Dar: Moto waunguza Maduka Mbagala rangi tatu

Dar: Moto waunguza Maduka Mbagala rangi tatu

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
27,638
Reaction score
62,539
moto1.jpg

Moto unawaka katika duka maeneo ya Rangi 3 Mbagala kwenye kona ya kuelekea Charambe.

Watu wanaendelea na Juhudi za kuuzima moto huo na kuokoa mali sambamba na kuzuia usisambae kwenye maduka mengine.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme.

Juhudi za kuuzima moto huo na kuokoa mali sambamba na kuzuia usisambae kwenye maduka mengine zinaendelea.

Pia soma: Soko la Kariakoo lateketea kwa moto
 
Pole zao wataopotewa na mali zao hapo Fire mpka ije sio leo
 
Dah kweli maisha hayako fair kabsa. Sasa ataanza kama alikuwa hana kitu vile
 
Piga simu FIRE mkuu ndo uje huku JF ni vyema zaidi kuliko kuanza kuhangaika na picha ili utupie humu ndani kama baadhi ya wajumbe wameshaanza kuomba picha.
 
Kuna taarifa za moto kutekeza maduka, mlioko uko leteni news
 
Kwa Ramani ya nyumba za Mbagala si rahisi kuzima moto kabla haujateketeza nyumba angalau 20
 
hiyo round about kwa kuungua
 
View attachment 691704
Moto unawaka katika duka maeneo ya Rangi 3 Mbagala kwenye kona ya kuelekea Charambe.

Watu wanaendelea na Juhudi za kuuzima moto huo na kuokoa mali sambamba na kuzuia usisambae kwenye maduka mengine.

Alafu hapo sijui kuna shida gani maeneo hayo kila siku moto tu.

Kama nawaona wafungwa waliofungwa kituoni pale wanavyokufa kihoro wanasikia moto moto tu hata kukimbia hawawezi.
 
Huu utandawazi shida kweli, watu wapo busy na simu kurekodi matukio kuliko kwenda kusaidia uokoaji.
 
Hapo roundabout kuna bar ilishaungua moto miaka michache ,patakuwa na pepo moto hapo
 
Back
Top Bottom