Chopa ya Ndesamburo yaitesa CCM

Chopa ya Ndesamburo yaitesa CCM

dm2000inter

Member
Joined
Oct 27, 2010
Posts
29
Reaction score
10
Wana JF,

Kama mtakumbuka, Jumamosi ya tarehe 18.4.2015 kada wa CCM Moshi mjini, Buni Athman Ramole aliingia katika mkutano wa CCM kata ya Pasua kwa mbwembwe na kudai ameilipia helkopta hiyo hadi Oktoba.

Jana kwenye mkutano mwingine wa hadhara amekanusha helkopta ile sio ya Mzee Ndesamburo bali ni ya kampuni ya General Aviation Services na kutoa nyaraka kwenye mkutano wa hadhara aliyodai ameilipia helkopta hiyo hadi Oktoba.

Imethibitika rasmi kuwa Helkopta hiyo ni ya Mzee Ndesamburo na General Aviation ina mkataba wa kukodi Helkopta hiyo toka kwa Ndesa kila wanapopata mteja. Je, hiyo inamuondoa Ndesamburo kuwa mmiliki wa Helkopta?

Pili hebu tazameni nyaraka aliyoisambaza kwa wananchi kama ni uthibitisho wa malipo au aliomba tu bei ya kukodi helkopta?.

Tazameni uongo huu wa kada anaywtaka kuwa Mbunge wa Moshi Mjini kwa tiketi ya CCM.

Hivi anafikiri wananchi wa Moshi ni mbulula?

attachment.php
 

Attachments

  • barua.jpg
    barua.jpg
    55.3 KB · Views: 1,314
Mzee Ndesa Pesa anatengeneza $$$$ ... Muda Ukikaribia hiyo Chopper itakuwa inatekeleza majumu ya CHADEMA na UKAWA ...
 
hii ni aibu. moshi mjini ni kamji kadogo sana sidhani hata kama kanahitaji vx achana na hiyo chopa. bajaji tu yatosha kukamaliza kwa only two hours. sasa chopa ya nini hapo? kweli ccm wanatumaliza tukijiona hivi hivi.
 
hii ni aibu. moshi mjini ni kamji kadogo sana sidhani hata kama kanahitaji vx achana na hiyo chopa. bajaji tu yatosha kukamaliza kwa only two hours. sasa chopa ya nini hapo? kweli ccm wanatumaliza tukijiona hivi hivi.

Hao ndio viongozi wetu wa kyama kya mapinduusi
 
Back
Top Bottom