change is gonna come

Moshe Dayan

JF-Expert Member
Feb 10, 2008
815
698
Ushauri wangu kwa CDM na wafuasi, mabadiliko yoyote makubwa ni lazima yawe na ukinzani mkubwa.., uvumilivu na kutokata tamaa unahitajika sana.ukiangalia historia za nchi nyingine ambazo utawala ulianguka kwa upinzani, zilikua namna hii hii, kwa vurugu ambazo wanazisababisha dola tawala na bado walianguka.

kwa wale waliopekua vitabu nadhani mtakumbuka kuna LEWIN'S CHANGE MODEL

Hii model japo ipo ki-corporate zaidi lakini inaelezea nini hua kinatokea pale mabadiliko makubwa yanapotaka kufanyika..., resistance!! Kuna watu, iwe isiwe, watapambana kwa hali na mali kupinga mabadiliko yenye maslahi.

kwa nchi ilipofika sasa, mabadiliko ya utawala mzima utakua brutal, bloody, mean with ironfist tryng to crash everything which comes on their way!

Ironfist ni dola kama za mahakama, police, usalama wa taifa etc,

Nani asiyejua fiesta ilikua inaendelea, same day mwangosi anauawa kulikua na mkutano bububu, wafuasi wa chadema msikate tamaa, hawa jamaa hawataachia madaraka kirahisi kwa sababu wanajua nini kitafata dhidi yao.

Kwa leo naishia hapa, ila jitahidi kupita youtube tujiliwaze kwa hizi nyimbo

SAM COOKE(1963) CHANGE IS GONNA COME, kipindi cha civil rights movement marekani,

Bob Marley, redemption song,

"WHO DARES, WINS!"
 
Back
Top Bottom