Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,760
Inashangaza sana Chama Cha CCM kimekuwepo madarakani zaidi ya miaka 50 ,kama maendeleo wameleta wao kama ni shida wameleta wao ,ikiwa Chama hiki kinajiamini kuwa kinapendwa na wananchi walio wengi ni kwanini kinategemea kushinda kwa magube .
Kinategemea kubebwa ,kulindwa ili kisipoteze uwakilishi katika maeneo mbali mbali hapa Tanzania ,chaguzi zilizomalizika hivi karibuni zimedhihirisha hayo ,kuwa bila ya mkono wa udanganyifu CCM inakuwa vigumu kushinda ,wenyewe wanaziita mbinu ila katika kutafuta haki ya uchaguzi mbinu za udanganyifu hazikubaliki, hilo ,jamaa zangu wa ccm lazima walielewe.
Haiwezekani mpo kwenye madaraka kwa miaka yote hiyo bado mnategemea udanganyifu ili mubaki madarakani ,huko ni kupoteza dira na kuishiwa zaidi tunasema ni kufilisika katika uwanja wa siasa ,tokea ilikuwa kushindwa kwenu ni siri hadi leo hii imekuwa si siri tena ,mnashindwa mchana kweupe na kushindwa kwenu hakufichiki tena ,watoto wadogo sasa wanauelewa wa kushindwa kwenu.
Bado inaonyesha akili zenu hazijakubali kuwa mupo kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa ,mnajiona mpo peke yenu ,huko ni kuchanganyikiwa na kupoteza muelekeo wa uongozi ,kinachoonekana kila awamu yenu inayokuja inakuwa ni ya kujali maslahi binafsi na si ya kujali uongozi na unaowaongoza ,uwajibikaji umekuwa duni kwenu,kila awamu inayokuja inakuwa ni mbaya kuliko iliyopita ,mnatupeleka wapi ?
Kuweni makini na mkubali siasa za kiushindani katika uwanja ulio sawa bila ya kutumia udanganyifu ,kitu gani kinachowafanya msijiamini ,mnaogopa aibu ? Ya kushindwa ,ikiwa hilo ndio reason basi hamfai kuwepo katika medani za kisiasa.kama mnategemea kudaganganya ,mnategemea kubebwa ,hamtaongoza nchi bali itakuwa kama tunavyoona corruptions every angle ,ndizo mnazotuletea na kufika kuviharibu hata vyombo vya dola viwe navyo vinaishi kwa kutegemea rushwa.
Someni alama za nyakati ,nchi zinabadilika ,mnaona,mnasoma,mnasikia yanayojiri nchi zingine si hadithi za kubuniwa ni mambo ya kiuhalisia kabisa ambayo yanahitaji mtu aliepo madarakani kujifunza na kuyakubali ukweli na sababu zake ,isiwe mnazikumbatia sababu na kujiona mtaweza kuzihimili na kuziweka chini ya udhibiti ,halitakufaeni jeshi wala polisi mambo yakiteguka ,labda nyie na mali zenu na hela mlizokwapua mtakimbia ,wananchi watakaobakia ndio watakaoteseka ,japo hilo haliwashughulishi ,lakini hisia za mtu na nchi yake ni majuto hapo baadae.
CCM jipangeni katika medani za kisiasa na muwache mara moja kutegemea kubebwa na kulindwa huu si wakati wa kuyakumbatia hayo ,aachwe alieshinda kiuhalali apewe ushindi wake kwa amani kabisa na kwa moyo mkunjufu sio kulazimisha ni lazima fulani au chama fulani kishinde na kulazimisha mwengine aonekane ameshindwa ,maendeleo katu hayatapatikana kwa njia hiyo katika Nchi hii.
Kinategemea kubebwa ,kulindwa ili kisipoteze uwakilishi katika maeneo mbali mbali hapa Tanzania ,chaguzi zilizomalizika hivi karibuni zimedhihirisha hayo ,kuwa bila ya mkono wa udanganyifu CCM inakuwa vigumu kushinda ,wenyewe wanaziita mbinu ila katika kutafuta haki ya uchaguzi mbinu za udanganyifu hazikubaliki, hilo ,jamaa zangu wa ccm lazima walielewe.
Haiwezekani mpo kwenye madaraka kwa miaka yote hiyo bado mnategemea udanganyifu ili mubaki madarakani ,huko ni kupoteza dira na kuishiwa zaidi tunasema ni kufilisika katika uwanja wa siasa ,tokea ilikuwa kushindwa kwenu ni siri hadi leo hii imekuwa si siri tena ,mnashindwa mchana kweupe na kushindwa kwenu hakufichiki tena ,watoto wadogo sasa wanauelewa wa kushindwa kwenu.
Bado inaonyesha akili zenu hazijakubali kuwa mupo kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa ,mnajiona mpo peke yenu ,huko ni kuchanganyikiwa na kupoteza muelekeo wa uongozi ,kinachoonekana kila awamu yenu inayokuja inakuwa ni ya kujali maslahi binafsi na si ya kujali uongozi na unaowaongoza ,uwajibikaji umekuwa duni kwenu,kila awamu inayokuja inakuwa ni mbaya kuliko iliyopita ,mnatupeleka wapi ?
Kuweni makini na mkubali siasa za kiushindani katika uwanja ulio sawa bila ya kutumia udanganyifu ,kitu gani kinachowafanya msijiamini ,mnaogopa aibu ? Ya kushindwa ,ikiwa hilo ndio reason basi hamfai kuwepo katika medani za kisiasa.kama mnategemea kudaganganya ,mnategemea kubebwa ,hamtaongoza nchi bali itakuwa kama tunavyoona corruptions every angle ,ndizo mnazotuletea na kufika kuviharibu hata vyombo vya dola viwe navyo vinaishi kwa kutegemea rushwa.
Someni alama za nyakati ,nchi zinabadilika ,mnaona,mnasoma,mnasikia yanayojiri nchi zingine si hadithi za kubuniwa ni mambo ya kiuhalisia kabisa ambayo yanahitaji mtu aliepo madarakani kujifunza na kuyakubali ukweli na sababu zake ,isiwe mnazikumbatia sababu na kujiona mtaweza kuzihimili na kuziweka chini ya udhibiti ,halitakufaeni jeshi wala polisi mambo yakiteguka ,labda nyie na mali zenu na hela mlizokwapua mtakimbia ,wananchi watakaobakia ndio watakaoteseka ,japo hilo haliwashughulishi ,lakini hisia za mtu na nchi yake ni majuto hapo baadae.
CCM jipangeni katika medani za kisiasa na muwache mara moja kutegemea kubebwa na kulindwa huu si wakati wa kuyakumbatia hayo ,aachwe alieshinda kiuhalali apewe ushindi wake kwa amani kabisa na kwa moyo mkunjufu sio kulazimisha ni lazima fulani au chama fulani kishinde na kulazimisha mwengine aonekane ameshindwa ,maendeleo katu hayatapatikana kwa njia hiyo katika Nchi hii.