Fandre
JF-Expert Member
- Sep 20, 2013
- 320
- 225
Askofu Dr. Josephat Gwajima
Ufufuo na Uzima-Headquarters
Dar es Salaam, Tanzania
03/05/2015
Maandiko:
Ufunuo Wa Yohana 13:17
Mwanzo 4:5
Wagalaatia 6:16
Ufunuo 9:4
Yoshua 2:15
Chapa ni alama anazowekewa mtu au kitu na kukitambulisha kuhusiana na jambo husika.
Dunia ina chapa nyingi kadhalika katika ulimwengu wa Kiroho yaani ule usiionekana kuna chapa za Mungu na chapa za Shetani yaani Chapa za Kichawi.
"Anything Satanic is witchcraft"
Upande wa pili:
Muhuri ni mchoro wa maandishi yanayoonyesha mwenye alama inayothibitisha uhalali wa jambo au mtu juu ya jambo fulani!
Sasa kwa maarifa haya ya Chapa na Mihuri ndivyo ilivyo hata kwa ulimwengu ule usioonekana(Rohoni) nao unaendeshwa na mambo haya muhimu.
Kuna mifano kadhaa ya watu waliowahi kuwekewa Chapa na mihuri katika Biblia ambao waliwekewa na Mungu:
1. Paulo
2. Kaini
Hivyo basi wachawi nao wanayo maarifa ya kuwawekea watu mihuri au chapa ambazo zitawafanya watu hao kuteseka kwa kulingana na mihuri waliowawekea.
Wapo waliowekewa mihuri ya:
1. Mihuri ya Kifo
2. Mihuri ya Magonjwa
3. Mihuri ya Umasikini
4. Mihuri ya Kukataliwa n.k.
Hivyo basi, mihuri ya kichawi huwafanya watu waliowekewa mihuri hii kufuatiliwa na kila matatizo na laana kulingana na muhuri aliowekewa mtu katika maisha yake.
Mihuri ina maana sana kwa sababu pasipo muhuri watu hawawezi kuamini uhalali Wa jambo hilo kwahiyo kwa kila tatizo linalompata mtu kuna muhuri ulikwishawekwa katika maisha ya mtu huyo katika ulimwengu wa roho ama na wachawi au waganga au warozi pasipo yeye kujua.
Familia/Kaya nyingi zimekua na matatizo ya kufuatana na yasiyoisha na zimekosa majibu na matatizo yamekua na kufuata kila mtu katika ukoo na wengi wamejaribu kujitoa katika maisha hayo lakini wameshindwa kujitoa na wamekosa majibu nini kilichopelekea kukutwa na shida au matatizo yao!
Kwahiyo ni jambo la kuaminika kabisa ya kuwa wapo watu wengi duniani na familia nyingi zimewekewa mihuri na chapa ambazo zinawafanya kuwa katika mazingira ya kuonewa na nguvu za Giza pamoja na wachawi kwani chapa hizo zinawapa wachawi Uhuru wa kuwatesa kulingana na chapa hizo!
Katika vitabu vya Ufunuo Wa mambo yajayo tunajifunza ya kuwa...."Watu watawekewa chapa ya mpinga Kristo ambayo itawafanya wawe na uwezo wa kununua au kutokununua"
Shetani anao uwezo wa kuweka chapa ambazo ni za mangamizi kwenye maisha ya watu.
Kwa lugha nyepesi CHAPA ni ile mipaka ambayo watu huwekewa katika maisha wasiweze kufikia malengo yao na mambo muhimu katika maisha.
Watu wengi waliowekewa chapa na mihuri ya umasikini wamefungwa akili zao ili wasijue nini cha kufanya ili kuendelea mbele.
Kuna watu hupata mishahara au pesa lakini mwisho wa siku hawajui pesa zimepotea namna gani kwani huisha pasipo kufanya jambo lolote la msingi!
Kadharika Taifa nalo linawez kuwekewa Chapa na mashetani kutokana na misingi ya viongozi Wa Taifa. Mfano: Tanzania inaweza kuwa imewekewa Chapa za Umasikini na kudolola kwa uchumi kutokana na misingi ya kichawi ya viongozi wa Taifa.
Watu wengi wana chapa wamewekewa wao ni kulogwa tu katika maisha yaani kila unapojitahidi kuwakimbia wachawi au matatizo bado yana wewe tu!
Kwahiyo ni jukumu la kila mwanadamu kuwa na maarifa ya kutosha juu ya namna ambavyo wachawi na shetani hutumia kuwaharibia watu maisha na kujua huku kitakusaidia kujua namna ya kumshinda shetani na wachawi.
**********Mwisho ***********
NB:
Kwa mafundisho zaidi ya Askofu Gwajima kwa mfumo wa DVD, MP3, Vitabu na maombezi kutoka katika vifungo vya kichawi na kishetani.
