amesema kuwa Mahakama imeridhika na ushahidi uliowasilishwa Mahakamani hapo ambao pasi na shaka umeweza kumuunganisha mtuhumiwa kutenda kosa hilo.