Chunusi: Chanzo, tiba na jinsi ya kuepukana nazo

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,320

Wapo watu ambao wanasumbuliwa na tatizo sugu la chunusi, madoa doa na kuharibika kwa ngozi. Ingawa chunusi hizi mara nyingi hutikea usoni, wakati mwingine hutokea pia katika maeneo tofauti ya mwili.

Kwa bahati mbaya baadhi ya waathirika wa chunusi wamejikuta wakitumia madawa mengi bila matibabu, hata mara nyingine kuharibu kabisa ngozi zao.

Habari njema ni kwamba, imegundulika kwamba matatizo mengi ya ngozi yanayotokea usoni, hasa chunusi ni kwa sababu ya aleji (mzio) ya vyakula tunavyokula, au matatizo mengine yatokanayo na vyakula vya protini. Kwa bahati mbaya, madaktari wengi wa aleji hawawezi kugundua kama chunusi ulizo nazo ni aleji kwa sababu wanafanya allergy test kwenye ngozi, wakati aleji yenyewe iko ndani tena kwenye kiungo specific na yanayoonekana nje ni madhara tu

Vyakula mabavyo vimetajwa kuwa huweza kusababisha allergy ni;
- Maziwa

- nyama
- mayai
- samaki
- kuku
- wadudu wanaoliwa kama senene, kumbikumbi nk

Hata hivyo sio rahisi kwa mtu mmoja kuwa na allergy ya hivyo vitu hapo juu vyote, na hivyo haimaanishi kama una hilo tatizo basi ndio mwisho wako wa kupata animal protein hapana, ingawa unaweza kuwa na allergy ya kimoja au baadhi ya hivyo.

Je, utagunduaje kama chunusi ulizo nazo zinasababishwa na allergy ya kimoja au baadhi ya vitu nilivyotaja hapo juu?
Kumbuka, unaweza kutembelea hospitali zote wakafanya allergy tests zote na wasione tatizo, lakini allergy bado iko pale pale. Kwa maana hiyo, namna pekee ni kwa wewe mwenyewe kujifanyia test kama ifuatavyo;

1. Acha kabisa kutumia vyakula vyote vilivyotajwa hapo juu kwa wiki 3. Ina maana kwa wiki hizo 3, utakuwa vegetarian..lol

2. Kama hautaona mabadiliko yeyote, then utagundua kuwa tatizo lako sio allergy hivyo endelea na maisha kama kawaida, huku ukitafuta matibabu mengine.

3. Kama utaona mabadiliko ya kupungua au kuisha kwa tatizo, then mshukuru Mungu wako, maana tatizo lako linaelekea kupata ufumbuzi. Cha kufanya hakikisha tatizo limeisha kabisa ndani ya hizo wiki tatu, au ukiona limepungua halijaisha, then subiri hadi liishe then nenda kwenye step 4 hapo chini.

4. Tatizo likiisha, anza kurudisha kimoja kimoja, ukianza na mayai. Kula mayai 1-2 kila siku kwa siku 7-10 halafu jiangalie kama tatizo lipo. Kama limerudi, acha mara moja kutumia mayai, na subiri hadi liishe kisha ndipo uende step 5 hapa chini.

5. Tumia maziwa (kumbuka hii ni siku 10 tangu uanze kutumia mayai). Unaweza kuendelea kutumia mayai (kama hayakuleta tatizo katika step 4), kwa rate ya kawaida uliyokuwa umezoea zamani. Kunywa takribani 200ml hadi 500ml kwa siku kwa siku kumi. Hapa naongelea maziwa ya ng'ombe. Kama unatumia maziwa ya mnyama mwingine, then nayo yawe tested katika step tofauti.

6. Endelea na vyakula vingine vilivyobaki, ukirudisha kimoja kimoja kila baada ya siku kumi, hadi utakapogundua ni kipi kati ya hivyo hapo juu kinachokusababishia tatizo

NB: 1. Nyama ya ng'ombe, mbuzi, nguruwe nk ziwe tested tofauti. Nina rafiki yangu anaathiriwa na nyama ya ng'ombe tu sio kitimoto wala mbuzi!

