CHADEMA Yatikisa Morogoro

CHADEMA Yatikisa Morogoro

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
CHADEMA ilisababisha shughuli kusimama kwa zaidi ya saa 3 katika Kata ya Tungi Morogoro wakati mgombea Udiwani wa Chama hicho Juma Tembo alipokuwa anachukua Fomu za kugombea Udiwani.

Mgombea huyo alisindikizwa kwa Msururu wa Pikipiki na Magari huku umati mkubwa wa watu ukiwa umejipanga kando kando ya barabara zote kumpungia mgombea huyo.Alipofika kwenye ofisi ya serikali mgombea huyo alikuta maelfu ya watu wakiwa wanamsubiri katika eneo hilo.

Akihojiwa baada ya kuchukua Fomu sababu ya kusindikizwa na Umati huo mgombea huyo Juma Tembo alisema hiyo ni kutokana na Imani kubwa wananchi waliyo nayo kwa CHADEMA.Mgombea huyo alisema ana uhakika mkubwa wa kushinda kiti hicho.

Source:Nipashe.
 
Tunakushukuru sana kamanda kwa taarifa hii , binafsi namfahamu mgombea huyo , ni mtu makini sana na anakubalika mno , namshauri mgombea wa ccm ili kutunza heshima yake ni bora ajitoe .
 
Mkuu ebu toa ufafanuzi kuna limsukule limekuja na hbr za kua eti katekwa na kapigwa sana huyu mgombea wetu
 
Mkuu ebu toa ufafanuzi kuna limsukule limekuja na hbr za kua eti katekwa na kapigwa sana huyu mgombea wetu

Mkuu hizo ni Porojo za Magamba baada ya kuona wameshashindwa kabla ya kuanza kampeni.
 
Afande Sele alikuwepo kumpiga tafu?

Kwanini Jaji Damiani Lubavu hutaki kuboresha daftari la wapiga kura tuizike CCM mchana kweupe?!
 
Afande Sele alikuwepo kumpiga tafu?

Kwanini Jaji Damiani Lubavu hutaki kuboresha daftari la wapiga kura tuizike CCM mchana kweupe?!

Watu wana Imani na Chadema kama Taasisi mpaka inakuwa raha.
 
Watu wa Tungi wanateseka sana hawajawahi kuona matunda ya Uhuru. Umeme mradi umekwisha lakini Tanesco wameshindwa kuwaunganishia wananchi meta hadi rushwa itendeke. maji ni bidhaa adimu. ni vema wakaamua kufanya maamuzi ya kupata mchapa kazi au kuendelea na shida zao.
 
huo ni mwanzo tu bado,wasubiri serikali za mitaa tutawapiga mchana kweupee ndio watajua chadema sio zito
 
Watu wa Tungi wanateseka sana hawajawahi kuona matunda ya Uhuru. Umeme mradi umekwisha lakini Tanesco wameshindwa kuwaunganishia wananchi meta hadi rushwa itendeke. maji ni bidhaa adimu. ni vema wakaamua kufanya maamuzi ya kupata mchapa kazi au kuendelea na shida zao.

ina maana huyu diwani ndo atawaletea umeme.atatatua shida zao?kesho tu akipata udiwani atawageuka.nyie chadema mkishashinda mkiulizwa ahadi mlizotoa mnasimgizia hamuwezi kutekeleza kwwa sababu hamna dola? hiyo ni danganya toto tu
 
2014 na 2015 panya wote lazima waishe. maana hii operation sio ya nyau peke yake chui na simba nao wameamua kuingia kazini maana nao ni paka pia.
 
Back
Top Bottom