Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Chama Cha Ukombozi wa Umma CHAUMMA, kimeahirisha uzinduzi wa mkutano wake wa hadhara uliokuwa ufanyike Juni Mosi, 2025 baada kukukosa kibali cha helkopta kutua na uwanja wa kufanyia mkutano huo.
Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama hicho, Benson Kigaila wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 29,2025 Jijini Mwanza.
Kigaila amesema awali walipanga tarehe ya mkutano wakitegemea kupata vibali hivyo mapema lakini hadi hivi sasa bado hawajafanikiwa kuvipata na hivyo kupanga kufanya mkutano huo Juni 3, 2025.
"Tulipofika Mwanza tumeona tusogeze siku mbele kwa sababu mbili, sababu ya kwanza mpaka leo hatujapata kibali cha helkopta, ukiwa hujapata kibali huwezi kuendelea na tarehe hiyo hiyo huku ziku za kutafuta kibali zinapungua kwa busara ya kawaida tumeona tusogeze siku mbele ili tuongeze juhudi ya kutafuta kibali, na uwanja wa kufanyia mkutano," amesema.
Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama hicho, Benson Kigaila wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 29,2025 Jijini Mwanza.
Kigaila amesema awali walipanga tarehe ya mkutano wakitegemea kupata vibali hivyo mapema lakini hadi hivi sasa bado hawajafanikiwa kuvipata na hivyo kupanga kufanya mkutano huo Juni 3, 2025.
"Tulipofika Mwanza tumeona tusogeze siku mbele kwa sababu mbili, sababu ya kwanza mpaka leo hatujapata kibali cha helkopta, ukiwa hujapata kibali huwezi kuendelea na tarehe hiyo hiyo huku ziku za kutafuta kibali zinapungua kwa busara ya kawaida tumeona tusogeze siku mbele ili tuongeze juhudi ya kutafuta kibali, na uwanja wa kufanyia mkutano," amesema.