Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Mbunge wa Viti Maalum mkoani Iringa, Chiku Abwao, ametangaza rasmi kwamba kazi ya kulitwaa Jimbo la Isimani linaloshikiliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, kuelekea uchaguzi mkuu ujao, itaongozwa na Operesheni Sangara ya chama chake.
Abwao ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Iringa, amesema Bunge limemalizika na kazi iliyobaki ni kuanza kukijenga chama chake katika mkoa huu.
Aliliambia NIPASHE jana katika mahojiano maalumu kuwa jimbo hilo litatwaliwa na kuongozwa na Chadema katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kutokana na ukweli kwamba tangu Lukuvi aliongoze jimbo hilo kwa kipindi kirefu, hakuna jitihada zozote anazozifanya kuwanasua wananchi katika lindi la umaskini.
"Kama unavyojua, sasa hivi tuna kazi ya kuyakomboa majimbo yote yanayoongozwa na vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mimi nina kazi moja tu ya kumng'oa Waziri Lukuvi kwa sababu tunataka kuirejesha Isimani katika sura ya kitaifa iliyokuwa nayo miaka ya nyuma...Amekaa katika jimbo hilo kwa muda mrefu na bado wananchi wake wanafikia mahali wanaomba chakula cha msaada. Hii ni aibu," alisema Abwao.
Akifafanua nia yake ya kutaka kuwania ubunge katika jimbo hilo, Abwao alisema Isimani ndilo eneo maarufu linalofahamika kitaifa kwa uzalishaji wa chakula kwa miaka mingi, lakini kutokana na kukosa fursa na mipango ya ushawishi kwa wananchi ili wajikwamue na umaskini, ndio sababu kuu iliyomfanya aamue kutangaza rasmi kuliwania jimbo hilo.
"Isimani itarejea tena na kuuinua mkoa wa Iringa kuwa kitovu cha uzalishaji wa chakula katika ile mikoa minne itakayokuwa ghala la taifa la chakula iwapo wananchi wataacha kasumba ya kuwabeba CCM na viongozi wao ambao kila kukicha wanakuja na mipango mibovu isiyolenga ukombozi wa mkulima," alisema.
Kwa mujibu wa Abwao, kazi ya kukijenga chama hicho katika jimbo hilo la Waziri Lukuvi, itaanza rasmi baada ya yeye kurejea kutoka jijini Dar es Salaam kuhudhuria mkutano wa dharura wa Kamati Kuu ya Chadema ambao unakwenda sambamba na mkutano wa Baraza Kuu la Taifa la chama hicho.
Source:Nipashe Ijumaa
Abwao ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Iringa, amesema Bunge limemalizika na kazi iliyobaki ni kuanza kukijenga chama chake katika mkoa huu.
Aliliambia NIPASHE jana katika mahojiano maalumu kuwa jimbo hilo litatwaliwa na kuongozwa na Chadema katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kutokana na ukweli kwamba tangu Lukuvi aliongoze jimbo hilo kwa kipindi kirefu, hakuna jitihada zozote anazozifanya kuwanasua wananchi katika lindi la umaskini.
"Kama unavyojua, sasa hivi tuna kazi ya kuyakomboa majimbo yote yanayoongozwa na vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mimi nina kazi moja tu ya kumng'oa Waziri Lukuvi kwa sababu tunataka kuirejesha Isimani katika sura ya kitaifa iliyokuwa nayo miaka ya nyuma...Amekaa katika jimbo hilo kwa muda mrefu na bado wananchi wake wanafikia mahali wanaomba chakula cha msaada. Hii ni aibu," alisema Abwao.
Akifafanua nia yake ya kutaka kuwania ubunge katika jimbo hilo, Abwao alisema Isimani ndilo eneo maarufu linalofahamika kitaifa kwa uzalishaji wa chakula kwa miaka mingi, lakini kutokana na kukosa fursa na mipango ya ushawishi kwa wananchi ili wajikwamue na umaskini, ndio sababu kuu iliyomfanya aamue kutangaza rasmi kuliwania jimbo hilo.
"Isimani itarejea tena na kuuinua mkoa wa Iringa kuwa kitovu cha uzalishaji wa chakula katika ile mikoa minne itakayokuwa ghala la taifa la chakula iwapo wananchi wataacha kasumba ya kuwabeba CCM na viongozi wao ambao kila kukicha wanakuja na mipango mibovu isiyolenga ukombozi wa mkulima," alisema.
Kwa mujibu wa Abwao, kazi ya kukijenga chama hicho katika jimbo hilo la Waziri Lukuvi, itaanza rasmi baada ya yeye kurejea kutoka jijini Dar es Salaam kuhudhuria mkutano wa dharura wa Kamati Kuu ya Chadema ambao unakwenda sambamba na mkutano wa Baraza Kuu la Taifa la chama hicho.
Source:Nipashe Ijumaa