Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Mbeya Kusini magharibi mwa Tanzania kimetangaza kuvunja rasmi kambi iliyokuwa imewekwa kushinikiza kupatikana kwa kada wao, Mdude Nyagali aliyetoweka tangu Mei 02, 2025.
Mdude anadaiwa kuvamiwa na kupigwa nyumbani kwake mtaa wa Iwambi jijini Mbeya tangu Mei 2, 2025 hajapatikana huku Chadema ikitumia njia tofauti kumtafuta mwanaharakati huyo bila mafanikio.
Akizungumza leo Jumatano Mei 21, 2025 Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya, Masaga Kaloli amesema baada ya kupata vitisho ikiwamo kumwagiwa vitu vinavyodhaniwa kuwa ni sumu, wameona harakati za kumpigania Mdude zihamie nyumbani ili kuokoa maisha ya wengine.
Amesema zipo njia nyingi za kuendelea kupambania kila mwananchi na mfuasi wa chama hicho na Mbeya itaendelea kuwa mfano kupitia tukio la Mdude. Masaga pia aliiomba Serikali na vyombo vya dola kusaidia kupatikana kwa mwanaharakati huyo.
Pia, Soma
"Tumeona kuendelea kuwa hapa ilihali tunapitia vitisho vyenye nia ovu bora tutumie njia nyingine kudai haki ya Mtanzania huyu, hadi sasa tunaomba Serikali na mamlaka nyingine zisaidie kupatikana kwa Mdude, sisi tutatoa aina yoyote ya ushirikiano kwa yeyote" amekaririwa Masaga akizungumza na Gazeti la Mwananchi.
Mdude anadaiwa kuvamiwa na kupigwa nyumbani kwake mtaa wa Iwambi jijini Mbeya tangu Mei 2, 2025 hajapatikana huku Chadema ikitumia njia tofauti kumtafuta mwanaharakati huyo bila mafanikio.
Akizungumza leo Jumatano Mei 21, 2025 Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya, Masaga Kaloli amesema baada ya kupata vitisho ikiwamo kumwagiwa vitu vinavyodhaniwa kuwa ni sumu, wameona harakati za kumpigania Mdude zihamie nyumbani ili kuokoa maisha ya wengine.
Amesema zipo njia nyingi za kuendelea kupambania kila mwananchi na mfuasi wa chama hicho na Mbeya itaendelea kuwa mfano kupitia tukio la Mdude. Masaga pia aliiomba Serikali na vyombo vya dola kusaidia kupatikana kwa mwanaharakati huyo.
Pia, Soma
"Tumeona kuendelea kuwa hapa ilihali tunapitia vitisho vyenye nia ovu bora tutumie njia nyingine kudai haki ya Mtanzania huyu, hadi sasa tunaomba Serikali na mamlaka nyingine zisaidie kupatikana kwa Mdude, sisi tutatoa aina yoyote ya ushirikiano kwa yeyote" amekaririwa Masaga akizungumza na Gazeti la Mwananchi.