+ 255 673 848428
Ufufuo na Uzima-Headquarters
Dar es Salaam, Tanzania
03/05/2015
Maandiko:
Ufunuo Wa Yohana 13:17
Mwanzo 4:5
Wagalaatia 6:16
Ufunuo 9:4
Yoshua 2:15
Chapa ni alama anazowekewa mtu au kitu na kukitambulisha kuhusiana na jambo husika.
Dunia ina chapa nyingi kadhalika katika ulimwengu wa Kiroho yaani ule usiionekana kuna chapa za Mungu na chapa za Shetani yaani Chapa za Kichawi.
"Anything Satanic is witchcraft"
Upande wa pili:
Muhuri ni mchoro wa maandishi yanayoonyesha mwenye alama inayothibitisha uhalali wa jambo au mtu juu ya jambo fulani!
Sasa kwa maarifa haya ya Chapa na Mihuri ndivyo ilivyo hata kwa ulimwengu ule usioonekana(Rohoni) nao unaendeshwa na mambo haya muhimu.
Kuna mifano kadhaa ya watu waliowahi kuwekewa Chapa na mihuri katika Biblia ambao waliwekewa na Mungu:
1. Paulo
2. Kaini
Hivyo basi wachawi nao wanayo maarifa ya kuwawekea watu mihuri au chapa ambazo zitawafanya watu hao kuteseka kwa kulingana na mihuri waliowawekea.
Wapo waliowekewa mihuri ya:
1. Mihuri ya Kifo
2. Mihuri ya Magonjwa
3. Mihuri ya Umasikini
4. Mihuri ya Kukataliwa n.k.
Hivyo basi, mihuri ya kichawi huwafanya watu waliowekewa mihuri hii kufuatiliwa na kila matatizo na laana kulingana na muhuri aliowekewa mtu katika maisha yake.
Mihuri ina maana sana kwa sababu pasipo muhuri watu hawawezi kuamini uhalali Wa jambo hilo kwahiyo kwa kila tatizo linalompata mtu kuna muhuri ulikwishawekwa katika maisha ya mtu huyo katika ulimwengu wa roho ama na wachawi au waganga au warozi pasipo yeye kujua.
Familia/Kaya nyingi zimekua na matatizo ya kufuatana na yasiyoisha na zimekosa majibu na matatizo yamekua na kufuata kila mtu katika ukoo na wengi wamejaribu kujitoa katika maisha hayo lakini wameshindwa kujitoa na wamekosa majibu nini kilichopelekea kukutwa na shida au matatizo yao!
Kwahiyo ni jambo la kuaminika kabisa ya kuwa wapo watu wengi duniani na familia nyingi zimewekewa mihuri na chapa ambazo zinawafanya kuwa katika mazingira ya kuonewa na nguvu za Giza pamoja na wachawi kwani chapa hizo zinawapa wachawi Uhuru wa kuwatesa kulingana na chapa hizo!
Katika vitabu vya Ufunuo Wa mambo yajayo tunajifunza ya kuwa...."Watu watawekewa chapa ya mpinga Kristo ambayo itawafanya wawe na uwezo wa kununua au kutokununua"
Shetani anao uwezo wa kuweka chapa ambazo ni za mangamizi kwenye maisha ya watu.
Kwa lugha nyepesi CHAPA ni ile mipaka ambayo watu huwekewa katika maisha wasiweze kufikia malengo yao na mambo muhimu katika maisha.
Watu wengi waliowekewa chapa na mihuri ya umasikini wamefungwa akili zao ili wasijue nini cha kufanya ili kuendelea mbele.
Kuna watu hupata mishahara au pesa lakini mwisho wa siku hawajui pesa zimepotea namna gani kwani huisha pasipo kufanya jambo lolote la msingi!
Kadharika Taifa nalo linawez kuwekewa Chapa na mashetani kutokana na misingi ya viongozi Wa Taifa. Mfano: Tanzania inaweza kuwa imewekewa Chapa za Umasikini na kudolola kwa uchumi kutokana na misingi ya kichawi ya viongozi wa Taifa.
Watu wengi wana chapa wamewekewa wao ni kulogwa tu katika maisha yaani kila unapojitahidi kuwakimbia wachawi au matatizo bado yana wewe tu!
Kwahiyo ni jukumu la kila mwanadamu kuwa na maarifa ya kutosha juu ya namna ambavyo wachawi na shetani hutumia kuwaharibia watu maisha na kujua huku kitakusaidia kujua namna ya kumshinda shetani na wachawi.
**********Mwisho ***********
NB:
Kwa mafundisho zaidi ya Askofu Gwajima kwa mfumo wa DVD, MP3, Vitabu na maombezi kutoka katika vifungo vya kichawi na kishetani.
+ 255 673 848428