CRDB bank wizi huu ni kwanini?

CRDB bank wizi huu ni kwanini?

Swiper

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2013
Posts
444
Reaction score
168
Leo nimeenda bank ya CRDB kama ilivyo ada kabla ya kuchukua mkwanja mteja unapenda kujua salio lako.. yaani balance inasomeka je. kuingia nakumpatia mhudumu wa benki, ananiambia kuna utaratibu mpya.

Andika jina na account number yako kwenye kitabu kisha utachajiwa gharama ya kuona au kjua salio lako ambao ni shilling 500/=. Nilishikwa na mstuko, maswali mengi yakaniijia kichwani.Je hii huduma ni ya kulipia.

je huu sio wizi wa mchana kweupe.kila mwezi kuna makato ya benki "monthly service fee" kila ukitoa hela wanakata, "withdrawal fee" mwajiri wako au money transfer ikifanyika wana kukata "service fee" n.k hapo ni kwenye account zetu za akiba.

Hivi nini maana ya monthly fee? kama haijumulisha na kutoa balance ukiomba na hadi leo sijawahi kutumiwa bank statement ya accounti yangu yapata miaka 5, je benk wanatoa huduma gani kwangu, kama hawatumi monthly statement ya account kwanini nisiombe balance? nikiomba kwanini nilipie.

Mamlaka ya kusimamia haki za mlaji/mteja yapo wapi. BOT regulator na supervisor wa mabenki mnalijua hilo? hiyo fee inamnyonya mlaji na mteja wa huduma ya benki, kumbuka salio langu na lako na mwenigine ndo sehemu ya mikopo CRDB wanatoa na kupata faida kubwa.

CRDB Bank Please tafadhali acheni wizi wa mchana kweupe, hiyo gharama mliyo ileta haitafanikisha kuongeza wateja, labda kama mnataka kupunguza wateja.

Nawasilisha.

SP
 
Nilishasema hapa siku moja uzalendo kamwe hautaletwa na makampuni ya nje kwanza inapaswa makampuni ya ndani yaoneshe uzalenzo! nasikitika siku hizi tunashindwa kutofautisha kampuni la nje na la ndani wote wamejikita kutafuta overprofit kwa kumuumiza mwananchi haijulishi kampuni za simu au laa! mfano mzuri kampuni za sukari zinazalisha sukari nchini zinauza 2000 kwa kilo moja wakati za nje zinauza 1600 mtaani
mara nyingine mi natamani hata bora makampuni ya nje tu tujue moja tunaibiwa kuliko kuumizwa na watanzania wenzetu hebu fikiri mtu anaelipwa mshahara laki mbili bank si atachukua laki na nusu kunakoelekea kwa ajili ya uhujumu huu unaofanyika wa taasisi binafsi
 
Naungana na ww kiukweli iyo chaji waliyoleta itamuumiza Mteja, kama staff ameajiriwa kukaa kaunta ili ahudumie Wateja iweje sasa mtuchaji walaji? Mbona miaka yote iyo chaji haipo , au waneona ndio chanzo cha mapato? Hii kitu niliwahi kuisikia nmb !!
Mm siongelei crdb tu , je taifa letu...
Imagine unapata mshahara unakatwa PAYE iyo ni kidogo , alaf inaingizwa kwenye Akaunti wanakata 3,000 salary processing fee, kwenye Akaunti unakatwa 1000 ya mwezi, mila ukitoa wanakata 700 kwenye ATM, alaf ukikusanya mshahara ili uzungushe upate faida unaambiwa nenda mamlaka za vibali, uko hela iyo iyo ya mshahatmra uliyokatwa kodi mwanzoni, inakatwa tena kodi kwenye vibali, then ukiwa na ako ka biahsara unalipia tena mapato ya biashara, unalipia pango alaf kwenye mshahara/ au kama ni loan wanakata interest....hili taifa uchumi kama ulivo dunia nzima uko kinyonyaji zaidi kwa low income earner.
Mwanajf kama una elfu20 au50 bila chanzo cha kuaminika chukua 50 yako weka nyumbani kumiliki Akaunti ni sawa na kutoboa gunia lako la nafaka eti nafaka zipate hewa , zitaisha kwa kudondoka, ebu fikiria:

Umedeposit elfu20

makato ya kadi 4000
Monthly maintainance 1000

Minimum balance 10,000

ATM fee700

Utaletewa cash available 4,300/= kwenye elfu20 unabaki na 4300
Unaambiwa Mpendwa mteja huwezi kuchukua hela haitoshelezi, ongeza Salio !!

