CHADEMA yasikitishwa na kifo cha Spika Mstaafu Job Ndugai, Yatuma salamu za Rambirambi

CHADEMA yasikitishwa na kifo cha Spika Mstaafu Job Ndugai, Yatuma salamu za Rambirambi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
137,304
Reaction score
271,567
Taarifa ya Chama hicho iliyosambazwa kote Duniani hii hapa.
===================
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai, kilichotokea tarehe 6 Agosti 2025 jijini Dodoma.

Soma Pia: Job Ndugai, aliyewahi kuwa Spika wa Bunge afariki Dunia

Mhe. Ndugai aliwahi kulitumikia Taifa akiwa Mbunge wa Jimbo la Kongwa, Naibu Spika, na baadaye Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Alikuwa sehemu ya uongozi wa Bunge katika kipindi cha mabadiliko ya kisiasa na mijadala muhimu ya kitaifa.

Chadema tunatoa pole za dhati kwa familia ya Marehemu, wananchi wa Jimbo la Kongwa, marafiki na wote walioguswa na msiba huu.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe. Amina.

Screenshot_2025-08-06-21-11-50-1.png
 
Huyu ni Spika wa hovyo kuwahi kutokea, yeye alikuwa kinara wa kuminya uhuru wa mawazo, hoja kinzani na demokrasia bungeni. Huyu ndie alikuwa nyuma ya "Covid 19".

Huyo ndie alie "injinia" Lissu kufukuzwa ubunge na kunyimaa mafao. Chadema hawakupaswa kuandika taazia ya mtu huyo. Dikteta wa mhimili wa bunge.
 
Huyu ni Spika wa hovyo kuwahi kutokea, yeye alikuwa kinara wa kuminya uhuru wa mawazo, hoja kinzani na demokrasia bungeni. Huyu ndie alikuwa nyuma ya "Covid 19".

Huyo ndie alie "injinia" Lissu kufukuzwa ubunge na kunyimaa mafao. Chadema hawakupaswa kuandika taazia ya mtu huyo. Dikteta wa mhimili wa bunge.
Mchawi mpe mwanao akulelee
 
🤣🤣🤣🤣😭🤣🤣🤣🤣 wanatoa pole huku moyoni wanafurahi.

Unafiki na siasa ni pete na kidole.

Hakuna haja ya kuwa mnafiki huyu ndugai hakuna wa kumuhurumia .kifo ni kifo tu
 
Taarifa ya Chama hicho iliyosambazwa kote Duniani hii hapa.
===================
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai, kilichotokea tarehe 6 Agosti 2025 jijini Dodoma.

Soma Pia: Job Ndugai, aliyewahi kuwa Spika wa Bunge afariki Dunia

Mhe. Ndugai aliwahi kulitumikia Taifa akiwa Mbunge wa Jimbo la Kongwa, Naibu Spika, na baadaye Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Alikuwa sehemu ya uongozi wa Bunge katika kipindi cha mabadiliko ya kisiasa na mijadala muhimu ya kitaifa.

Chadema tunatoa pole za dhati kwa familia ya Marehemu, wananchi wa Jimbo la Kongwa, marafiki na wote walioguswa na msiba huu.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe. Amina.

View attachment 3434217
Chadema waungwana sana.
 
Huyu ni Spika wa hovyo kuwahi kutokea, yeye alikuwa kinara wa kuminya uhuru wa mawazo, hoja kinzani na demokrasia bungeni. Huyu ndie alikuwa nyuma ya "Covid 19".

Huyo ndie alie "injinia" Lissu kufukuzwa ubunge na kunyimaa mafao. Chadema hawakupaswa kuandika taazia ya mtu huyo. Dikteta wa mhimili wa bunge.
Kweli alivyoingia alotangaza kifo chake alifanya nn na hao covid, hivi kwanza bunge lipo ama lishavunjwa maana najichanganya vile
 
Back
Top Bottom