GE2025 CHASO yapanga kumfungulia Kesi Rais wa TAHLISO, Geofrey Kiliba kwa kukiuka misingi ya Katiba ya umoja wa wanafunzi vyuo vikuu

GE2025 CHASO yapanga kumfungulia Kesi Rais wa TAHLISO, Geofrey Kiliba kwa kukiuka misingi ya Katiba ya umoja wa wanafunzi vyuo vikuu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mwenyekiti wa CHASO (CHADEMA Student Organization) mkoa wa Dar es Salaam Martin Samson Abduli ametoa tamko kwa waandishi wa habari akilalamikia mwenendo wa Rais wa TAHILISO Geofrey Kiliba akidai kuwa unakiuka misingi ya Katiba ya umoja huo wa wanafunzi wa vyuo na vyio vikuu nchini

Akizungumza jijini Dar es Salaam Abduli amesema kuwa Rais wa TAHILISO anatakiwa kutumia majukwaa yake kuzungumzia changamoto zinazowakabili wanafunzi badala ya kujihusisha na siasa za upande wowote au vyama, jambo ambalo linaenda kinyume na Katiba ya umoja huo

"Wanafunzi wanapitia changamoto nyingi kwenye masomo na maisha ya kila siku, hizo ndizo angekuwa anazizungumza badala ya mambo ya kisiasa" -Abduli

Aidha, Abduli amebainisha kuwa tayari mchakato umeanza wa kufungua kesi ya Kikatiba Mahakamani dhidi ya Rais huyo wa TAHILISO, huku akitoa wito kwa wanafunzi kote nchini kuunga mkono jitihada hizo


Soma pia GE2025 - Katibu Mkuu, TAHLISO: Malalamiko ya ukiukwaji wa Maadili ya Uongozi na Katiba dhidi ya Rais Geofrey Kiliba kwa upendeleo wa Kisiasa



Chanzo: Jambo TV
 
Back
Top Bottom