2. Kwa akina dada/mama, tofauti na chakula pia tatizo linaweza kuhusiana na proteins zilizomo kwenye semen za mwanaume/wanaume, na bahati mbaya sana ni kwamba unaweza kuathiriwa na semen ya mwanaume mmoja na sio mwingine! Kivumbi kitakuwa pale unapoathiriwa na semen za mumeo, mbaye kumwambia mtumie condom sio rahisi... Kama tatizo ni hili, hapa inabidi mpime ama kukubali kuishi nalo, au uwe unatumia anti-ellergens kila mnapokutana, lambo ambalo hakuna Dr yeyote duniani atakushauri ufanye.

Kama hujaelewa hiyo regime hapo juu, unaweza ukauliza na kupata ufafanuzi mzuri zaidi...


Additionally,
matatizo ya ngozi usoni yanaweza kukupa ishara ni kiungo kipi cha mwili wako kina mataizo



===========
Vipele hivyo hutokea wakati vishimo vya kupitisha jasho katika ngozi vinapozibwa kwa mafuta au seli za ngozi zilizokufa au wadudu, yaani bakteria.


Kwa lugha ya kidaktari, chunusi inaitwa ‘Acne Vulgaris.’ Ni ugonjwa wa ngozi unaomuathiri binadamu kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano, nchini Marekani pekee, inaelezwa kuathiri watu zaidi ya milioni 17.


Chunusi inaweza kujitokeza katika umri wowote wa binadamu, lakini ina kawaida ya kuwaathiri sana vijana, hasa katika umri wa balehe (adolescence).


Dawa 20 za asili
1. Barafu; Hii ni dawa inayoweza kupunguza chunusi zionekane ndogo na kupunguza madhara yanayosababishwa.

Namna ya kutumia barafu kutibu chunusi ni rahisi na haraka zaidi. Chukua kipande cha barafu na ukipitishe sehemu zilipo na chunusi mara kadhaa kwa wastani wa dakika tatu hadi tano.

Pia, mwenye chunusi ukumbuke kusafisha vizuri uso wako, kabla ya kuanza kupitisha hiyo barafu kwenye uso wako.

2. Kitunguu swaumu; Hii inajulikana kama kitu cha kushangaza katika tiba. Huko Mashariki ya mbali, inafananishwa na miujiza.

Hiyo ni kwa sababu ina nguvu za kuua bakteria mbalimbali na kuzuia magonjwa, ikiwemo kutibu chunusi. Kuna namna mbili ya kutumia kitunguu swaumu katika tiba ya chunusi.

Namna ya kwanza ni kukitumia kitunguu swaumu kwenye vyakula vinavyopikwa kila siku na namna ya pili, ni kukitwangwa kitunguu swaumu na kukipaka moja kwa moja katika sehemu yenye chunusi.

Mbali na harufu yake isiyopendwa na wengi, kitunguu swaumu, kina uwezo wa kumpa mtu afya na urembo unaouhitaji.

Kinasaidia kupunguza ukubwa wa chunusi. Hata hivyo, unahitajika umakini, kwani kitunguu swaumu kinaweza kuunguza ngozi yako, usipokuwa makini na ili kuepuka, jaribu kuchanganya kidogo na maji baada ya kukitwanga, ili kupunguza makali yake.

3. Limau; Dawa nyingine nzuri kwa ajili ya chunusi usoni na mwilini ni limau. Hiyo inapatikana kwenye vyakula vingi, mathalan haikosekani kwenye lishe ya supu au mapishi kama ya samaki.

Limau ina kiasi kingi cha vitamini C, inayoweza kutumika kama antibaiotiki inayozuia kuongezeka na kukua bakteria wanaosababisha chunusi. Pia, ina tindikali maalumu inayohamasisha chunusi kutoka katika ngozi.

Kinachotakiwa kufanywa ni kwamba, mtu anakata limau katika pande mbili au nne na kisha anapaka maji yake taratibu kwenye chunusi, kwa wastani wa dakika 10, kisha anajisafisha na maji safi.

