R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,578
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimezindua kampeni za udiwani kwa mbwembwe, ambapo wametumia helikopta kudondosha vipeperushi vyenye maelezo ya wagombea wao.
Madiwani hao wa kata za Kimandolu, Elerai, Kaloleni na Themi, walifukuzwa uanachama baada ya kudaiwa kukiuka maagizo ya vikao vya juu vya chama chao.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo, Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Arusha, Ephata Nanyaro alisema helikopta hiyo itaendelea kutumika muda wote wa kampeni za udiwani.
Mbunge wa Jimbo la Arusha mjini, Godbless Lemay alisema hatahudhuria vikao vya Bunge kwa kipindi chote cha kampeni, kuhakikisha chama hicho kinarejesha viti hivyo.
Alisema lengo la Chadema ni kuweza kuongoza halmashauri ya jiji baada ya kukinyanganya CCM kiti cha udiwani Kata ya Daraja Mbili, kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika mwaka jana.
CCM na Chadema zimeweka wagombea kwenye kata zote nne, lakini CUF inayoshiriki uchaguzi huo kimesimamisha wagombea katika kata tatu za Kaloleni, Elerai na Themi.
Kampeni za uchaguzi huo zinatarajiwa kugubikwa na vituko vilivyojaa ushindani kati ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) na chama hicho kikuu cha upinzani nchini. Chadema na CCM vimekuwa na mvutano wa kisiasa mara kwa mara mkoani humo.
Madiwani hao wa kata za Kimandolu, Elerai, Kaloleni na Themi, walifukuzwa uanachama baada ya kudaiwa kukiuka maagizo ya vikao vya juu vya chama chao.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo, Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Arusha, Ephata Nanyaro alisema helikopta hiyo itaendelea kutumika muda wote wa kampeni za udiwani.
Mbunge wa Jimbo la Arusha mjini, Godbless Lemay alisema hatahudhuria vikao vya Bunge kwa kipindi chote cha kampeni, kuhakikisha chama hicho kinarejesha viti hivyo.
Alisema lengo la Chadema ni kuweza kuongoza halmashauri ya jiji baada ya kukinyanganya CCM kiti cha udiwani Kata ya Daraja Mbili, kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika mwaka jana.
CCM na Chadema zimeweka wagombea kwenye kata zote nne, lakini CUF inayoshiriki uchaguzi huo kimesimamisha wagombea katika kata tatu za Kaloleni, Elerai na Themi.
Kampeni za uchaguzi huo zinatarajiwa kugubikwa na vituko vilivyojaa ushindani kati ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) na chama hicho kikuu cha upinzani nchini. Chadema na CCM vimekuwa na mvutano wa kisiasa mara kwa mara mkoani humo.