Wasusujane
Member
- Mar 25, 2011
- 18
- 6
Wanajamvi katika pita pita zangu leo hapa jijini Mwanza, nikawa nimepunzika Gold Crest Hotel, Mara nikasikia zogo wadada watatu nikaambiwa wanatoka baraza la habari MCT na UTPC, taasisi hizo kwa pamoja zimeandaa maadhimisho ya Siku ya haki ya kujua Duniani (The right to know day) yanayofanyika Mwanza kitaifa jijini Mwanza.Taasisi hizo zilifanya booking katika ukumbi wa Nyerere Gold Crest wiki tatu zilizopita, lakini Clouds na shughuli ya wanayoitangaza sana ya fursa wakafanya booking jumanne wiki hii, lakini ndiyo walopewa ukumbi.
Kulikuwa na patashika nzito wale wadada wakiwalaani wafanyakazi we hotel na njama chafu za clouds kufanya uhuni huo kwa kuwa wamewaalika manaibu mawaziri Makamba na Masele kwenye Semina hiyo ya fursa,, shughuli zote zinafanyika Jumamosi tarehe 28 Septemba, nilivyomaliza kwa wine kangu nikaondoka, najiuliza hivi clouds umafia hata kwenye taasisi zenu, nyie nao si chombo cha habari mnapaswa kushirikiana na wanataaluma wenzenu?
Lakini kanisikitisha Meneja wa Hoteli hiyo nimejua jina moja anaitwa Kimario, yaani alikuwa anawajibu dry wale wadada mmoja nusura washikane, niliondoka nikaacha mzozo unaendelea sijui umeishaje, lakini clouds walishanza kupamba ukumbi, kaaaaaaaz kweli kweli!
Kulikuwa na patashika nzito wale wadada wakiwalaani wafanyakazi we hotel na njama chafu za clouds kufanya uhuni huo kwa kuwa wamewaalika manaibu mawaziri Makamba na Masele kwenye Semina hiyo ya fursa,, shughuli zote zinafanyika Jumamosi tarehe 28 Septemba, nilivyomaliza kwa wine kangu nikaondoka, najiuliza hivi clouds umafia hata kwenye taasisi zenu, nyie nao si chombo cha habari mnapaswa kushirikiana na wanataaluma wenzenu?
Lakini kanisikitisha Meneja wa Hoteli hiyo nimejua jina moja anaitwa Kimario, yaani alikuwa anawajibu dry wale wadada mmoja nusura washikane, niliondoka nikaacha mzozo unaendelea sijui umeishaje, lakini clouds walishanza kupamba ukumbi, kaaaaaaaz kweli kweli!