CHADEMA ni chama kinachoendeshwa kwa
misingi ya ulaghai. Chama kama hiki mtu yeyote
atakayetaka kukiunga mkono kwa hoja anajikuta
anakwazika. Hii imesababisha CHADEMA
kuungwa mkono zaidi na makundi mawili ya
watanzania:
1. wale ambao ni bendera fuata upepo.
2. wale wenye malengo ya kupanda haraka na
kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa.
Nitayachambua makundi haya mawili kama
ifuatavyo:
1. Wale ambao ni bendera fuata upepo. Katika
kundi hili kuna watu wa aina tatu:
i) Wale ambao wamedanganyika na propaganda
kuwa chadema ni chama cha kikabila au cha
kikanda na kwa vile wao wanatoka kwenye
kanda hizo basi wanajisikia ukaribu zaidi na
chadema. Hapa utaona kuwa propaganda za
kukichafua chama kuwa ni cha kikabila au cha
kikanda kimeweza kuwaongezea chadema nguvu
katika maeneo inayoshutumiwa kuyapendelea.
ii)Wale ambao wamelaghaika na propaganda za
kuwa chadema ni chama cha udini. Kuna
waumini wengi wameviunga mkono vyama vya
chadema na CUF kwa sababu tu wamekuwa
wakisikia kuwa vyama hivyo vinashabiiana na
dini zao. Hawa ni bendera fuata upepo ambao
hawachuji ukweli wa taarifa na hawajiulizi
chama kinaweza kuwanufaishi vipi kama
waumini wa dini husika.
iii)Kundi la tatu katika bendera fuata upepo ni
vijana ambao wanaona kuwa chadema ni kama
fashion. Ukikaa nao chini vijana hawa kuwauliza
kwanini wanaiunga mkono chadema hawana
lolote la kuongea. Mfano wa watu waliomo
kwenye kundi hili ni members wa jamiiforums
ambao hurusha matusi kwa kila mtu anayehoji
jambo juu ya chadema.
Makundi haya matatu ya bendera fuata upepo
huwa ni rahisi sana kuvunjwa moyo na
kukikimbia chama mara tu upepo utakapoelekea
upande tofauti. Kwa mfano, iwapo chadema
itafanya jitihada za kuhakikisha jamii inajua
ukweli kuwa siyo chama cha ukanda wala
ukabila, basi makundi haya mawili i) na ii)
yatatoweka.
Vilevile iwapo chadema itasambaza elimu ya
uraia na kuwawezesha wananchi kuchagua
vyama vyama vya kuviunga mkono kwa hoja,
basi makundi yote iii),ii) na i) itayapoteza.
Hizi ni changamoto zinazohitaji political
calculations kudeal nazo.
2. Wale wenye malengo ya kupanda haraka na
kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa:
Katika kundi hili wamo wanasiasa kama Dr.
Wilbroad Slaa na Shibuda. Misingi ya wanasiasa
wa aina hii kuhama kutoka kwenye chama
kimoja mpaka kingine ni kuhakikisha tu kuwa
wanaendelea kuwepo kwenye shughuli za kisiasa
katika nafasi za uongozi. Hawana ugomvi wa
kiitikadi na CCM.
Kimsingi hawa ni watu ambao iwapo leo hii CCM
itawahakikishia kuwa watapata fursa ya kuwa
viongozi wa juu, basi wako tayari kujiunga nayo.
Wamejitoa CCM kwa sababu tu walinyimwa
fursa ya kuwa viongozi katika ngazi
walizogombea. Iwapo chadema itawanyima fursa
ya kuwa viongozi, wataikimbia pia.
Mfano mzuri umeonekana hivi karibuni Lushoto
ambaye kijana mpya katika siasa Deogratius
Kisandu aliikimbia chadema kwa kukosa fursa
za uongozi ambapo kimsingi alijiunga chadema
kwa kuamini kuwa fursa hizo atazipata kwa
urahisi zaidi ndani ya chama hicho.
CHADEMA imekosa uungwaji mkono katika
misingi ya itikadi. Hii imesababishwa na ukweli
kwamba cHADEMA imechukua itikadi zilezile za
CCM, TANU na ASP na kushindwa kuwapa
wananchi chaguo jipya. Zaidi ya hayo, hata
kwenye ilani za uchaguzi za chadema hakuna
offer tofauti na zile ambazo wananchi wanapewa
na CCM. Kuthibitisha hili, chadema imepata
wakati mgumu sana kupokelewa katika maeneo
ambayo kuna chama kingine cha upinzani
kilichojijenga kama Zanzibar. Iwapo chadema
wangekuwa na itikadi au sera mpya ambazo
utekelezaji wake unaelezeka, isingekuwa vigumu
kupata wafuasi katika maeneo hayo.
Kwa vile CCM imeshapewa fursa ya kutawala,
mapungufu yake yameonekana. Jukumu la
chadema kwenye hili linatakiwa ni kuja na
mkakati unaoelezea kwa undani ni vipi
watafanya tofauti na CCM. Badala yake, kazi
pekee inayofanywa na chadema ni kuainisha
matatizo na kuyahubiri majukwaani bila kuelezea
iwapo wana mkakati wowote mpya ili wananchi
waupime. Hii inasababisha hata wasomi
wanapovifananisha hivi vyama wanakosa zile
tofauti za kuzijadili na mwishowe hujadili tabia
za viongozi vya vyama na utendaji wao badala
ya kujadili sera zake na itikadi.
Ulaghai wa CHADEMA ni sababu nyingine
iliyofanya chama hiki kupoteza wafuasi makini.
Mtu yeyote atakayejaribu kuichunguza chadema
kidogo tu atagundua kuna mambo mengi
yasiyofaa yanayofanywa na viongozi wake.
