KERO Chuo Kikuu Huria (Open University) hawanipi ushirikiano ninapoulizia kuhusu kufanya research

KERO Chuo Kikuu Huria (Open University) hawanipi ushirikiano ninapoulizia kuhusu kufanya research

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Naelekea Mwaka mmoja tangu nimemaliza masomo, ila nilibakiza research hapo Chuoni (Chuo Kikuu Huria). Nilipata kazi Uganda, kwahiyo nikaamua kubadilisha sehemu ninayotakiwa kufanya research yangu kuwa Uganda iwe rahisi zaidi.

Ajabu, ni Mwaka sasa, simu hazijibiwi, e-mails hazijibiwi, Ma-CR hawatoi ushirikiano wa kutosha, halafu huku Watu tunakosa kazi kiutanitani hivi hivi, kwasababu hakuna atakayekuajiri bila matokeo kamili (naishia kutumia cheti cha Diploma).

Hawa watu wanatukosea sana, yani sana.

Watu tunachakalika kutafuta ajira Botswana, South Africa halafu tunaharibiana vitu vidogo. Kwani tumewakosea nini hawa walimu wa pale Huria.

Ila ningejua nisingekanyaga hiki chuo, dharau zimezidi sana.

Serikali iboreshe mazingira ya Wanafunzi wanaofanya utafiti kwani hii siyo mara ya kwanza kuona malalamiko ya aina hiyo, kuna wengangu wengi tu ambao wameshalalamika mara nyingi bila hatua kuchukuliwa, inaonekana ni "biashara" ya kawaida kwa Wasimamizi kutengeneza mazingira hayo.

Pia soma:
~
~ Serikali iangalie walimu wanaosimamia somo la Utafiti (Research) OPEN University, kuna mmoja ipo siku kitamkuta kitu
~ Ucheleweshwaji wa matokeo chuo kikuu huria(OUT)
~ Barua ya Wazi kwa Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
~ Madai ya Chuo Kikuu Huria (OUT) kutolipa Watumishi stahiki zao, Chuo chatoa ufafanuzi
 
Wakati unabadilisha sehemu unayotakiwa kufanyia research uliwasiliana na msimamizi wako? Mara ya mwisho kuwasiliana na msimamizi wako ilikua lini?
 
Kwakweli uongozi wa OUT unatakiwa ujitafakari sana...malalamiko yameshakuwa mengi. Na hakuna chcht wanafanya. Jamani tunateseka sana wanafunzi wa huku. Tunalazimishwa kulipia kusoma. Yani ulipe ada bado mwalimu akupigie simu sijui nipe kiasi hiki nije kukufundisha mkoani kwako..mara sijui nunua kitabu...yani ukijifanya kukaza shingo ndugu kuhitimu utapasikia kwa wenzio. Rushwa imezidi sana OUT. Natamani mama avunje uingozi wote kuanzia mkuu wa chuo maana malalamiko ni mengi lkn hakuna hatua yyt isliyowahi kuchukuliwa....aisee wahusika tusikieni...tusaidieni
 
Huyo atakuwa ni Abdul Kilima, yule dogo anajikuta sana
Ninamtafutia dawa yake asipobadilika au labda nisimalize masters yangu pale
 
Wakati unabadilisha sehemu unayotakiwa kufanyia research uliwasiliana na msimamizi wako? Mara ya mwisho kuwasiliana na msimamizi wako ilikua lini?
Wewe mtu anakwambia email hazijibiwi wala simu hazipokelewi unafikiri ni email na simu za nani sasa kama sio wasimamizi???
 
Wewe mtu anakwambia email hazijibiwi wala simu hazipokelewi unafikiri ni email na simu za nani sasa kama sio wasimamizi???
Kwahiyo unataka kutuaminisha kwamba tangu ameanza chuo mpaka anabakiza research hajawahi wasiliana na uongozi wala hao ma CR? Huyo hajafuata taratibu husika na ndio maana niliuliza hivyo. Course works na mitihani alifanyaje?
 
Naelekea Mwaka mmoja tangu nimemaliza masomo, ila nilibakiza research hapo Chuoni (Chuo Kikuu Huria). Nilipata kazi Uganda, kwahiyo nikaamua kubadilisha sehemu ninayotakiwa kufanya research yangu kuwa Uganda iwe rahisi zaidi.

Ajabu, ni Mwaka sasa, simu hazijibiwi, e-mails hazijibiwi, Ma-CR hawatoi ushirikiano wa kutosha, halafu huku Watu tunakosa kazi kiutanitani hivi hivi, kwasababu hakuna atakayekuajiri bila matokeo kamili (naishia kutumia cheti cha Diploma).

Hawa watu wanatukosea sana, yani sana.

Watu tunachakalika kutafuta ajira Botswana, South Africa halafu tunaharibiana vitu vidogo. Kwani tumewakosea nini hawa walimu wa pale Huria.

Ila ningejua nisingekanyaga hiki chuo, dharau zimezidi sana.

Serikali iboreshe mazingira ya Wanafunzi wanaofanya utafiti kwani hii siyo mara ya kwanza kuona malalamiko ya aina hiyo, kuna wengangu wengi tu ambao wameshalalamika mara nyingi bila hatua kuchukuliwa, inaonekana ni "biashara" ya kawaida kwa Wasimamizi kutengeneza mazingira hayo.

Pia soma:
~
~ Serikali iangalie walimu wanaosimamia somo la Utafiti (Research) OPEN University, kuna mmoja ipo siku kitamkuta kitu
~ Ucheleweshwaji wa matokeo chuo kikuu huria(OUT)
~ Barua ya Wazi kwa Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
~ Madai ya Chuo Kikuu Huria (OUT) kutolipa Watumishi stahiki zao, Chuo chatoa ufafanuzi
Nipe namba yako ya simu, au E-MAIL yako (Inbox) nikuunganishe na wahusika.
 
Kwahiyo unataka kutuaminisha kwamba tangu ameanza chuo mpaka anabakiza research hajawahi wasiliana na uongozi wala hao ma CR? Huyo hajafuata taratibu husika na ndio maana niliuliza hivyo. Course works na mitihani alifanyaje?
Niko open u nafanya masters .... niishie kusema huyu mlalamikaji yuko sahihi .... madudu ni mengi
 
Niko open u nafanya masters .... niishie kusema huyu mlalamikaji yuko sahihi .... madudu ni mengi
Hata mimi nafanya masters OUT, sasa sijajua labda ni kwa upande wenu ila naona kama Kuna vitu vingine vya kufikirisha sana.
 
Back
Top Bottom