Mwalimu Makini
Member
- Dec 5, 2009
- 65
- 23
Nimeifuma habari hii ya kutisha kuhusu aina ya siasa zinazofanyika katika jimbo la Moshi mjini mkoani Kilimanjaro.
Wastaarabu someni TAMKO hili la Katibu wa CHADEMA mkoa wa Kilimanjaro na tuchambue yaliyotokea huko kwa lengo la kulinda mustakabali wa nchi yetu
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Kilimanjaro kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za matukio ya kinyama yaliyofanywa na CCM katika kata za Longuo A na Longuo B za wilayani Moshi.
Mnamo tarehe 18/6/2010 majira ya saa 10 jioni vijana zaidi ya 300 wa Chama Cha Mapinduzi waliokuwa wamevalia sare rasmi za chama chao (kijani na njano walikuwa katika maandamano wakitokea Mweka walikofanyia semina ya wiki moja nzima walikokuwa wakifundishwa mbinu za kukabili uchaguzi mkuu na kushinda jimbo la Moshi Mjini.
Mambo waliyofundishwa katika semina hiyo na watu waliokuwa wakifundisha huko si tatizo kubwa kwetu ingawaje tuna taarifa ya kila jambo lililofanyika huko. Tunasubiri hatua muhimu chache za kutangaza maelekezo ya kinyama yaliyokuwa yakifundishwa na kutolewa na viongozi wa ngazi za juu wa CCM katika kambi hiyo.
Tunachotaka kukemea leo ni vitendo vilivyofanyika siku ya Ijumaa tarehe 18/6/2010 vijana hao walipokuwa wakirudi kutoka kambini.
Vijana hawa walipita katika barabara kuu itokayo Mweka kuingia mjini Moshi wakiimba na kuonyesha ishara ya dole gumba ambayo hutumiwa na chama chao. Kila walikopita na kukosa kushangiliwa na pengine kupungiwa kwa alama ya vidole viwili vya ushindi alama inayotumiwa na CHADEMA walisitisha maandamano na kuwafuata watu hao na kuwapiga sana.
Katika utekeleza wa maagizo hayo ya kujeruhi na kuwatisha wakazi wa mji wa Moshi wamewajeruhi watu kadhaa na kupora mali zao. Huu ni uhuni ambao hatujauzoea mjini Moshi vijana wa chama wanapora simu kutoka kwenye sidiria ya mama mtu mzima? Hatuwezi kunyamazia udhalilishaji wa kijinsia uliofikia kiwango hiki.
CHADEMA mkoa wa Kilimanjato imesikitishwa sana na kitendo cha wahuni hawa kuingia katika majengo ya kitengo cha damu salama cha hospitali ya rufaa ya KCMC Moshi na kuwapiga wafanyakazi wote waliowakuta mle, wakavunja vifaa na vioo vya magari na hivyo kusababisha huduma ya kugawa damu salama kukosekana kwa siku hiyo.
Ni watu wangapi wamefariki kutokana na kukosekana kwa damu siku hiyo?
Je CCM wameamua sasa hata kumwaga damu iliyotolewa na wasamaria wemu kwa lengo la kuokoa maisha ya watanzania wenzao? Kiu ya Damu ya CCM inaiwakia nchi kwa makali makubwa. Sasa wanaitaka damu hadi kuifuata katika kituo c ha damu salama.
Taarifa zenye uhakikia tulizo nazo ni kuwa katika msafara huo walikuwepo viongozi wa chama na pia msafara uliongozwa na askari wa usalama barabarani. Wakati vitendo vya vurugu vikifanyika askari hawakuchukua hatua yoyote zaidi ya kutuliza mambo kwa wanaojeruhiwa na kuharibiwa mali zao.
Tunajiaminisha kuwa kiburi cha vijana hawa wa CCM hakitokani tu na mafunzo waliyopewa bali maagizo waliyopewa na viongozi wa chama chao na serikali. Vijana hawa wamehakikishiwa kuwa hakuna mtu wa kuwafanya lolote watakapovunja sheria za nchi.
Hadi sasa jeshi la polisi wilayani Moshi halijachukua hatua yoyote dhidi ya CCM wala wahuni hawa.
CHADEMA mkoani Kilimanjaro inaamini kuwa ni jukumu la Polisi kulinda raia wote na mali zao. Jukumu hili linatokana na ukweli kuwa raia wote wanalipa kodi ili kuwezesha upatikanaji wa huduma kutoka katika idara zote za serikali.
CHADEMA mkoa wa Kilimanjaro inazo taarifa kuwa viongozi wa ngazi za juu serikalini na katika Chama Cha Mapinduzi wamekuwa wakiwachochea vijana hawa kufanya vurugu eti kwa lengo la kuwatisha wakazi wa Moshi Mjini kutokana na msimamo wao wa kuichagua CHADEMA.
