bampami
JF-Expert Member
- Nov 5, 2011
- 5,697
- 4,107
Kuna Jamaa yangu, kanipigia simu kunijulisha kuwa soko la mbagala rangitatu linaungua,
Mwenye updates atujulishe...
=======
Leo saa moja asubuhi umezuka moto katika soko la Mbagala Rangi 3. Sehemu iliyoathirika zaidi ni ya wauza mitumba. Imefika gari ya jeshi la zima moto na kuzima moto huo bila mafanikio. Mpaka naondoka eneo la tukio hakuna aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa.
Chanzo cha moto huo inadhaniwa ni hitilafu ya umeme.
====
UPDATES:
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kipolisi Temeke Emmanuel Likula amesema kuwa Moto ambao umezuka leo katika Soko la Mbagala Rangi tatu na kuteketeza Mabanda ya wafanyabiashara umeanza kwenye kibanda cha muuza samaki wabichi na kisha kusambaa kwenye vibanda vingine
Tarehe 6 February 2018, moto pia uliunguza maduka Mbagala na sababu ikidaiwa ni Hitilafu ya umeme. Habari zaidi, Soma=>Dar: Moto waunguza Maduka Mbagala rangi tatu
Mwenye updates atujulishe...
=======
Leo saa moja asubuhi umezuka moto katika soko la Mbagala Rangi 3. Sehemu iliyoathirika zaidi ni ya wauza mitumba. Imefika gari ya jeshi la zima moto na kuzima moto huo bila mafanikio. Mpaka naondoka eneo la tukio hakuna aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa.
Chanzo cha moto huo inadhaniwa ni hitilafu ya umeme.
====
UPDATES:
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kipolisi Temeke Emmanuel Likula amesema kuwa Moto ambao umezuka leo katika Soko la Mbagala Rangi tatu na kuteketeza Mabanda ya wafanyabiashara umeanza kwenye kibanda cha muuza samaki wabichi na kisha kusambaa kwenye vibanda vingine
Tarehe 6 February 2018, moto pia uliunguza maduka Mbagala na sababu ikidaiwa ni Hitilafu ya umeme. Habari zaidi, Soma=>Dar: Moto waunguza Maduka Mbagala rangi tatu