Chuo cha utapeli Tabata Magengeni

Chuo cha utapeli Tabata Magengeni

Airun

New Member
Joined
Feb 10, 2013
Posts
2
Reaction score
1
Kuna chuo kinaitwa TANZANIA AVIATION UNIVERSITY COLLEGE kipo Tabata Magengeni Dar es Salaam kina husika na maswala ya anga, kwanza hakina hadhi ya kuwa chuo kikuu cha anga Tanzania, pili hakina ma instructor (waalimu) wenye hadhi na vigezo vya uana anga, tatu kiko mazingira hatarishi kwa wanafunzi chuo cha anga kinatakiwa kiwe around airport ili wanafunzi wasome kwa vitendo na nadharia sasa badala ya kuona ndege wanafunzi wanaona walevi na mwisho kabisa hakijasajiliwa yani kina leseni feki na hata katika mtandao kinaonekana kimefungwa na hakiruhusiwi kusajiliwa tena maana hakina hadhi sasa wazazi kuweni makini chuo hakina future watoto wameenda kukua tuu na kuna vigogo wameshikilia ndo maana hakifungwi. Mwanzo kilikuwa airport kikafungwa sasa hivi wamebadilisha jina wamekileta Buguruni kuweni makini watanzania.
 
Imekaa kiudaku lkn! Vp ni chuki binafsi!!? Au wamekufukuza kazi!!
 
Si udaku kuna ukweli hapo, as a desperate parent just be careful
 
Chuo kikiwa karibu u/ndege kama hakifundishi vizuri ndo nini? Hapo walipo wanatumia masaa mangapi, kwenda uwanja wa ndege kama Wanahitaji kujifuza kwa vitendo. hii mada hajakamilika.
 
Ni kweli vyuo vingi sana navyovijua Mimi Kama cha emirates,etihad,Qatar airways nk,vipo maeneo ya airport na masomo Yao mengi ni ya vitendo sio kuandika notes,siku hizi vyuo vingi vikubwa vya mambo ya anga vinamilikiwa na airlines na vipo airport,sisemi vyote bali nasema vingi,nilisoma kidogo pale emirates aviation college Dubai ,hivyo naelewa kwa nini vinatakiwa view airport,pale kuna ndege maalumu kwa ajiri ya kujifunzia...sasa sina uhakika Kama hicho tajwa hapo juu kipo hivyo.
 
Kwa mujibu wa mkuu wa chuo hicho akikinadi katika mahojiano na mtangazaji wa TBC1,notes wanafunzi huzipata kwa kutegemea "wikipedia".
 
Kuna chuo kinaitwa TANZANIA AVIATION UNIVERSITY COLLEGE kipo tabata magengeni dar es salaam kina husika na maswala ya anga kwanza hakina hadhi ya kuwa chuo kikuu cha anga Tanzania pili hakina ma instructor(waalimu) wenye hadhi na vigezo vya uana anga tatu kiko mazingira hatarishi kwa wanafunzi chuo cha anga kinatakiwa kiwe around airport ili wanafunzi wasome kwa vitendo na nadharia sasa badala ya kuona ndege wanafunzi wanaona walevi mwaisho kabisa hakijasajiliwa yani kina leseni feki na hata katika mtandao kinaonekana kimefungwa na hakiruhusiwi kusajiliwa tena maana hakina hadhi sasa wazazi kuweni makini chuo hakina future watoto wameenda kukua tuu...na kuna vigogo wameshikilia ndo maana akifungwi mwanzo kilikuwa airport kikafungwa sasahiv wamebadilisha jina wamekileta buguruni kuweni makini watanzania....

kabla hujaanza kuzungumza jiulize....maswali haya
udsm...kuna kozi ya mining and mineral proccessing je wako karibu na migodi?
i.f.m ...kuna kozi ya banking and finance je kuna benki pale i.f.m?
udom ,,kuna kozi ya petroleum engineering je kuna petrol pale?
udsm..kuna kozi ya water resorces je kuna bahali paleee
c.b.e kuna kozi ya indurial .... je kuna kiwanda pale......

ukipata jibu jiulize tuna mitalaaaa.....
 
kwani wanawalazimisha wanafunzi kwenda acha hizo weweeee! kuna vyuo vimesajiliwa na havina walimu au uanjitoa ufahamu. Acha watu wajiajiri. hata mimi nikipata mtaji ntaanzisha changu mimi sitatoa cheti nitatoa elimu. nimekutana na madereva wengi wana leseni lakini hawajui hata kuendesha gari je ndio kusajiliwa unakokuongelea?
 
Back
Top Bottom