Tindikali katika limau inaweza kuzidhuru seli zilizopo juu ya ngozi yako, hivyo tumia dawa hiyo mara moja au mbili kwa wiki na siyo kila siku.

Vitamini C iliyomo kwenye limau husaidia kukinga mwili dhidi ya magonjwa mengi, sababu ndiyo vitamini inayosaidia kuongeza kinga ya mwili.

Kinga ni bora. Hivyo, inaaswa kutumia lishe ya vitamini C kila mara au kunywa juisi ya limau kila siku, ili kuuweka mwili katika afya bora zaidi muda wote.

4. Mshubiri (Alovera); Mshubiri au Alovera kama ilivyozoeleka na namna nzuri kwa wote wanaotaka kubaki na ngozi nyororo na ya kupendeza kila siku.

Unafanyaje? Chukua kipande cha mshubiri ‘freshi’ na ukikate, kisha chukua maji yake na kupaka moja kwa moja usoni huku ukijisugua polepole kwa muda wa kati ya dakika 15 hadi 20, kisha kujisafisha na maji safi.

Dawa hiyo inatumiwa mara mbili hadi tatu kwa wiki. Hiyo ndiyo njia rahisi ya kutibu chunusi bila kukuacha na madhara mengine mabaya.

5. Dawa ya mswaki; Dawa ya mswaki au dawa ya meno ni nyenzo nyingine ya asili mtu anaweza kutumia kujitibu chunusi. Hii inatumika usiku tu.

Pakaa kiasi fulani cha dawa hiyo kwenye chunusi iliko na kulala nayo, kisha asubuhi ajisafishe na maji safi. Hilo linaloaswa kufanyika kila baada ya siku moja, hadi mgonjwa wa chunusi anapopona.

6. Tango; Hilo ni tunda, mboga pia chanzo kizuri cha kiini cha potasiamu na vitamini nyingi ambazo zina kazi muhimu katika ngozi ya binadamu. Ina kawaida ya kuifanya ngozi ionekane laini na inayopendeza.

Tango ni mojawapo ya dawa kamili za kutibu chunusi na rahisi katika kulitibu chunusi.

Unaanza kwa kulikata tango katika vipande vidogo mfano wa slesi na kisha inabandikwa juu ya ngozi yenye chunusi. Ukumbuka kwanza kusafisha kwanza yako, kabla ya kubandika hizo slesi za tango.

Namna nyingine ni ya kusaga tango, upate juisi yake na uchanganye na sukari na kisha jisuguwe nazo kwenye ngozi yenye chunusi kwa dakika walau mbili hadi tatu na unamalizia kwa kujisafisha na maji safi.

7. Asali; Asali mbichi ya asili ni dawa nzuri sana ya kutibu chunusi. Ina antibaiotiki ya asili inayosaidia kupunguza ukubwa wa chunusi na maumivu yake.

Pia, asali inaweza kuzuia ngozi isipatwe na maambukizi mengine, ambayo yangeweza kusababisha matatizo kwenye ngozi au makovu.

Hivyo, asali inachukuliwa kama sehemu ya dawa za asili nzuri zinazotibu chunusi.

Inavyotumiwa, inaanza kwa kusafisha ngozi vizuri na maji ya vuguvugu na kisha jipake asali moja kwa moja kwenye sehemu yenye chunusi. Inaacha kwa dakika 30 na kisha jisafishe na maji safi ya vuguvugu.

Dawa hiyo inatumika ama mara mbili au tatu, ndiyo inakuwa katika nafasi nzuri ya kutoa majibu sahihi ya kitabibu.

8. Baking Soda; Moja ya sababu za kutokea chunusi katika ngozi ni kuwepo uchafu juu ya ngozi. Matumizi ya ‘baking soda’ ni moja ya njia rahisi ya kusafisha taka hizo, hivyo kuifanya ngozi ipumue vizuri.

