CRDB Mkopo wanaiba au ndio halali?

CRDB Mkopo wanaiba au ndio halali?

AZUSA STREET

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2013
Posts
2,007
Reaction score
1,898
Nimechukua ka m 14 toka CRDB hapa mkoa fulani, kwenye account wameniwekea m 13.4 yaani kama laki sita yote wamekata hawajadeposite. nikawafuata, walitakiwa wanikate kwenye mshahara wangu laki tatu na nusu kila mwezi, toka kwenye laki sita hapo ukitoa laki tatu na nusu inabaki kama laki mbili na nusu (250,000/=), wakasema kuwa, hiyo laki tatu na nusu ambayo wamenikata hata kabla mwezi haujaanza wamechukua kama bond, mshahara wangu ukikatwa na wao kuletewa watanirudishia kwenye account yangu.

Matokeo yake, mshahara ulishakatwa na inavyoonekana ni kama hawatarudisha kwenye account yangu, tatizo ninaloliona ni kwamba, hela hiyo imeenda wapi, imeenda kwenye mifuko wa wafanyakazi wa bank au imekuwaje, nimekatwa hata kabla mwezi wa kukatwa haujaanza. bahati mbaya nimesafiri niko mbali kurudi eneo husika si chini ya miezi miwili.

Kama kuna mfanyakazi wa CRDB hapa atueleweshe, hivi garama za kushughulikia nyaraka za mkopo mnakata hadi kufikia laki tano hadi sita kwa hela ndogo kama hiyo au? Nikiwapigia simu wanasema nimeshakatwa, na hela kwenye statement haipo, haijaingia, bahati mbaya zaidi ni kwamba wao wanalete e-statement kwenye email yangu kila mwezi hivyo inaonyesha kila transaction niliyoifanya.
 
Mshahara unalipwa na hazina??? If yes bas crdb huwa wanakata marejesho ya mwezi husika kama mkopo wako umepitishwa baada ya tarehe 7 ya kila mwez...this is because payroll ya serikal inafungungwa baada ya tarehe 7...
 
Mshahara unalipwa na hazina??? If yes bas crdb huwa wanakata marejesho ya mwezi husika kama mkopo wako umepitishwa baada ya tarehe 7 ya kila mwez...this is because payroll ya serikal inafungungwa baada ya tarehe 7...
kwa hiyo wakikata namna hiyo hawarudishi wakipata toka hazina? ni kweli unatoka hazina....manake wao waliniambia tumekukata mwanzoni ili tusikudai mwezi ujao lakini hazina wakileta cheki tunaurudisha kwenye account yako....ninachoogopa hazina walishakata kitambo sasa naogopa isije hela ikaenda mfukoni mwa mtu binafsi kwasababu walinihakikishia watairudisha baada ya kuwaconfront.
 
Hapana kama hazina wakikata this month bas kabla ya tarehe 4 crdb huwa wanarudisha pesa yako kwny account yako...wala usipate strec chief....
 
Hapana kama hazina wakikata this month bas kabla ya tarehe 4 crdb huwa wanarudisha pesa yako kwny account yako...wala usipate strec chief....
nashukuru mkuu. lakini leo ni tarehe 9...hahaha. i hope wataipata hii msg na kurusha hela yangu. laki tatu unusu parefuuuuu
 
Jaribu kumulza huyu afsa mikopo crdb, namba 0717011162.
hata nikimpigia huyu sidhani kama atakuwa anatoka kwenye tawi nililochukulia kwasababu nimeshawapigia kadhaa toka matawi mengine kwenye simu walizotupatia nao wananitaka niende kwenye tawi nililofungulia, na kwenye tawi huko ni mbali mimi nimesafiri kikazi kwa siku nyingi nitakuwa huku na hela nilikuwa nimechukua kwa malengo. hadi nije nirudi washanichelewesha sana.
 
Hapana kama hazina wakikata this month bas kabla ya tarehe 4 crdb huwa wanarudisha pesa yako kwny account yako...wala usipate strec chief....
kwa mashirika ya umma, hazina hawakati pesa ya mkopo wa CRDB kwenye mshahara wako. Bali CRDB wanakata pesa yao kwenye ile pesa unayowekewa kwenye akaunti yako
 
kwa mashirika ya umma, hazina hawakati pesa ya mkopo wa CRDB kwenye mshahara wako. Bali CRDB wanakata pesa yao kwenye ile pesa unayowekewa kwenye akaunti yako
sasa kwanini nianze kukatwa kabla hata ya kupata mkopo? unaomba 14m badala ya kukupatia hiyo wanakukata kato hata kabla hawajakuwekea kwenye account, malengo yangu mimi wanayavuruga sasa, achilia mbali laki kama mbili na nusu wanasema za uchakavu/services za mkopo ambazo sijui ni services zipi? za kuprint zile form, au mafuta ya wao kwenda hazina au sijui ni soda hata sielewi laki zote hizo kuwa za services. ok, mmekata laki mbili na nusu kwenye ile niliyoomba, halafu tena mnakata na kato la kwanza hata kabla sijapata mkopo wenyewe? why
 
Hapo ndugu hakuna tatizo. hayo makato waliyochukua toka 14m ni documentation ama facility fee ambayo ni lazima ukatwe unapochukua mkopo.

hiyo nyingine iliyokatwa hazina ni kwa vile mkopo wako ilikuwa ni lazima uingie kwanza kwenye payroll ya serikali waone makato yanakuja ndio wakupe mkopo. sasa wakiona na hii ya safari hii imekuja watarudisha tu hiyo hela yako uliyokatwa awali.
Tatizo hapa ni mfumo wa sasa wa kuingiza makato kwenye mfumo wa payroll wa serikali na wafanyakazi kwa kujua hilo wamekuwa wakiomba mikopo kwenye taasisi nyingi kwa wakati mmoja na ataewahi kuweka kwenye payroll ya hazina analamba bingo mkopeshaji mwingine analia tu. ndio maana hakikisho hilo ni la lazima kwa sasa hadi hapo mfumo utakapo badilika tena
 
Back
Top Bottom