Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,799
- 59,262
Chama Chahitaji Mapinduzi.
Sote tunajua kinachojiita Chama cha Mapinduzi hakijawahi kufanya mapinduzi yoyote. Neno mapinduzi kwa kadiri ninavyoelewa linaashiria mabadiliko ya haraka ya kisiasa wakati mwingine hata kumwagika damu au vurugu kama tulivyoona kule Misri na Tunisia. Katika nchi yetu mabadiliko ya aina hiyo yalitokea Zanzibar lakini hadi hivi sasa mjadala bado upo juu ya nani hasa walihusika. TANU tunajua haikuhusika (japo kwa wazi) na ASP kwa kadiri ninavyosoma humu inaonekana walidandia tu mbele ya safari.
Sasa kwanini CCM inajiita Chama cha Mapinduzi kama hakijawahi kushiriki mapinduzi yoyote? Ninaamini kuwa badala ya kukiita Chama cha Mapinduzi kana kwamba kina mapinduzi yoyote ni vizuri kukiita Chama Chahitaji Mapinduzi kwani jinsi kilivyo sasa hakiwezi kuendelea mbele bila mabadiliko makubwa ya ndani.
Kauli za Nape na zile za Katibu Mkuu wa CCM kuwa kumbe yale maneno ya kujivua gamba yalikuwa ni maneno tu na yasiyo na maana iliyotarajiwa zimenifanya niamini kuwa CCM inahitaji mapinduzi zaidi na labda ni mapinduzi ya kuvua magamba! Mapinduzi kwa kawaida ni kitu kigumu kama ilivyo kwenye kujivua magamba na wakati mwingine yanakuja na maumivu sana kama ilivyo kujivua magamba hivyo haiwezi kujivua magamba kiukweli kama haiko tayari kupitia hatua zote stahiki na kuleta mapinduzi wanayoyataja kila siku kwenye jina la chama chao.
Mimi ninavyoangalia hadi hivi sasa sioni ni nani ndani ya CCM anayeweza kuleta mapinduzi? Kule Misri na Tunisia walioleta Mapinduzi yaliyosababisha mabadiliko ya utawala ni vijana. Tatizo hapa kwetu vijana wenyewe wa CCM ndio wanaonekana kama sehemu ya magamba yenyewe!Vijana wa CCM ndio wa kwanza kutokea na magambaz yao ya kijani na njano kushangalia chama chao na hata wakianza kuzungumza maneno ya mabadiliko hawachelewi kuanza kupingana wenyewe kwa wenyewe.
Je, yawezekana watakaoleta mapinduzi ndani ya CCM watakuwa ni wazee waliochoshwa na siyo vijana? Ja yawezekana wazee ndio wanaona hasa mahitaji ya mabadiliko makubwa ndani ya CCM na siyo vijana? Je vijana walioko CCM ambao hawaoni haja ya mapinduzi ndani ya chama chao wanaweza kuwa tumaini la CCM huko mbeleni hasa katika siasa zetu zinazoonekana kubadilika kwa haraka kila siku?
Je bila Mapinduzi CCM inaweza kusurvive huko mbeleni? Au wameridhika kwa kujiita tu Chama cha Mapinduzi bila kuwa na Mapinduzi yoyote zaidi ya jina? Au wanafikiria mapinduzi ni jina la heshima tu bila kuwa na maana? Kama mapinduzi ya kweli na yenye manufaa hawajawahi kushiriki na wala hawana mpango wa kujipindua angalau wabadili tu hata jina liendane na wanayofanya.Nadhani wakati umefika CCM ibadili jina kabisa; isiwe kitu chochote mapinduzi na kiwe CCM -Chama cha Matanuzi!
Sote tunajua kinachojiita Chama cha Mapinduzi hakijawahi kufanya mapinduzi yoyote. Neno mapinduzi kwa kadiri ninavyoelewa linaashiria mabadiliko ya haraka ya kisiasa wakati mwingine hata kumwagika damu au vurugu kama tulivyoona kule Misri na Tunisia. Katika nchi yetu mabadiliko ya aina hiyo yalitokea Zanzibar lakini hadi hivi sasa mjadala bado upo juu ya nani hasa walihusika. TANU tunajua haikuhusika (japo kwa wazi) na ASP kwa kadiri ninavyosoma humu inaonekana walidandia tu mbele ya safari.
Sasa kwanini CCM inajiita Chama cha Mapinduzi kama hakijawahi kushiriki mapinduzi yoyote? Ninaamini kuwa badala ya kukiita Chama cha Mapinduzi kana kwamba kina mapinduzi yoyote ni vizuri kukiita Chama Chahitaji Mapinduzi kwani jinsi kilivyo sasa hakiwezi kuendelea mbele bila mabadiliko makubwa ya ndani.
Kauli za Nape na zile za Katibu Mkuu wa CCM kuwa kumbe yale maneno ya kujivua gamba yalikuwa ni maneno tu na yasiyo na maana iliyotarajiwa zimenifanya niamini kuwa CCM inahitaji mapinduzi zaidi na labda ni mapinduzi ya kuvua magamba! Mapinduzi kwa kawaida ni kitu kigumu kama ilivyo kwenye kujivua magamba na wakati mwingine yanakuja na maumivu sana kama ilivyo kujivua magamba hivyo haiwezi kujivua magamba kiukweli kama haiko tayari kupitia hatua zote stahiki na kuleta mapinduzi wanayoyataja kila siku kwenye jina la chama chao.
Mimi ninavyoangalia hadi hivi sasa sioni ni nani ndani ya CCM anayeweza kuleta mapinduzi? Kule Misri na Tunisia walioleta Mapinduzi yaliyosababisha mabadiliko ya utawala ni vijana. Tatizo hapa kwetu vijana wenyewe wa CCM ndio wanaonekana kama sehemu ya magamba yenyewe!Vijana wa CCM ndio wa kwanza kutokea na magambaz yao ya kijani na njano kushangalia chama chao na hata wakianza kuzungumza maneno ya mabadiliko hawachelewi kuanza kupingana wenyewe kwa wenyewe.
Je, yawezekana watakaoleta mapinduzi ndani ya CCM watakuwa ni wazee waliochoshwa na siyo vijana? Ja yawezekana wazee ndio wanaona hasa mahitaji ya mabadiliko makubwa ndani ya CCM na siyo vijana? Je vijana walioko CCM ambao hawaoni haja ya mapinduzi ndani ya chama chao wanaweza kuwa tumaini la CCM huko mbeleni hasa katika siasa zetu zinazoonekana kubadilika kwa haraka kila siku?
Je bila Mapinduzi CCM inaweza kusurvive huko mbeleni? Au wameridhika kwa kujiita tu Chama cha Mapinduzi bila kuwa na Mapinduzi yoyote zaidi ya jina? Au wanafikiria mapinduzi ni jina la heshima tu bila kuwa na maana? Kama mapinduzi ya kweli na yenye manufaa hawajawahi kushiriki na wala hawana mpango wa kujipindua angalau wabadili tu hata jina liendane na wanayofanya.Nadhani wakati umefika CCM ibadili jina kabisa; isiwe kitu chochote mapinduzi na kiwe CCM -Chama cha Matanuzi!