Kimsingi, mtu akiwa na chunusi, afikiri inasaidia kubandua seli za ngozi zilizokufa na kufanya mafuta yaliyozidi kuondoka.

Ni rahisi zaidi kutumia ‘baking soda’ kutibu chunusi. Hatua zake, inaanza na kuchukua ‘baking soda’na kuichanganya kidogo na vijiko vinne vidogo vya maji au maji ya limau na mchanganyiko huo unapakwa moja kwa moja kwenye chunusi, kisha inaachwa kwa wastani wa dakika 10, ndio mhusika anajisafisha na maji ya moto.

9. Mvuke; Huo unasaidia kusafisha ngozi. Ni rahisi sana kutumia mvuke kutibu chunusi.

Mchakato wake unaaza kwa kuchemsha maji kwenye chombo kilichofunikwa na inaachwa sufuria nafasi kidogo ya mvuke kutoka.

Mtu anachofanya anachukua taulo kidogo na kisha anajifunika usoni, huku akisogelea karibu na mvuke unapokea na kuruhusu umpate kwa mbali.

Baki hapo kwa dakika tano hadi 10, huku mtu akiwa umetulia au kitaalamu hutajwa ‘relaxed.’Huu mvuke utakusaidia pia kujisikia mtulivu na kukuondolea mfadhaiko wa akili.

Mwishoni wake ni kwamba mtu ajisafishe uso wake na maji ya baridi.

10. Papai; Dawa nyingine madhubuti ya chunusi ni papai. Tunda hilo ni moja ya matunda yanayotumika kwa ajili ya urembo kwa kinamama.

Hatua zake ni papai inachukuliwa na inachanganywa na asali kidogo, linakorogwa kidogo na kisha kujipaka sehemu yenye chunusi kusugua kwa dakika 15.

Baada ya hapo, mtu anatakiwa kujiosha usoni na maji ya moto na baada ya kumalizia, arudie kujisafisha na maji baridi.

Hilo linatakiwa kufanyika kwa wastani wa mara mbili mpaka tatu kwa wiki.

11. Aspirin: Hii ni dawa. Inatajwa kuwa moja ya dawa nzuri za chunusi.

Inachofanyika ni kuchukuliwa ama vidonge viwili au vitatu vya aspirin vinavyotwangwa kupata unga wake, kisha inaongezwa maji kidogo ili kupata mithili ya uji mzito unatokanao na mchanganyiko wa dawa na maji.

Kisha pakaa mchanganyiko huo moja kwa moja kwenye sehemu yenye chunusi kwa wastani wa mara 10 hivi, kisha jisafishe kwa kutumia maji safi.

Hilo likifanyika kwa wastani wa mara moja kwa wiki, linakuwa lenye mafanikio.

12. Ute mweupe wa yai; Hiyo inaweza kuchukuliwa kama njia rahisi na isiyo na gharma katika kutibu chunusi.

Kwa mujibu wa wanasayansi, kutumia mchanganyiko wa ute mweupe wa yai na maji ya limau, ni namna nzuri ya kutibu chunusi.

Changanya ute mweupe wa mayai matatu na kijiko kidogo kimoja cha maji ya limau na ukoroge vizuri. Pakaa mchanganyiko huo usoni na uache kwa dakika 15, kisha jisafishe na maji ya moto.

Hilo nalo linaloshauriwa kufanywa kati ya mara moja au mbili kwa wiki.

13. Siki ya tufaa (Apple vider Vinegar); Imo katika dawa zinazojulikana kutibu chunusi. Ina uwezo wa kurudishia tindikali katika ngozi. Bakteria wabaya, mafuta na uchafu mwingine wataondoka juu ya ngozi inayotibiwa.

Changanya siki na maji kidogo na umwagie ndani ya kitambaa kisafi kizito na upitishe kitambaa katika sehemu yenye chunusi mara kadhaa kwa dakika 10, kisha jisafishe uso wako na maji ya baridi.

14. Chumvi na mafuta ya zeituni; Mchanganyiko wa chumvi na mafuta ya zeituni (olive oil) ni dawa nyingine inayotibu chunusi.

