Chama Cha Mapinduzi TUKAZE BUTI


Hizi ni bhange, tena bhange ya Iringa nasikia ukiivuta iyo inakufanya ufyatuke na uozo wa mawazo ya aina hii.

Kama kanu baada ya kuishinda CCM tutaizika, Jaji kesi ya Igunga kashindwa kuchakachua kwani anajua 2015 atakuwa chini ya Gvt tukufu ya CDM
 

Ni sawa kama unayoyasema yanatoka moyoni, lakini kama ni unafiki basi.
 

Tatizo la CCM kwa sasa ni wao kuchukulia uongozi kama sehemu ya kupeana kula. Kama ingekuwa hivyo sivyo Nape angekwishwa pumzishwa na Sofia Simba au Anna Kilango wasingekubaliwa kupitishwa majina yao
 
Mwanzoni ulionekana ukiongea kama mtu mwenye busara, lakini kwa hili la sasa unaongea kama mwenda wazimu.

Siamini kama kukifagilia chama cha mapinduzi ni kukosa busara. Inawezekana kabisa kuamini kila linalosemwa na CDM ni kulemaa kwa ubongo, haiwezekani chama ambacho hakijawahi kuongoza nchi ukakiamini kiasi hicho. yanayoendelea nchi za LIBYA, TUNISIA na Misri ni mifano hai ya hivi vyama ambavyo vinatumia kila aina ya njia kuhakikisha vinawalaghai wananchi.
 
Ushauri mzuri,tatizo ccm hawayaoni hayo wamebakia kushinda kwenye majukwaa kubishana na chadema,wanapaswa kutambua kwamba tatizo la watu kuichukia ccm sio chadema bali baadhi ya watu waliopo ccm ni hopeless,mfano kiongozi km mwigulu kwa kitendo cha kumvisha mbwa bendera ya chadema anadhani kinawafurahisha watu kumbe anajichafua zaidi
 
Hizi ni bhange, tena bhange ya Iringa nasikia ukiivuta io inakufanya ufyatuke na uozo wa mawazo ya aina hii.
Kama kanu baada ya kuishinda CCM tutaizika, Jaji kesi ya Igunga kashindwa kuchakachua kwani anajua 2015 atakuwa chini ya Gvt tukufu ya CDM
Hivi wewe na MAFILILI nani anatumia bangi? Huna sababu ya kutukana, jibu hoja za bwana MAFILILI badala ya kutukana. Alichokisema MAFILILI ni sawa kabisa hasa ukizingatia kuwa hivyo vyma unavyodhania ni zaidi ya CCM havijawahi kuongoza nchi tukaona vimetufikisha wapi.
 

Unajua kama kweli unataka CCm ikaze buti na kusonga mbele, then una maanisha wooote waliokwenda kinyume nyume na sababu za kuzaliwa CCm mwaka 1977 wajirudi!!!

Wakijirudi hao au pengine wachache kati yao, basi chama kinameguka, kikimeguka kinapoteza ukubwa na kugawana kura, hapo ndipo tutakapojua siri zooote za ushindi wenu, hayo yakianikwa mnapoteza dola.

It is only when tha happens, ndo CCM itarudi kuwa ya wakulima na wafanya kazi!!! Period mazee. Sisi wengi wetu hatuna cha kufanya zaidi ya kuwahamasisha wana vijiji wenzetu wajitokeze wengi kupiga kura na kukataa vijizawadi...
 
Mwanzoni ulionekana ukiongea kama mtu mwenye busara, lakini kwa hili la sasa unaongea kama mwenda wazimu.

Ha ha ha ha ha! Mkuu hawa jamaa (magamba) ndio zao. Hoja ikashakuwa hot wako tayari kufanya lolote hata kuvua nguo hadharani ni kawaida sana kwao.
 

pendekeza another approach, kila kukicha chuki inaongezeka dhidi yake kwa kushindwa
 

busara haipatikani anapokuwepo chenge wewe! Au wadhani mkaahapa ana chembe ya busara, muulizeni net group solution ilikuja na uwekezaji mtaji kiasi gani pale tanesco.