Mambo gani haya??

Tunaangamia!!
 
Hata Mimi nmesikia rafiki yangu analalamika kuwa naye kaibiwa.Kwa kweli sio vizuri maana Tumewaamini ili muhifadhi pesa zetu alafu mnatuibia acheni huo mchezo
 
Hivi hakuna mfanyakazi wa crdb humu? Ili ajibu hizi tuhuma?, ukimya unazua maswali na mashaka dhidi yenu.
 
Leo nimeenda bank ya CRDB kama ilivyo ada kabla ya kuchukua mkwanja mteja unapenda kujua salio lako.. yaani balance inasomeka je. kuingia nakumpatia mhudumu wa benki, ananiambia kuna utaratibu mpya.

Andika jina na account number yako kwenye kitabu kisha utachajiwa gharama ya kuona au kjua salio lako ambao ni shilling 500/=. Nilishikwa na mstuko, maswali mengi yakaniijia kichwani.Je hii huduma ni ya kulipia.

je huu sio wizi wa mchana kweupe.kila mwezi kuna makato ya benki "monthly service fee" kila ukitoa hela wanakata, "withdrawal fee" mwajiri wako au money transfer ikifanyika wana kukata "service fee" n.k hapo ni kwenye account zetu za akiba.

Hivi nini maana ya monthly fee? kama haijumulisha na kutoa balance ukiomba na hadi leo sijawahi kutumiwa bank statement ya accounti yangu yapata miaka 5, je benk wanatoa huduma gani kwangu, kama hawatumi monthly statement ya account kwanini nisiombe balance? nikiomba kwanini nilipie.

Mamlaka ya kusimamia haki za mlaji/mteja yapo wapi. BOT regulator na supervisor wa mabenki mnalijua hilo? hiyo fee inamnyonya mlaji na mteja wa huduma ya benki, kumbuka salio langu na lako na mwenigine ndo sehemu ya mikopo CRDB wanatoa na kupata faida kubwa.

CRDB Bank Please tafadhali acheni wizi wa mchana kweupe, hiyo gharama mliyo ileta haitafanikisha kuongeza wateja, labda kama mnataka kupunguza wateja.

Nawasilisha.

SP

watetezi wetu washajifia wao wanaona sawa tu sisi kuumizwa hakika inauma sna mkuu
 
Mamlaka ya kusimamia haki za mlaji/mteja yapo wapi. BOT regulator na supervisor wa mabenki mnalijua hilo? hiyo fee inamnyonya mlaji na mteja wa huduma ya benki, kumbuka salio langu na lako na mwenigine ndo sehemu ya mikopo CRDB wanatoa na kupata faida kubwa.

CRDB Bank Please tafadhali acheni wizi wa mchana kweupe, hiyo gharama mliyo ileta haitafanikisha kuongeza wateja, labda kama mnataka kupunguza wateja.

Nawasilisha.

SP
Hapo kwenye RED wanalijua sana na wala usipoteze muda kuangaika nao kwani hautafanikiwa, labda ni sehemu ya ulaji huu. Unajua jinsi mabenki yanavyoibia watu kwenye mikopo ama umesahau, hali ni ngumu na hao hao BOT wanabariki kwani mwisho wa mwaka wanatumiwa Calender za mabenki husika labda na vijizawadi vingine.

Unaweza kuomba mkopo mkakubaliana riba mfano 18%, baada tu ya kuingia wanaongeza wanavyotaka hata hadi 26% kwa visingizio mbali mbali mara "inflation " imependa mara oh wenzetu wamepandisha na sisi tunafanya hivyo na madai mengine kama hayo. BOT wapo tu wanasubiri mahesabu yatakayoonyesha kuwa benki imepata faida 25%. Wewe hushangai mlundikano wa mabenki ya kigeni hapa nchini. Nenda kwa wenzetu walioko makini kama Ethiopia uone kama kuna upuuzi huu. Hili ni shamba la bibi kwani mlinzi wa shamba "BOT" kasinzia mkuu!
 