Mafuta ya zeituni yanadhibiti bakteria na huondoa sumu vitu ambavyo vinafanya kuwa dawa nzuri kutibu chunusi na matokeo ya chunusi.

Changanya nusu kijiko kidogo cha chai cha mafuta ya zeituni na kiasi kidogo cha chumvi katika chombo kisafi. Safisha vizuri uso wako.

Kisha jipake mchanganyiko huu kwenye uso wako na uache kwa dakika 10 hivi. Mwisho jisafishe vizuri na maji ya uvuguvugu.

15. Mdalasini na asali; Mchanganyiko wa mdalasini na asali ni dawa nzuri ya kutibu chunusi.

Changanya asali vijiko vikubwa viwili na mdalasini ya unga kijiko kikubwa kimoja na kisha safisha vizuri uso wako.

Hatua inayofuatia ni kupakaa mchanganyiko huo kwenye uso usiku na asubuhi na baada ya hapo unasafisha vizuri uso wako.

16. Binzari, maziwa na asali; Hii ni jozi ambayo utengenezaji matumizi yake yanahitaji Binzari ya unga, maziwa fresh, asali, bakuli na kijiko cha chai

Hatua kwa hatua namna ya kutumia:

a)Weka kijiko kidogo kimoja cha binzari ya unga ndani ya bakuli na kisha ongeza kijiko kidogo kimoja cha asali ndani yake.

Baada ya hapo, ongeza tena kijiko kidogo kimoja au viwili vya maziwa fresh na uchanganye vizuri mchanganyiko huo upate uji mzito.

Hatua inayofuata ni kuipaka mchanganyiko huo polepole kwenye sehemu yenye chunusi na baada ya kati ya dakika tano na saba hivi na ujisafishe uso wako. Lifanye hilo kati ya mara mbili au tatu kwa wiki.

17. Uwatu (Fenugreek); Ni dawa nyingine ya asili inayotumika kutibu chunusi, unaoondoa sumu na maambukizi mbalimbali.

Hatua chache za kutibu chunusi kwa kutumia uwatu ni kwamba, chukua kijiko kidogo cha unga wa mbegu za uwatu na ongeza maji kidogo kupata uji mzito na kisha pakaa mchanganyiko huo katika sehemu yenye chunusi.

Pili, iache hiyo kwa dakika 20 au hata hadi usiku mzima na kisha jisafishe na maji safi. Hilo linaweza kufanyika kwa wastani wa mara mbili au tatu kwa wiki

18. Tumia maganda ya ndizi; Unachohitaji hapo ni kuwa tu na maganda ya ndizi yanayoandaliwa kwa kwa hatua za kumenya ndizi na ganda lake likandamizwe katika sehemu ya ndani ya ganda hilo kwenye sehemu yenye chunusi.

Hilo likifanyika, unatakiwa usubiri kwa wastani wa dakika 30 na kisha jisafishe na maji safi.

19. Parachichi na asali; maandalizi yake inahitajika kijiko kimoja cha asali na parachichi zinazoandaliwa na kutumiwa kwa hatua zifuatazo.

a) Safisha vizuri uso wako.b) Kausha na taulo au kitambaa uso wako.c) Chukua nyama ya ndani ya parachichi.d) Ongeza asali kijiko kimoja ndani ya parachichi.e) Changanya vizuri vitu hivyo viwili kupata uji mzito.f) Pakaa mchanganyiko huo kwenye sehemu yenye chunusi na kuiacha kwa wastani wa kati ya dakika 15 mpaka 20 hivi na mwisho jisafishe na maji ya vuguvugu na ujifute vizuri

20. Mtindi na asali; Hii inaelezwa kuwa dawa rahisi zaidi za kutibu chunusi.

Mahitaji yake ni: Kijiko kimoja cha asali, piakijiko kimoja cha mtindi

Unaanza kwa kuchanganya mahitaji hayo mawili vizuri na kisha kupakaa polepole mchanganyiko huo usoni.

