China yakubali utendaji wa Serikali ya awamu ya Tano ya Tanzania

Zurie

JF-Expert Member
Jul 6, 2014
1,740
4,228
Naibu waziri wa mambo ya nje wa Jamhuri ya watu wa china Guo Yezhou ambaye pia ni mjumbe wa chama cha Kikomunisti cha nchini humo ametembelea makao makuu ya chama cha mapinduzi CCM Mkoani Dodoma ambacho ni chama rafiki huku akisema nchi yake inafurahishwa na utendaji wa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli katika kukabiliana na matumizi mabaya ya fedha za umma rushwa na ufisadi

Akizungumza mara baada ya kuwasili mjini Dodoma Naibu waziri huyo wa mambo ya nje kutoka nchini China amesema Serikali ya China na Tanzania zimekuwa zikifanya kazi kwa ushirikiano mkubwa ambapo pia ametumia fursa hiyo kumtaka raisi magufuli kufanya kazi kwa kufuata misingi iliyoachwa na mwasisi wa taifa hili Hayati Mwalimu Julius Nyerere ili tanzania iweze kupiga hatua kimaendeo na kiuchumi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Alhadji Adam Kimbisa ambaye ndie aliyekuwa mwenyeji wa kiongozi huyo kutoka uchina amesema chama cha mapinduzi na Serikali yake kitaendelea kudumisha ushirikiano kati ya Mataifa hayo mawili ambao umedumu kwa muda mrefu.

Tanzania na china zina urafiki wa kudumuumedumu kwa mrefu ambapo mpaka sasa ni miaka zaidi ya miaka 49 zikishirikiana katika mambo mbalimbali yakiwemo kiuchumi,siasa, jamii na usalama.


Chanzo: itv
 
China hawajawahi kataa serikalj yoyote duniani hata ya nkurunziza waliikubali, chezea Chinese wewe
 
China hawajawahi kataa serikalj yoyote duniani hata ya nkurunziza waliikubali, chezea Chinese wewe
Kweli mkuu inabidi wasifie wanachojali nikupata rasilimali kutoka Africa kuendeleza viwanda vyao.
 
IMG-20160402-WA0043.jpg
Suala la China kuikubali serikali ya ccm hilo si h oja,labda ingekuwa uchina imetofautiana na ccm kuhusu sarakasi za awamu ya tano ndiyo tungehoji iweje kada huyu mwaminifu wa ccm aikosoe ccm hadharani badala ya kutumia vikao vya chama.

Hata hivyo uchina ni muungaji mkono wa serikali zote,hats zile zilizowekwa madakani kwa bila mgano SMZ na serikali ya Nkulunzinza.Wachina in lvibarua wa dunia,wanahaha nchi zote kutafuta kandarasi mbalimbali,ulitegemea wawe kinyume na serikali hizo?Ni lazima wasifie ili wapate fursa ya kupiga dili.

So tu wachina wameisifia serikali ya ccm,wachina ni wanachama wa ccm na wanamiliki kafi halali za ccm.
 
Ukiona china inakusifia sana ujue raslimali zako zinapatikana kwa urahisi sana.
 
Naibu waziri wa mambo ya nje wa Jamhuri ya watu wa china Guo Yezhou ambaye pia ni mjumbe wa chama cha Kikomunisti cha nchini humo ametembelea makao makuu ya chama cha mapinduzi CCM Mkoani Dodoma ambacho ni chama rafiki huku akisema nchi yake inafurahishwa na utendaji wa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli katika kukabiliana na matumizi mabaya ya fedha za umma rushwa na ufisadi

Akizungumza mara baada ya kuwasili mjini Dodoma Naibu waziri huyo wa mambo ya nje kutoka nchini China amesema Serikali ya China na Tanzania zimekuwa zikifanya kazi kwa ushirikiano mkubwa ambapo pia ametumia fursa hiyo kumtaka raisi magufuli kufanya kazi kwa kufuata misingi iliyoachwa na mwasisi wa taifa hili Hayati Mwalimu Julius Nyerere ili tanzania iweze kupiga hatua kimaendeo na kiuchumi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Alhadji Adam Kimbisa ambaye ndie aliyekuwa mwenyeji wa kiongozi huyo kutoka uchina amesema chama cha mapinduzi na Serikali yake kitaendelea kudumisha ushirikiano kati ya Mataifa hayo mawili ambao umedumu kwa muda mrefu.

Tanzania na china zina urafiki wa kudumuumedumu kwa mrefu ambapo mpaka sasa ni miaka zaidi ya miaka 49 zikishirikiana katika mambo mbalimbali yakiwemo kiuchumi,siasa, jamii na usalama.


Chanzo: itv
Wasi wasi wangu ni viumbe hai hasa tembo wetu
 
China hawajawahi kataa serikalj yoyote duniani hata ya nkurunziza waliikubali, chezea Chinese wewe
Hata marekani hawajakataa serikali yoyote mpaka wakikuchoka tu. Walimkubali Sadaam na Mobutu, na bado wanapiga kelele kuhusu democracy wakati marafiki zao wakubwa Saudi Arabia hawana hata chembe ya hiyo democracy.
 
Hata marekani hawajakataa serikali yoyote mpaka wakikuchoka tu. Walimkubali Sadaam na Mobutu, na bado wanapiga kelele kuhusu democracy wakati marafiki zao wakubwa Saudi Arabia hawana hata chembe ya hiyo democracy.
Una kazi sana mkuu, ushawahj ona balozi wa marekani kavaa sare ya chama chochote??
 
Naibu waziri wa mambo ya nje wa Jamhuri ya watu wa china Guo Yezhou ambaye pia ni mjumbe wa chama cha Kikomunisti cha nchini humo ametembelea makao makuu ya chama cha mapinduzi CCM Mkoani Dodoma ambacho ni chama rafiki huku akisema nchi yake inafurahishwa na utendaji wa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli katika kukabiliana na matumizi mabaya ya fedha za umma rushwa na ufisadi

Akizungumza mara baada ya kuwasili mjini Dodoma Naibu waziri huyo wa mambo ya nje kutoka nchini China amesema Serikali ya China na Tanzania zimekuwa zikifanya kazi kwa ushirikiano mkubwa ambapo pia ametumia fursa hiyo kumtaka raisi magufuli kufanya kazi kwa kufuata misingi iliyoachwa na mwasisi wa taifa hili Hayati Mwalimu Julius Nyerere ili tanzania iweze kupiga hatua kimaendeo na kiuchumi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Alhadji Adam Kimbisa ambaye ndie aliyekuwa mwenyeji wa kiongozi huyo kutoka uchina amesema chama cha mapinduzi na Serikali yake kitaendelea kudumisha ushirikiano kati ya Mataifa hayo mawili ambao umedumu kwa muda mrefu.

Tanzania na china zina urafiki wa kudumuumedumu kwa mrefu ambapo mpaka sasa ni miaka zaidi ya miaka 49 zikishirikiana katika mambo mbalimbali yakiwemo kiuchumi,siasa, jamii na usalama.


Chanzo: itv
Wachina wanahangaika sana au kwa vile bwana shamba wa shamba la bibi amebadilishwa. Mara kwenye chama tawala mara serikalini. Magufuli kaza roho, hawa siku hizi hawana tofauti na mmarekani.
 
Naona kama kuna dili la ndovu hapo, maana ukichanganya hizo rangi za kijani na wachina ni full balaa kwa tembo wetu
Watachukua ndovu halafu watarudi kutuuzia bidhaa sisi wenyewe
 
Back
Top Bottom