Mathalan Katibu Mkuu wa CCM Mhe. Yusuph Rajab Makamba alifika mjini Moshi na kufikia kutaja majina ya viongozi waandamizi wa CHADEMA ambao atawashughulikia yeye binafsi. Aliendelea kutamba kuwa yeye ndiye mwenye serikali na wanaweza kufanya lolote bila kuhojiwa. "Sisi tunaiagiza serikali kufanya kitu bila kuhojiwa" alijitapa.
Mtunza hazina wa CCM taifa Amos Makala akifungua kambi hiyo ya vijana aliwaagiza vijana hao kuwa "Mtu wa CHADEMA akikupiga ngumi moja wewe mpige kumi"
Taarifa tulizo nazo ni kuwa Mhe. Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM taifa akiwa katika ziara mkoani kwetu aliwahakikishia vijana wa CCM kuwa yeye ndiye mwenye serikali na kwamba analitaka jimbo la Moshi |Mjini kwa gharama yoyote.
Kwa kauli hizi za viongozi ambao wote si wazaliwa wala wakazi wa Moshi ni wazi kuwa hawajali umwagaji damu unapofanyika mjini hapa. Wanajua wazi kwa kauli zao zitaishia kusababisha umwagaji damu lakini hawaogopi kwani familia zao haziko hapa. Wala hawana ndugu yeyote aishiye mjini Moshi.
CCM wanajitapa kuwa wametengeneza jeshi lake la kupambana kulinda maslahi yake. Sisi CHADEMA tunauliza je sheria ya vyama vya siasa inaruhusu umiliki na uendeshaji wa jeshi kufanywa na chama cha siasa.
Kama CHADEMA nasi tukaamua kuunda jeshi letu la kupambana na uonevu wa CCM tutaepuka vipi umwagaji damu?
Kwa nini CCM hawataki kufanya siasa za kistaarabu? Kwa nini hawataki tushindani kwa kujinadi kwa wananchi?
Tunasubiri majibu na hatua zitakazochukuliwa na jeshi la Polisi hapa Moshi ili nasi tutangaze msimamo wetu na namna tutakavyowalinda watu wa Moshi na mali zao.
Tutatoa pia maelezo ya kila jambo lililotokea na kuwapelekea wahisani wa nchi yetu na jumuia za kimataifa endapo serikali haitachukua hatua za kuturidhisha dhidi ya wahuni hawa.
HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE
SIGNED
..........................
Basil Lema
KATIBU (M)
Wastaarabu someni TAMKO hili la Katibu wa CHADEMA mkoa wa Kilimanjaro na tuchambue yaliyotokea huko kwa lengo la kulinda mustakabali wa nchi yetu
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
Mkoa wa Kilimanjaro
P.O BOX 933, MOSHI
Mkoa wa Kilimanjaro
P.O BOX 933, MOSHI
20/6/2010
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UVUNJIFU WA AMANI ULIOFANYWA NA CCM MJINI MOSHI
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Kilimanjaro kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za matukio ya kinyama yaliyofanywa na CCM katika kata za Longuo A na Longuo B za wilayani Moshi.
Mnamo tarehe 18/6/2010 majira ya saa 10 jioni vijana zaidi ya 300 wa Chama Cha Mapinduzi waliokuwa wamevalia sare rasmi za chama chao (kijani na njano walikuwa katika maandamano wakitokea Mweka walikofanyia semina ya wiki moja nzima walikokuwa wakifundishwa mbinu za kukabili uchaguzi mkuu na kushinda jimbo la Moshi Mjini.
Mambo waliyofundishwa katika semina hiyo na watu waliokuwa wakifundisha huko si tatizo kubwa kwetu ingawaje tuna taarifa ya kila jambo lililofanyika huko. Tunasubiri hatua muhimu chache za kutangaza maelekezo ya kinyama yaliyokuwa yakifundishwa na kutolewa na viongozi wa ngazi za juu wa CCM katika kambi hiyo.
Tunachotaka kukemea leo ni vitendo vilivyofanyika siku ya Ijumaa tarehe 18/6/2010 vijana hao walipokuwa wakirudi kutoka kambini.
Vijana hawa walipita katika barabara kuu itokayo Mweka kuingia mjini Moshi wakiimba na kuonyesha ishara ya dole gumba ambayo hutumiwa na chama chao. Kila walikopita na kukosa kushangiliwa na pengine kupungiwa kwa alama ya vidole viwili vya ushindi alama inayotumiwa na CHADEMA walisitisha maandamano na kuwafuata watu hao na kuwapiga sana.
Katika utekeleza wa maagizo hayo ya kujeruhi na kuwatisha wakazi wa mji wa Moshi wamewajeruhi watu kadhaa na kupora mali zao. Huu ni uhuni ambao hatujauzoea mjini Moshi vijana wa chama wanapora simu kutoka kwenye sidiria ya mama mtu mzima? Hatuwezi kunyamazia udhalilishaji wa kijinsia uliofikia kiwango hiki.