Inapokauka, hili linarejewa mpaka mchanganyiko wote na kisha inaachwa kwa dakika 10 hadi 15 na mwisho ajisafishe na maji ya vuguvugu.

Mambo muhimu ya kuzingatia:
  1. Fanya mazoezi ya viungo kwa saa moja kila siku.
  2. Kunywa maji mengi kila siku.
3. Ondoa mfadhaiko.
4. Weka homoni sawa kama hazijakaa vizuri.
5. Kuwa msafi wa mwili wote kila mara.6. Usiziguse chunusi au kuzitoboa na mikono yako au na chochote, kuepuka makovu yasiyo ya lazima.

Vyakula vya kuepukwa na mwenye chunusi
Epuka vyakula vifuatavyo kama unasumbuliwa na chunusi kila mara, navyo ni pamoja na:

a) Vyakula vyenye mafuta sana

b) Vyakula vinavyopikwa katikati ya mafuta mengi

c) Kahawa

d) Chai ya rangi.

e) Pombe na vilevi vingine.

f) Chokoleti.

g) Popcorn.

h) Maziwa

i) Mapera

j) Vyakula vya kwenye makopo

k) Pizza.

============

Michango ya wadau:





 
Mkaa mweusi, ni ngumu sana kutoa chunusi kabisa ndani ya siku chache kama utakavyo, ninachojua mimi utapunguza tu makali ya chunusi hizo ndani ya wiki mbili kama utaconcentrate kati Tips chache zifuatazo...
  • Kwanza kama unatumia any cream usoni kwa sasa achaa
  • Nenda HS Amon nunua facial inaitwa ''Cleans up'' inauzwa 10,000
  • tafuta( asali halisi) ya nyuki isyo na chemicals,utakuwa unachanganya na kiini cha yai kila siku
  • Nunua sabuni ya ''spot removal ya nyanya, sh 3000 tu madukani
Osha uso asubuhi na jioni kwa kutumia hiyo sabuni, then ufanye facial ya clean up, facial mara moja tu kwa siku, bandika mchanganyiko wa asali na yai usoni, acha ukauka vizuri, osha uso kwa maji ya vuguvugu, usipakae oily lotion, ukimaliza tu kukaucha uso waweza paka poda

Nilishajaribu ikanisaidia kwa muda wa siku 10.
Note.. huwezi kuclear madoa yote kwa muda mfupi, itaheal pole pole.
Caution, Wapambaji ni wataalam sana, usiwe na wasiwasi wa siku yako, mpambaji ataweka make ups wala hazitaleta show mbaya siku ya harusi, usiende tu kwa mpambaji mbaya.
 
Chunusi ni matatizo ya ndani ya ngozi amabyo ama husababishwa na hormones au wingi wa mafuta mwili, kwa hivyo hakuna dawa ya kupaka inayoweza kutibu chunusi. Lakini zipo dawa na njia za kuweza kupunguza ikiwemo asali. Nyengine ni utomvu wa Alaoe vera, mafuta au cream zilizotengenezwa nayo. Wakati unatumia njia yoyote, hakikisha unawacha kabisa kula vyakula vyenye mafuta pamoja na sukari kama vile chocolates na vitu vitamu vyengine isipokuwa matunda.
 
Sijui umri wako lakini chunusi mara nyingi huwapata vijana wanaobalehe na hii ni kwa sababu wanakuwa na vichocheo aina ya androgens kwa wingi ambavyo kwa namna moja au nyingine husababisha chunusi. Pia kuna vimelea vya bacteria aina ya p. acnes, ambavyo baada ya matundu ya vinyweleo kuziba hukaa ndani ya matundu hayo kuzaliana na kusababisha chunusi kuvimba.

Matibabu sana ni usafi wa ngozi ya uso, angalau mara mbili kwa siku na sabuni yenye dawa (medicated soap), acha kupaka mafuta ya mgando usoni, acha kuminya hizo chunusi kwani husababisha zipate uambukizo wa pili wa bacteria (secondary bacterial infection) ambao watasabisha usaha na makovu makubwa usoni, usishike shike uso wako kwa mikono mara kwa mara.