Viongozi hawa hufanya hivi kujinufaisha wao
wenyewe na familia zao. Kwa vile umaarufu wa
chadema umetokana na uhubiri wa ufisadi,
uwepo wa ufisadi ndani ya chadema
umewavunja sana moyo wananchi walioamini
kuwa wamepata tumaini jipya. Wale
wanaoishabikia chadema kwa kufuata upepo
wanapojua ulaghai huu, huvunjwa moyo na
kuikimbia. Mfano wa hili ni kijana Mtela
Mwampamba ambaye aliamini kuwa chadema ni
tumaini jipya mpaka pale alipojionea mwenyewe
kwa macho yake uhalisia wa mambo ndani ya
chama hicho.
Hapa nitaainisha baadhi ya mambo
yanayoiondoa CHADEMA usoni na moyoni mwa
watanzania wanaotaka chama kinachopinga
ufisadi.
1. Mmiliki wa jengo lililopangishwa na CHADEMA
Kinondoni kama ofisi za makao makuu na bei ya
pango kwa mwezi vimefanywa siri. Mara kadhaa
swali hili limeibuliwa lakini hakuna jibu lililoweza
kutolewa na uongozi wa CHADEMA.
2. Wanachama walioomba fursa ya kushiriki
tenda ya kununua magari ya chama
wamenyimwa fursa hiyo na hatimaye tenda hiyo
imetolewa kwa usiri mkubwa. Chris
Lukosi amekuwa akishutumiwa kuwa sababu ya
kujitoa kwake CHADEMA ni kunyimwa tenda hii,
lakini pale wadau walipohoji baada ya Lukosi
kunyimwa tenda hiyo ni nani amepewa na kwa
vigezo vipi?, kinaibuka kigugumizi.
3. Swala la Katibu Mkuu wa chama kujikopesha
mamilioni ya shilingi zilizochangwa na walalahoi
kwa ajili ya shughuli za chama. Ikumbukwe
kuwa watu waliochangia M4C walifanya hivyo
kwa vile waliamini kuwa michango yao
itakiwezesha chama kujiimarisha. Taarifa kuwa
pesa zimetumika kifisadi zimewavunja watu
moyo.
4. Taarifa za Josephine Mushumbusi kulipwa
mamilioni ya shilingi za chama kwa kazi
anayoiita ya kujitolea. Wadau walihoji kuwa na
wao wangependa kujitolea kwenye shughuli za
chama ili walipwe hayo mamilioni. Ilidhihirika
kuwa Josephine alipata fursa hiyo kwa
upendeleo.
5. Pesa za ruzuku zimekuwa zikiishia Makao
Makuu. Watendaji wa chama mawilayani
wamekuwa wakifanya kazi bila nyenzo. Hii
ilisababisha mpaka kukawa na mtafaruku huko
Mpanda kwa kukosa ofisi ya wilaya ambayo
kimsingi ni jukumu la chama makao makuu
kuhakikisha chama kina ofisi za wilaya.
Ikumbukwe pia kuwa matumizi haya mabaya ya
fedha yalikuwa sababu ya mvutano wa kisiasa
kati ya marehemu Chacha Wangwe na kiongozi
Mkuu wa Chama.
6. Kumekuwa na taarifa za matumizi mabaya ya
pesa za Sabodo jambo ambalo limeelezewa
kuwa sababu ya kumfanya Sabado kuahirisha
ahadi yake ya kuijengea CHADEMA ofisi za
makao makuu na chuo cha siasa.
7. Katibu Mkuu wa CHADEMA ni miongoni mwa
washutumiwa wa ufisadi wa mamilioni ya pesa
za mradi wa maji wa Karatu.
8. Viti Maalum vya ubunge vimetolewa kwa
upendeleo ambapo akinamama waliojitolea
kukijenga chama wameachwa pembeni na nafasi
hizo kupewa akinamama walio karibu na
viongozi wa juu wa chama. Hapa ikumbukwe
kuwa mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la
CHADEMA (BAWACHA) wa Taifa alishinda nafasi
ya uchaguzi wa viti maalum, lakini akatolewa
kwa kuambiwa kuwa hajakidhi vigezo vya kuwa
mbunge ingawa amewaongoza wanawake
wenzake kwa muda mrefu ndani ya chadema.
Wakati huohuo mwanamama anayeishi
Marekani, Leticia Nyerere amepewa Ubunge wa
viti maalum kutokana na "kufahamiana" na
mwenyekiti wa chama. Hili limewavunja moyo
wengi walioanza kuiamini chadema.
9. Vijana kama zito walioonekana kuwa na
ari ya mabadiliko ndani ya chama wamekuwa
wakinyimwa nafasi ya kugombea uongozi
kinyume na katiba.
10. CHADEMA kukanusha kauli ya Nape kuwa
wanapewa msaada na chama cha siasa cha
Ujerumani, baadae ikadhihirika kuwa ni kweli
wanapokea msaada huo. Hii imedhihirisha kuwa
CHADEMA sio wawazi katika utendaji wao.
Wadau wanajiuliza chama hicho cha siasa
kinataka nini Tanzania mpaka kikipinge chama
kilichoasisiwa na wapigania Uhuru na kutaka
chadema iingie madarakani? Ikumbukwe kuwa
muasisi wa CHADEMA Mzee Mtei, alikataa
kushiriki harakati za kupigania uhuru na pia
alikataa kujitolea kuijenga nchi baada ya Uhuru.
11. Hesabu za pesa zinazochangwa na walalahoi
kwa ajili ya M4C imekuwa ni jambo la siri kubwa
ndani ya CHADEMA.