Ni CCM pekee yenye kuwa na ilani kila uchaguzi inayokidhi matarajio nakukata kiu ya watanzania,Ni CCM pekee yenye kuwa na ilani kila uchaguzi inayoendana na mahitaji ya watanzania,Ni CCM yenye kuwa na ilani kila uchaguzi yenye kujibu maswali ya watanzania,Ni CCM pekee inayokuwa na ilani yake kila uchaguzi yenye kubeba Sera na ajenda zinazogusa maisha ya watanzania,ndio maana inaungwa mkono ,kuchaguliwa na kupita kwa kishindooo katika kila uchaguzi.
Mavyama mengine Ni ya msimu tu,Ni wasaka tonge tu,Ni vikundi vya wasaka fursa,Ni vyama vya kurithishana Kama ilivyo kwa chadema kwa mtu kumuachia Chaka mkwe wake Kama kitega uchumi chake na ndio maana huko Chadema ukigusa ukigoda tu Ni sawa na kulamba sumu kwa ulimi wako mwenyewe.
Mavyama hayo ya upinzani hayana Sera Wala ajenda Wala maono,Ni vyama visivyoweza hata kuandaa mgombea Urais na ndio maana mwaka 2015 ilibidi Chadema waazime mgombea kutoka CCM ,ambapo wakawa hawana hata ilani zaidi ya kuwaambia wafuais wao waliojikatia Tamaa kuwa wakaitafute kwenye MTANDAO.
Hinyi ningekushauri usipoteze muda wako kuzitafuta ilani zao za upinzani maana wao huenda kimzuka mzuka tu kulingana na biti la mgombea wao na kile kinachomjia kichwani na mdomoni mwake. Ilani ya upinzani Ni mgombea mwenyewe ndio ilani Yao.