Kwa upande wa dawa tafuta cream ya benzoyl peroxide (hii ni cream ya dawa ina antibacterial effect sio ya urembo), osha uso wako vizuri na ukaushe then ipake hiyo cream kwenye sehemu zote zilizoathirika na chunusi, paka mara moja au mara mbili kwa siku kutegemeana na ukubwa wa tatizo.Pamoja na hiyo cream antibiotics aina ya tetracyline hutolewa pia, zitumike kwa siku 10 mpaka wiki 2.

Chunusi zikizidi kamuone daktari bingwa wa ngozi (dermatologist) atakusaidia vizuri zaidi.
 
Pasha asali kidogo, paka usoni usiku asbh unanawa.

Pia maji ya limao yanasaidia kupunguza mafuta usoni, kamua limao kwenye maji kidogo nawa nayo.

Acha kula vitu vya mafuta kama karanga, blue band nk.

Kunya maji walau lita tano kwa siku inasaidia sana kutoa uchafu mwilini.

Ikizidi muone mtaalamu wa ngozi.
 
kama kuna vitu vilinitesa kwenye usichana wangu ni chunusi, nakumbuka mpaka dada zangu walikuwa wananiita dudu!! au wanasema mamdogo umekuwa na sura ka ganda la fenesi!!

Nilikuwa naona aibu hata kutoka na wenzangu ila namshukuru Mungu kwa sasa uso wangu u kama wa mtoto!!! ila nilichotumia hata sikumbuki maana makorokoro yote ya uso nilimaliza.
 
Utakesha sana hospitali. Hilo ni tatizo la mwili wako kushindwa kutoa uchafu mwilini. Kunywa maji ahai ya bio disc. Soma Amezcua na uwasiliane nami privately. unique
 
Let me tell you the best natural treatments for acne. These methods are also a very good alternative for the people who don't want to go through surgical treatment or the ones who cannot afford enough money for the treatment.

Virgin Coconut Oil: It is very efficient in curing skin ailments and also to lighten pigmentation. Usually your acne marks are hyper-pigmented, so you can replace your moisturizer with coconut oil in order to lighten your acne marks.

Papaya: They are commonly known for its ability to lighten skin. Papaya is an important constituent in soaps and highly effective in treatment of acne marks. You can use the fruit pulp and smear it over the mark. Now leave it like this for about half an hour and allow your skin to absorb all its nutrients.

Sandalwood Oil: It is very helpful in reducing pigmentation therefore it can be used for treating your acne marks. You could also use it as night renewal oil when you apply it over the marks and leave it overnight. It can also work as a moisturizer during the day time.

Aloe Vera: It is the latest method used now days for treatment of acne. There are many soaps and gels made of Aloe Vera which are used to heal the skin damaged by acne.

Mix Lime Juice and Rose-Water: What you need to do is to mix lime juice and rose-water every night in equal portions after you had thoroughly washed your face. Now keep it like this for 30 minutes. Wash your face again and let the pat dry. This is one of most effective natural treatments for acne.

Mix Honey and Cinnamon Powder: You can just make a paste by mixing honey and cinnamon powder. Apply this paste on your face before going to sleep and wash it the next morning you get up.

All these methods are natural treatments for acne. So they will never harm your skin or body. Plus all the ingredients you need are easily accessible and cheap.

Natural Treatments for Acne - How To Get Rid of Acne Permanently

http://www.kamusi.org/en/lookup/en?Word=acne
 
Nina rafiki yangu wa kike ambaye ana tatizo la muda mrefu sana linalomsumbua ambalo ni akikaribia siku zake za hedhi hupata pimples ambazo baada ya kumaliza hiyo hedhi humuacha na alama ambazo huwa hazitoki yaani ni za muda mrefu. Wakati mwingine hizo pimples humtokea usoni au kifuani na pia mgongoni na hizo alama hubaki katika sehemu husika na hivyo kumfanya ashindwe hata kuvaa nguo za mabega wazi kwa ajili ya makovu ya chunusi hizo. Ninashukuru Kwa yeyote ambaye ataweza kumshauri , pia madaktari tunaomba pia mtusaidie chanzo cha hizi chunusi na jinsi ya kukabiliana nazo.
 
