CRDB bank acheni ubabaishaji mnatutesa

CRDB bank acheni ubabaishaji mnatutesa

Hakyanani wapuuuzi sana,na ukiwapigia customer care wao,..wanajibu kama hawataki kufanya kazi,haswa wenye jinsia ya kike...pumbavu zenu sana,shenzi kabisa...hela zangu halafu wanaleta ujinga na upumbavu...
 
Hmmm ya kweli hayo?

Wengine tushazoea kuletewa tena kupitia njia ya barua.

Muda wa kuisha tu ukikaribia unatumiwa kadi yako mpya.

Uamuzi wa kui activate unakuwa wako. Ukitaka unasubiri hadi ya zamani inamaliza muda wake au ukitaka unai activate hiyo mpya na mara moja hiyo ya zamani inaacha kutumika/ kufanya kazi.

Hakuna hassles kabisa.

Ni ya kweli kabisa Nyani Ngabu, tena unatakiwa ujaze form uambatanishe na picha. Benki ya nmb ndio wanajitahidi kwani kadi yako ikiexpire ukienda siku hiyo hiyo unapata nyingine.
 
NMB ndio baba lao kwa sasa wako very serious na kazi na wanaheahimu sana wateja...wamebadilika na wameingia mpaka kwenye mfumo wa visa cards.
 
Mi ndo maana nimejiunga na hawa wakaburu tu.
 
sio crdb tuu mpaka nmb,nilikutana na jamaa yangu maeneo ya tazara akaseme kamaliza nusu na robo ya mji mzima kutafuta hela kote kakosa hapo alikuwa safarini kwenda sehemu ya mwisho ambayo ilikuwa mlimani city.
 
Bora uwe kama Mimi ninayeweka hela kwenye kibubu.
 
Hawa jamaa hawafai Jumamosi nilienda k/koo uhuru na Lumumba nikamalizia na Segerea sheli zikawa hazifanyi kazi nikarudi home jumapili nikaenda tena Segerea shell chafu, Tabata reli (sheli),Ubungo Oilcom hapo ndo kabisaaaaaa sasa sijui nirudi enzi za mababu zetu kuchimbia hela chini ya ardhi maana ishakua shidaaa.

Na mara nyingi ATM ya Segerea Sheli weekend huwa haina hela
 
Hiyo SIMBANKING nayo ni tatizo... Kila saa ina tatizo na ukishapiga ile namba ya sim banking hatakama hujapata huduma VODA wanakulamba fasta... Ukijaribu mara kadhaa voda wanaendelea kulamba salio lako mpaka unakosa hela ya kuangalizia salio. Na ukifanikiwa kuingia sim banking nao hao CRDB wanakulamba kama kawa... Yaani ni kwamba unapigwa kila idara.. Voda wanakuumiza CRDB wanakuumiza... Dah mi saa zingine sionagi umuhimu wa hizi huduma.. Huwa naona zimekaa kiwizi wizi sana
Tena hii ndo haifai unaweza kuhamisha hela leo transaction ikaja kukamilika baada ya wiki moja au zaidi
 
Back
Top Bottom