October 2pm
JF-Expert Member
- May 2, 2023
- 1,124
- 1,983
Chikwete kawafunga vibwebwe hawa kwa miaka ishirini na sijui mwishowe lini Kama si mile. Na alivyopandikiza vigingi vyake, si kazi ya mlo mmoja kuving’oa, wallahi. Hata akija mwenye jina, hukuta kiti kimeshikwa kwa nanga!
We ukijifanya mnoko akufunika kama leso la Chokoraa. Alianza na Gowasa huyo alifikiria kavuka, kumbe bado yu mtoni. Kisha akamleta Nyembe, naye akachezwa kama bao la kiswahili. Akarudi kwa Fuguo, akaigeuza meza, na sasa hii round anamchamba hadi kiwambo Katani wa Bulibuli.
Yule Katani, roho yake ilianza kumsogeza kwenye meza ya Chikwete. Meza imetandikwa vyema nyama, wali, mamlaka, hata misosi ya kisiasa. Lakini Mzee Baba ah, si mtu wa mchezo huyo. Akasema: 'Hawa watoto wa mtaani wasinijazie meza, nami nina wa kwangu. Kwani Hirizimbili anashida gani. Bi Mdashi mwenyewe yuaongoza, sembuse kijana wangu Mwanaume kamili huyu!'
Unasikia? Wanaume wanapigwa chini kiroho safi, lakini cha kufanya hawana. Wamebaki wanapiga pingu za moyo kimyakimya. Na bado, mdundo haujaisha."
We ukijifanya mnoko akufunika kama leso la Chokoraa. Alianza na Gowasa huyo alifikiria kavuka, kumbe bado yu mtoni. Kisha akamleta Nyembe, naye akachezwa kama bao la kiswahili. Akarudi kwa Fuguo, akaigeuza meza, na sasa hii round anamchamba hadi kiwambo Katani wa Bulibuli.
Yule Katani, roho yake ilianza kumsogeza kwenye meza ya Chikwete. Meza imetandikwa vyema nyama, wali, mamlaka, hata misosi ya kisiasa. Lakini Mzee Baba ah, si mtu wa mchezo huyo. Akasema: 'Hawa watoto wa mtaani wasinijazie meza, nami nina wa kwangu. Kwani Hirizimbili anashida gani. Bi Mdashi mwenyewe yuaongoza, sembuse kijana wangu Mwanaume kamili huyu!'
Unasikia? Wanaume wanapigwa chini kiroho safi, lakini cha kufanya hawana. Wamebaki wanapiga pingu za moyo kimyakimya. Na bado, mdundo haujaisha."