Yaan crdb hasa bank ya tanga wamezidi ukiritimba na kunyanyasa wateja wao wanatia hasira sana kwanza foleni ni kubwa wahudumu wako slow wanaringa sana
 
Crdb ni uwizi mwingine tz juzi nilikwend tawi la songea kutengenezewa kadi yangu iliyoisha muda wake wakaniambia nilipie 7700 Tsh yaani tanzania ni twanga kotekote!
 
watetezi wetu washajifia wao wanaona sawa tu sisi kuumizwa hakika inauma sna mkuu


Mtemi Andrew Chenge wakimkata hiyo kwenye vile "vijisenti" vyake anaona poa tu. Kazi kwetu sisi kwenye balance ya elfu 20,000 ikipungua 500 tu, hela haitoki - huna salio lakutosha kutoa hela.
 
CRDB wanafanya hivo kwa kuwa wana wateja wengi mno na kimsingi wengine hawana haja na nyie.

Nashangaa mtu analalamika wakati kuna benki kibao ndogo na zinakupa huduma zote kama crdb au zaidi. Siku hizi kuna mobile banking zinazotolewa na bank nyingi hata zile ndogo. Kwa nini mnakaa CRDB?

Ukiendelea kukaa, tulia waendelee kukufaidi na usilalamike make ni uzembe
 
CRDB wanafanya hivo kwa kuwa wana wateja wengi mno na kimsingi wengine hawana haja na nyie.

Nashangaa mtu analalamika wakati kuna benki kibao ndogo na zinakupa huduma zote kama crdb au zaidi. Siku hizi kuna mobile banking zinazotolewa na bank nyingi hata zile ndogo. Kwa nini mnakaa CRDB?

Ukiendelea kukaa, tulia waendelee kukufaidi na usilalamike make ni uzembe

mkuu hapo unakosea.....
tutahama vipi wengine waajiriwa hivyo benki bado kuaminika sana na serikali
Lakini kwanini watuibiee????

SP
 
Nilishasema hapa siku moja uzalendo kamwe hautaletwa na makampuni ya nje kwanza inapaswa makampuni ya ndani yaoneshe uzalenzo! nasikitika siku hizi tunashindwa kutofautisha kampuni la nje na la ndani wote wamejikita kutafuta overprofit kwa kumuumiza mwananchi haijulishi kampuni za simu au laa! mfano mzuri kampuni za sukari zinazalisha sukari nchini zinauza 2000 kwa kilo moja wakati za nje zinauza 1600 mtaani
mara nyingine mi natamani hata bora makampuni ya nje tu tujue moja tunaibiwa kuliko kuumizwa na watanzania wenzetu hebu fikiri mtu anaelipwa mshahara laki mbili bank si atachukua laki na nusu kunakoelekea kwa ajili ya uhujumu huu unaofanyika wa taasisi binafsi

Naungana na ww hapo kwenye sukari mkuu. bora watu wa nje walete tu sukari yao.
 
Hata Mimi nmesikia rafiki yangu analalamika kuwa naye kaibiwa.Kwa kweli sio vizuri maana Tumewaamini ili muhifadhi pesa zetu alafu mnatuibia acheni huo mchezo

Mi pia nimewahi kuibiwa mkuu na hao CRDB . Wapuuzi kweli
 
Mwaka huu tutaona mengi. Nasubiria BOT watangaze noti mpya....ni mwaka wa uchaguzi....
 
Hiyo benki ina wenyewe sio watu km nyie mnaolalamikia sh 500m wkt unakatwa pesa nyingi sana tigo pesa mpesa na airtel money transactions.
 
Mtetezi wa wanyonge alishazikwa Butiama. Waliobaki ni wapiga mabao hata mlie vipi hawatawasikiliza kwasababu wao hawaoni machungu ya maisha. After all raha zote za maisha wanazozipata na familia zao ni jasho la masikini wa nchi hii. Ninyi si mnaona wanavyogawana mabilioni kwenye lumbesa, sandarusi na maboksi na nyingine kupelekwa hadi magogoni? Hawa watakuwa na uchungu na ninyi kweli?!
 
Back
Top Bottom