The Conquerer
Member
- Aug 16, 2012
- 79
- 94
Leo CHADEMA kimevunja rekodi katika mji mdogo wa Tunduma baada ya maelfu ya wakazi wa mji huo kuhudhuria kwa wingi mkutano wa hadhara uliohutubiwa na mbunge wa Musoma Mjini Mh. Vincent Nyerere akiwa na mwenyeji wake mbunge wa jimbo la Mbozi Magharibi Mh. David Silinde.
Katika mkutano huo, Mh.Nyerere alisema wakati umefika sasa wananchi kuchukua hatua na kukiondoa madarakani Chama cha Mapinduzi CCM kwa kuwa serikali yake ndiyo iliyowasababishia wananchi umasikini uliokithiri kwa kupora rasilimali za nchi na kuziuza kwa mabepari kwa bei chee kwa faida ya viongozi peke yake.
Mh. Nyerere amekemea tabia ya viongozi wa serikali kuwasomesha watoto wao nje ya nchi huku watoto wa masikini wakikosa huduma hiyo, na hivyo kujenga matabaka kati ya wenye elimu na wasio na elimu, matajiri na masikini jambo ambalo ni hatari kwa mustakabali wa amani ya taifa letu.
Aidha Mh. Vincent nyerere aliitaka serikali kuwajali wananchi bila kubagua kwa kuwa serikali ya sasa inawajali watu matajiri kuliko masikini. Hii ni kutokana na kuuwawa kikatili kwa mwanachama mmoja wa CHADEMA katika mji wa Tunduma tarehe 15/12/2012 na serikali haijachukua hatua yoyote.
Amemtaka mkuu wa polisi nchini inspekta Said Mwema kutuma jopo la wapelelezi ili kuwabaini wauwaji hao na kuchukua hatua kali kama alivyofanya kwa kifo cha aliyekuwa mkuu wa polisi mkoa wa Mwanza na wakubwa wengine.
Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Mbozi Magharibi, Mh. David Silinde alitumia mkutano huo kueleza mafanikio makubwa aliyoyapata kwa muda mfupi wa miaka miwili tangu ameingia madarakani. Ametaja miradi ya barabara, ujenzi wa madarasa ya shule, na miradi ya maji ambayo imefanikiwa chini ya uongozi wake akisaidiana na mh. Diwani wa tunduma nd. Frank Mwakajoka.
Tazama picha jinsi miamba miwili, mh. David Silinde (sauti ya simba) na mh. Vincent Nyerere mbunge wa Musoma Mjini walivyotingisha mji wa Tunduma.
Katika mkutano huo, Mh.Nyerere alisema wakati umefika sasa wananchi kuchukua hatua na kukiondoa madarakani Chama cha Mapinduzi CCM kwa kuwa serikali yake ndiyo iliyowasababishia wananchi umasikini uliokithiri kwa kupora rasilimali za nchi na kuziuza kwa mabepari kwa bei chee kwa faida ya viongozi peke yake.
Mh. Nyerere amekemea tabia ya viongozi wa serikali kuwasomesha watoto wao nje ya nchi huku watoto wa masikini wakikosa huduma hiyo, na hivyo kujenga matabaka kati ya wenye elimu na wasio na elimu, matajiri na masikini jambo ambalo ni hatari kwa mustakabali wa amani ya taifa letu.
Aidha Mh. Vincent nyerere aliitaka serikali kuwajali wananchi bila kubagua kwa kuwa serikali ya sasa inawajali watu matajiri kuliko masikini. Hii ni kutokana na kuuwawa kikatili kwa mwanachama mmoja wa CHADEMA katika mji wa Tunduma tarehe 15/12/2012 na serikali haijachukua hatua yoyote.
Amemtaka mkuu wa polisi nchini inspekta Said Mwema kutuma jopo la wapelelezi ili kuwabaini wauwaji hao na kuchukua hatua kali kama alivyofanya kwa kifo cha aliyekuwa mkuu wa polisi mkoa wa Mwanza na wakubwa wengine.
Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Mbozi Magharibi, Mh. David Silinde alitumia mkutano huo kueleza mafanikio makubwa aliyoyapata kwa muda mfupi wa miaka miwili tangu ameingia madarakani. Ametaja miradi ya barabara, ujenzi wa madarasa ya shule, na miradi ya maji ambayo imefanikiwa chini ya uongozi wake akisaidiana na mh. Diwani wa tunduma nd. Frank Mwakajoka.
Tazama picha jinsi miamba miwili, mh. David Silinde (sauti ya simba) na mh. Vincent Nyerere mbunge wa Musoma Mjini walivyotingisha mji wa Tunduma.