Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 42,451
- 50,183
Wandungu, nimeingia mji kasoro bahari leo, kinachoshangaza hakuna usafiri wa daladala kama ilivyozoeleka, usafiri pekee ni bodaboda, kilikuu na bajaji, nimeuliza watu kadhaa wanasema wenye daladala wamegoma.
Je, nini kimeshindikana kuzungumzika mpaka kufikia adha hii!?
-----
Je, nini kimeshindikana kuzungumzika mpaka kufikia adha hii!?
-----
Kwa zaidi ya saa nane wakazi wa mkoa wa Morogoro wamekosa huduma ya usafiri wa daladala kutokana na mgomo wa madereva kwa madai ya bajaji kupakia abiria
Kwa zaidi ya saa nane wakazi wa mkoa wa Morogoro wamekosa huduma ya usafiri wa daladala kutokana na mgomo wa madereva kwa madai ya bajaji kupakia abiria kinyume na utaratibu waliowekewa hivyo kuwaathiri kibishara.
Madereva wa daladala wanalalamikia walichodai wingi wa bajaji kunakobabisha wao kukosa abiria na kwamba wameamua kurudisha magari yao kwa wamiliki kutokana na kufanya kazi bila maslahi, ingawa baadhi ya mabasi yameonekana kubeba abiria na kuwashusha katika standi hiyo ya daladala.
Kufuatia mgomo huo wa madereva, mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk,Kebwe Steven Kebwe ameagiza mkuu wa wilaya kutoa elimu kwa kwa madereva wa bajaji ili wafanye kazi kwa mujibu wa leseni zao na wanaokiuka kuchukuliwa hatua stahiki .