Pole sana kaka, ukikosa msaada humu jaribu kwenda madaktari wa ngozi.
 
Hilo tatizo huwa linasababishwa kwa asilimia kubwa na kupasuka kwa 'layer' nyembamba ya ngozi (skin) inayoitwa "acid mantle".Hii huletwa na mabadiliko ya 'hormones' yanayotokea wkt wa hedhi.
JINSI YA KUJIKINGA: aepuke kula vyakula vyny mafuta sana(hasa ya wanyama),ale mboga za majani,matunda,anywe maji ya kutosha. Pia anaweza kupaka 'vinegar'(apple cider) usoni siku 7 kabla ya siku za hedhi yake.
TIBA(zikishakuwa zimetokea): atumie calamine lotion wkt wa usiku au white toothpaste wkt wa usk! Asijaribu kuvitumbua hii inachangia sana ktk kuacha makovu.
 
Pole sana mkuu, kama upo Dar, nenda pale Muhimbili Hospitali kuna Madaktari bingwa wa masuala ya ngozi wanamfanyia vipimo na kumpa matibabu!
 
Tatizo la pimples ni kubwa na linaweza kuongezwa na majaribio yeyote ya kupambana nazo. Namaanisha kuwa wapo watu wanaishia kupata madhara makubwa sana ya ngozi kwa kuajribu 'matibabu' tofauti kuondokana na tatizo la pimples.

Hivyo cha kwanza kumshauri huyo dada ni kuwa asijaribu kila anachoambiwa apake, kwani mara nyingi response inategemea na mtu binafsi, na vitu vingine vinaweza kukusababishia madhara magumu sana kuyatibu baadae.

tukirudi kwenye tatizo ni kuwa mara nyingi pimples hutokea kutokana na level ya hormones fulani hasa hasa oestrogen. Hormone (pamoja na nyingine) hii hucontrol kiasi cha mafuta yanayokuwa deposited kwenye ngozi, na yanapozidi na kushindwa kutoka, pimples zinatokea. Kabla ya kujaribu njia za kupaka vitu, namshauri ajaribu njia za asili, yaani scrubbing.

Hapa siongelei ile scrubbing ya kwenda kufanya sijui salon, ila scrubbing ya kufanya mwenyewe home. Kila baada ya siku moja, jioni akioga a-scrub kwa kutumia dodoki ikitegemea na ugumu wa ngozi. Asiogope maumivu hasa siku za mwanzo, ascrub kwa dakika tano kwa nguvu akitumia dodoki, maji ya uvuguvugu, na sabuni isiyo na dawa (kama jamaa).

Baada ya hapo apake vaseline (natural petroleum jelly), na afanye hilo kuwa zoezi la kudumu kuwa kila baada ya siku moja, akioga lazima asugue uso na maeneo mengine yote yenye pimples kwa nguvu. Akumbuke pia kuwa Vaseline ni dawa murua ya fangazi ambalo ni tatizo kubwa kwa watu wanoishi maeneo yenye joto...
 
Umri umri hii ndo jamii forum watu hawakurupuki kutoa ushauri,pili hapo S.H amon umeonana na wataalamu au wafanyabiashara? sio maneno yangu nimenukuu kutoka kwa wadau juu hapo
 
Nakushauri unywe maji kwa wingi sio chini ya glass nane kwa siku, mazoezi kidogo na chakula chako kiwe na mboga mboga zaid na matunda. Kila la heri
 
kama wewe ni mwanamke
mahitaji
1 johnsons facial scrub
2johsons facial cleanser
3johnsons toner
4johnsons day cream
5johnsons night cream utapewa na jinsi ya kutumia ukishindwa nipm

pia kunywa maji na matunda kwa wingi epuka na red meat
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…