CHADEMA mkoa wa Kilimanjato imesikitishwa sana na kitendo cha wahuni hawa kuingia katika majengo ya kitengo cha damu salama cha hospitali ya rufaa ya KCMC Moshi na kuwapiga wafanyakazi wote waliowakuta mle, wakavunja vifaa na vioo vya magari na hivyo kusababisha huduma ya kugawa damu salama kukosekana kwa siku hiyo.
Ni watu wangapi wamefariki kutokana na kukosekana kwa damu siku hiyo?
Je CCM wameamua sasa hata kumwaga damu iliyotolewa na wasamaria wemu kwa lengo la kuokoa maisha ya watanzania wenzao? Kiu ya Damu ya CCM inaiwakia nchi kwa makali makubwa. Sasa wanaitaka damu hadi kuifuata katika kituo c ha damu salama.
Taarifa zenye uhakikia tulizo nazo ni kuwa katika msafara huo walikuwepo viongozi wa chama na pia msafara uliongozwa na askari wa usalama barabarani. Wakati vitendo vya vurugu vikifanyika askari hawakuchukua hatua yoyote zaidi ya kutuliza mambo kwa wanaojeruhiwa na kuharibiwa mali zao.
Tunajiaminisha kuwa kiburi cha vijana hawa wa CCM hakitokani tu na mafunzo waliyopewa bali maagizo waliyopewa na viongozi wa chama chao na serikali. Vijana hawa wamehakikishiwa kuwa hakuna mtu wa kuwafanya lolote watakapovunja sheria za nchi.
Hadi sasa jeshi la polisi wilayani Moshi halijachukua hatua yoyote dhidi ya CCM wala wahuni hawa.
CHADEMA mkoani Kilimanjaro inaamini kuwa ni jukumu la Polisi kulinda raia wote na mali zao. Jukumu hili linatokana na ukweli kuwa raia wote wanalipa kodi ili kuwezesha upatikanaji wa huduma kutoka katika idara zote za serikali.
CHADEMA mkoa wa Kilimanjaro inazo taarifa kuwa viongozi wa ngazi za juu serikalini na katika Chama Cha Mapinduzi wamekuwa wakiwachochea vijana hawa kufanya vurugu eti kwa lengo la kuwatisha wakazi wa Moshi Mjini kutokana na msimamo wao wa kuichagua CHADEMA.
Mathalan Katibu Mkuu wa CCM Mhe. Yusuph Rajab Makamba alifika mjini Moshi na kufikia kutaja majina ya viongozi waandamizi wa CHADEMA ambao atawashughulikia yeye binafsi. Aliendelea kutamba kuwa yeye ndiye mwenye serikali na wanaweza kufanya lolote bila kuhojiwa. "Sisi tunaiagiza serikali kufanya kitu bila kuhojiwa" alijitapa.
Mtunza hazina wa CCM taifa Amos Makala akifungua kambi hiyo ya vijana aliwaagiza vijana hao kuwa "Mtu wa CHADEMA akikupiga ngumi moja wewe mpige kumi"
Taarifa tulizo nazo ni kuwa Mhe. Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM taifa akiwa katika ziara mkoani kwetu aliwahakikishia vijana wa CCM kuwa yeye ndiye mwenye serikali na kwamba analitaka jimbo la Moshi |Mjini kwa gharama yoyote.
Kwa kauli hizi za viongozi ambao wote si wazaliwa wala wakazi wa Moshi ni wazi kuwa hawajali umwagaji damu unapofanyika mjini hapa. Wanajua wazi kwa kauli zao zitaishia kusababisha umwagaji damu lakini hawaogopi kwani familia zao haziko hapa. Wala hawana ndugu yeyote aishiye mjini Moshi.
CCM wanajitapa kuwa wametengeneza jeshi lake la kupambana kulinda maslahi yake. Sisi CHADEMA tunauliza je sheria ya vyama vya siasa inaruhusu umiliki na uendeshaji wa jeshi kufanywa na chama cha siasa.
Kama CHADEMA nasi tukaamua kuunda jeshi letu la kupambana na uonevu wa CCM tutaepuka vipi umwagaji damu?
Kwa nini CCM hawataki kufanya siasa za kistaarabu? Kwa nini hawataki tushindani kwa kujinadi kwa wananchi?
Tunasubiri majibu na hatua zitakazochukuliwa na jeshi la Polisi hapa Moshi ili nasi tutangaze msimamo wetu na namna tutakavyowalinda watu wa Moshi na mali zao.
Tutatoa pia maelezo ya kila jambo lililotokea na kuwapelekea wahisani wa nchi yetu na jumuia za kimataifa endapo serikali haitachukua hatua za kuturidhisha dhidi ya wahuni hawa.
HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE
SIGNED
..........................
Basil Lema
KATIBU (M)