Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Mitandao ya kijamii imekuwa sehemu ya maisha ya kila siku kwa vijana wengi, lakini pia imegeuka kuwa uwanja wa changamoto zisizo na maana wala faida yoyote kwa jamii.
Hivi karibuni, kijana anayejulikana kwa jina la Tonie Professor ameibua mjadala baada ya kuanza kurekodi na kusambaza video akinywa vilevi vikali kama Konyagi na vinywaji vingine kwa wingi, huku akifanya hivyo kama sehemu ya “challenge” kwa mashabiki wake katika mitandao ya TikTok na Instagram.
Mashabiki wake, kwa kutaka kuona zaidi, humtupia maoni yenye kumshawishi kunywa pombe zaidi na zaidi. Hali hii imeanza kuigwa na vijana wengine ambao wanataka kuonekana mashujaa wa ulevi, jambo linaloongeza hofu kubwa katika jamii.
Wataalamu wa afya wamekuwa wakionya mara kwa mara juu ya athari za kunywa vilevi kwa kiwango kikubwa, zikihusisha uharibifu wa ini, figo, moyo na hata kuathiri mfumo wa fahamu. Lakini hatari kubwa zaidi sasa ni kitendo cha vijana kushindana kwa kigezo cha nani anaweza kunywa zaidi bila kupoteza fahamu.
Je, mamlaka na wizara husika hazioni? Je, ni mpaka pale ambapo tutaamka na taarifa za vifo vya vijana kutokana na changamoto hizi ndipo hatua zichukuliwe?
Mitandao inaweza kutumika kuelimisha na kujenga, lakini kwa sasa imekuwa jukwaa la hatari linalowachochea vijana kushindana katika ulevi. Ni wakati wa mamlaka, wazazi na jamii kwa ujumla kuchukua hatua madhubuti ili kunusuru mustakabali wa vijana wetu.
NIKIUMWA SINA HELA MPAKA NYUMBANI
Hivi karibuni, kijana anayejulikana kwa jina la Tonie Professor ameibua mjadala baada ya kuanza kurekodi na kusambaza video akinywa vilevi vikali kama Konyagi na vinywaji vingine kwa wingi, huku akifanya hivyo kama sehemu ya “challenge” kwa mashabiki wake katika mitandao ya TikTok na Instagram.
Mashabiki wake, kwa kutaka kuona zaidi, humtupia maoni yenye kumshawishi kunywa pombe zaidi na zaidi. Hali hii imeanza kuigwa na vijana wengine ambao wanataka kuonekana mashujaa wa ulevi, jambo linaloongeza hofu kubwa katika jamii.
Wataalamu wa afya wamekuwa wakionya mara kwa mara juu ya athari za kunywa vilevi kwa kiwango kikubwa, zikihusisha uharibifu wa ini, figo, moyo na hata kuathiri mfumo wa fahamu. Lakini hatari kubwa zaidi sasa ni kitendo cha vijana kushindana kwa kigezo cha nani anaweza kunywa zaidi bila kupoteza fahamu.
Je, mamlaka na wizara husika hazioni? Je, ni mpaka pale ambapo tutaamka na taarifa za vifo vya vijana kutokana na changamoto hizi ndipo hatua zichukuliwe?
Mitandao inaweza kutumika kuelimisha na kujenga, lakini kwa sasa imekuwa jukwaa la hatari linalowachochea vijana kushindana katika ulevi. Ni wakati wa mamlaka, wazazi na jamii kwa ujumla kuchukua hatua madhubuti ili kunusuru mustakabali wa vijana wetu.
NIKIUMWA SINA HELA MPAKA NYUMBANI