Mnamo Desemba 1937, wakati wa mechi ya mpira wa miguu huko Stamford Bridge huko London kati ya Chelsea FC na Charlton FC, mchezo ulisimamishwa katika dakika ya 60 kutokana na ukungu mkubwa.
Kwa bahati mbaya, kipa wa Charlton FC, Sam Bartram, hakujua kwamba mechi ilikuwa imesimamishwa na aliendelea kulinda lango lake kwa dakika nyingine kumi na tano. Hakusikia filimbi ya mwamuzi kwa sababu ya kelele kutoka kwa umati nyuma yake. Akiamini kwamba wachezaji wenzake walikuwa wakishambulia lango la wapinzani, alisimama akiwa amenyoosha mikono, akiwa makini kabisa kulinda lango lake huku kukiwa na ukungu mnene.
Ilikuwa dakika kumi na tano tu baadaye polisi wa uwanjani walipomwendea na kumfahamisha kuwa mechi hiyo ilikuwa imesimamishwa dakika kumi na tano Nyuma
Sam Bartram, alihuzunishwa sana na kutamka maneno ambayo yalikuja kuwa nukuu maarufu
Alisema;
View attachment 3203768
“INASIKITISHA JINSI KUWA MARAFIKI ZANGU WALINISAHAU NILIPOKUWA NALINDA LANGO LAO.