Dah! Wabongo buana eti mathsjery ni tapeli

mathsjery

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2015
Posts
2,287
Reaction score
1,855



Katika maisha yangu, tangu nianze kufanya kazi kama web developer sikuwahi kubahatika kufanya kazi na mtanzania yeyote mbali na ile task ndogo ya Mkaruka ambayo aliileta hapa jamvini inayohusu blog ya ajiraalert nb: mimi si mtegenezaji wa hiyo blog bali nilirekebisha tu kisehemu kidogo, ataeleza mkaruka mwenyewe akipenda, na hakuna hata siku moja niliwahi fuatwa PM na mtu serious kwa kazi ya web development, in majority nimebahatika kufanya na watu weupe tena remotely.

Kifupi tuache hisia zisizo na maana kwakuwa hatuna ushahidi, wapo watu wengi wamekuwa wakija pia PM nawasaidia bila malipo mahali walipokwama sasa kama kuna mtu niliwahi mtapeli kwa lolote alete ushahidi hapa, naomba Mod msimpigeban wala msifute chochote kutoka PM kitakacholetwa na wadau hapa.

Ahsanteni.
Mlolongo na chilubi I'm a real developer msisite kunitafuta popote pale kikazi zaidi mimi sio matthew
refer

Kwanini Ma IT bongo sio matajiri?
 
Unachotakiwa kukifanya thibitisha kuwa wewe si tapeli..! Alasivyo unachokifanya ni kupunguza imani zaidi kwa watu!
 
Unachotakiwa kukifanya thibitisha kuwa wewe si tapeli..! Alasivyo unachokifanya ni kupunguza imani zaidi kwa watu!
Kweli siyo kila aliye jela ni mhalifu.


Kwamba mathsjery ni tapeli, aisee!!
Jamaa binafsi niko Dar na yeye yuko Mwanza na amenisaidia bure kabisa tena nilimpa details zangu muhimu kabisa.
Ninyi ndio huwa mnaharibu watu wema, labda kama umechanganya majina.
 
Umesoma nilichoandika kwa sauti ya tofauti rudia kwa uyakinifu
 
Siwezi thibitisha zaidi ya hapo, kwa kuwa hakuna aliyethibitisha utapeli wangu kwa evidence.

Ukisoma vizuri hiyo convo, chilubi kamtaja Matthew, Mlolongo akaibuka kwa kutaja kumbe mathsjery ni tapeli!

Chilubi akajibu kwamba kama hiyo ID ya Mathsjery ni ID nyingine ya Matthew, ndiyo.

Otherwise, kama hiyo ID ya Mathsjery siyo ya Matthew, basi siyo.

Mleta thread pitia vizuri.

Nafikiri Mlolongo anaweza kufafanua, kwa nini alimtaja Mathsjery wakati anayezungumziwa ni Matthew.
 
Itapendeza zaidi ndo maana nikasema tusifanye kwa hisia
 

Hakuna member anayeitwa/anayejiita Matthew humu jamiiforums. Hayupo!
 
Hakuna member anayeitwa/anayejiita Matthew humu jamiiforums. Hayupo!

Chilubi alimtaja Matthew, kwa nini hukuuliza ID sahihi na ukaja na conclusion kwamba ni mathsjery?

Hata Chilubi alipojibu kwamba kama hiyo ni ID nyingine ya Matthew basi ndiyo, wewe ulikaa kimya as if ni kweli unajua hi ni ID nyingine ya Matthew.

Jaribu kupitia hiyo convo uone jinsi wewe ulivyoperform hapo.
 
Huyo aliyetapeliwa alete ushahidi, tumalize mzizi ea fitina

Mzee iko hivi....
Mtu akisema: " Kuna jamaa humu jamiiforums anaitwa Mkarukaa amenitapeli 40,000"

Kwa watu walio familiar na wewe Mkaruka moja kwa moja wata-link shutuma hizo na jina lako. Kwa sababu majina yanaendana sana, inawezekana mwandishi alikose spelling tu.

Na ikitokea jamiiforums hakuna member mwingine mwenye username inayofananana na wewe Mkaruka unategemea nini?

Mkarukaa -> Mkaruka

Matthew -> mathsjery

Bila shaka Mailman sasa unakubaliana na mimi. Asante.
 

Matthew poul, Matthewthomas ni ID ambazo zinaanza na Matthew.

Mkuu kubali kwamba ulikurupuka, then tutoke hapo twende kwa chilubi, atuambie alimaanisha nani na alete ushahidi.

Kwenye case sensitive kama hizi, usipende kufanya conclusion kwa kubadili hata herufi moja ya jina na kuweka lako.

Watu walio familiar! Naona kwa statement hii, kuna kitu zaidi unachotaka kufanya kwa makusudi, mwanzo nilijua umekosea bahati mbaya, ila naona umejikosesha makusudi kwa sababu uko familiar.
 
Mfano humu ndani kuna mimi Mkaruka , kuna mukaruka mzee na kuna mkaruka ataja rinu .

Sasa mtu akipiga tukio, kusingiziana siyo poa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…