Msaidie kujibu kama waweza.
 


ulipoanza ulianza vizuri na kwa busara za kuonyesha ili CCM iweze kubalika vizuri ni bora wakajibadilisha cha ajabu haya uliyoyasema hapo juu ndio chanzo cha kushindwa kwa CCM sababu hutaki kubadilika. naomba ujiulize swali moja ni kwa nini watanzania wengi wana bweteka na vyama vya msimu na ni kwa nini wanaamini vyama vya msimu kuwaongoza ili hali hawajawahi kushika hatamu ya nchi toka uhuru.

ili kukusaidia jibu ni kwamba CCM inaongozwa na wale wale, kwa mtindo ule ule na kwa akili zile zile kufikia hata ndani ya chama mnayumba kwa sababu zile zile, mtindo ule ule na akili zile zile.
 
labda wakaze yebo yebo,jana nimeona ofice yao ya kisutu imebomolewa na NHC! WALIJUA NHC HAWAWEZI SABABU WAO NDO KILA KITU,SASA NAONA WAMESHITUKA KIDOGO.PIA WATENDAJI WAO NDO WANZIDI KUHARIBU,KAMA HUAMINI FATILIA ISSUE NZIMA YA SENSA ETI WAKUU WA WILAYA NDO KILA KITU WANAIBA MPAKA POSHO,
 

Natamani wangekusikiliza; lakini wahenga walisema "Sikio la kufa halisikii dawa" kwa bahati mbaya CCM has to die first before it gets reborn, kama kuna kitu kama hicho!!!

Kujenga hoja za kuibomoa CDM ni vigumu kwa sababu tuhuma zinazowakabili wao hazisafishiki hata kwa magadi; wapiga kampeni zaidi ya hao uliowataja ni hakuna kwani wengi wao ni wachafu kuliko maelezo; CCM lazima ife kama vyama vingine vyote (post independence political parties) katika ukanda huu wa afrika mashariki vilivyokufa; KANU (Kenya), UPC (Uganda), MCP (Malawi), UNIP (Zambia) etc..
 
Wanaoharibu chama hawa wakina Nape & yule muhuni wa mtera anayepanda jukwaani na kuanza kuporomosha matusi badala ya kumwaga sera. CCM inapigwa nyundo sana kwa sasa kutokana na makosa yake yenyewe. Chama kimetoka kwa wakulima na wafanyakazi kimeingia kwa mabepari. Matokeo yake hata kwenye kampeni inabidi watumie muda mwingi kujitetea kuliko kutangaza sera.Wakubali moja wapitishe fagio wakirudishe chama kwa wananchi au waache kife taratibu kama hivi sasa.
 
so late. kuirudisha mioyo ya watanzania kwa ccm ni kazi kubwa kuliko kumlazimisha ng'ombe kunywa maji wakati hana kiu ya maji
 
thats great of u! maana lila k2 mimekuwa siasa
 
Wakati wenzao wa CHADEMA wanafanya siasa ya uhakika wakivuna wanachama wapya usiku na mchana.

CCM wao wamebaki kuvalisha mbwa bendera na kupanga mikakati ya propaganda na fujo.

CCM haiwezi kubadilika na siku ikitoka madarakani na kufa inakufa.
 
Heshima sana MAFILILI

Matatizo yanayoikumba CCM ni kuacha misingi yake ya kuwasemea wanyonge au kwa lugha nyingine wakulima na wafanyakazi.Mwl Nyerere katika uhai wake aliwahi kukionya chama cha mapinduzi lakini viongozi wake kuanzia ngazi ya juu taifa hadi mashinani hawakumwelewa.Kuwalaumu Nape,Mwigulu au viongozi wa CCM ni kuwaonea bure,viongozi wote wa CCM wanatumikia mfumo wa kuwaabudu na kuwalinda matajiri bahati mbaya wengi wa matajiri wamekwapua mali za umma.

CCM ya leo inaangamia si kwasababu CDM ni chama chenye sera nzuri bali wananchi wengi wanaona ni afadhali kuiweka CCM kando kwakuwa kimeshindwa kulinda rasilimali za taifa,kimeshindwa kuwafikisha mbele ya sheria wezi wa mali za umma,kimeshindwa kuondoa umasikini,kimeshindwa kufuta ujinga,kimeshindwa kuwahakikishia waTanzania masikini upatikanaji wa huduma bora za afya.Huduma bora za afya zinawekezwa India kwaajili ya tabaka la watawala [wabunge,mawaziri,makatibu wakuu,majaji,makamishna,wakurugenzi na nk].Tabaka hili pia limehakikishiwa kipato kizuri.

Baada ya CCM kushindwa kuwahudumia vyema waTanzania kimekimbilia sera za kuwagawa waTanzania kwa misingi ya dini,ukabila na ukanda ili kujijengea uhalali wa kuendelea kutawala.Hii si mara ya kwanza CCM kukimbilia Masheikh kutoa matamko ya kutugawa imefanya hivyo mara nyingi sana ndiyo maana tunaona leo Sheikh Ponda akiwakataza waIslam wasishiriki sensa anajua serekali ya CCM imekuwa mbia wa muda mrefu kuhalalisha makosa yao ndani ya jamii pana.


 
Last edited by a moderator:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…