Swali bila job description ni kubahatisha kuwinda kizani.
Job description ita stick kwenye objectives na priorities za taasisi hiyo.
Kama nilivyosema mwanzo, swali halina jibu moja.
Ila wakikuuliza unawezaje kuboresha huduma za IT utawajibuje?
Mimi ningependa kuona serikali na taasisi zake/ mashirika yake wanakuwa wawazi zaidi na waongeze kutoa meaningful data kwa wananchi, sio tu kwenye websites, bali hata in downloadable format.
Mfano halisi ni matokeo ya Form Four yaliyotolewa hivi karibuni.
Tunajua nchi yetu ina matatizo ya internet connectivity, baraza la mitihani walitakiwa kutoa ki file kama hiki hapa
Downloading: CSEE2012.zip - Uploadingit
Kidogo tu ambacho mtu anaweza kuki download kwenye laptop yake kwa dakika mbili tatu akiwa kwenye internet cafe, halafu aka disconnect akiwa na data za matokeo ya nchi nzima kwenye computer yake, bila kuhitaji kuwa na internet connection.
Lakini tafuta file kama hilo kutoka NECTA, huwezi kukuta. Inaonekana watu wa IT NECTA hawako practical.
Kwa hiyo kuna watu wengine wanataka kuzidadavua hizi data, tusiishie kutaka websites tu, tunataka tools za data analysis tuone patterns ambazo kwa juu juu hatuzioni.
Huu ni mfano mmoja tu wa unavyoweza kupeleka usaili na kuonyesha una kitu cha kuchangia.
Lakini kuelewa zaidi nini kinatakiwa angalia job description. Inawezekana wao priority yao ikawa security zaidi kuliko transparency na wewe uki emphasize transparency ukawapeleka kusiko.