Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Uanaharakati ndio hasa siasa za chadema na ni ngumu kutoka kwa uongozi uliopo.1) Kupunguza uanaharakati kujipanga kuongoza
2) Uongozi ngazi za vijiji wapewa meno kuamua
3) Makao makuu wabaki na sera na mbinu mpya kupata viongozi
4) Halmashauri zao kuwa mfano wa kuigwa
5) Wataka kodi za majengo zibaki kwenye kata.
Hapa hakuna MaigizoUanaharakati ndio hasa siasa za chadema na ni ngumu kutoka kwa uongozi uliopo.
Asante sana wazee wa ku copy naona mapovu yanawatoka maana mwisho wa maigizo umefikaSafi sana siku zote mabadiliko huwa yanakuwa na faida na hasa yanayoletwa bila shinikizo bali kwa ubunifu, hongera chadema
Unawaza kimaigizo maigizohata mtembee kichwa chini miguu juu: chadema ni ile ile ya kisanii.
Hapo kwenye akili zao ndio balaa
Kijana unapoelekezwa tulia,usipaniku
unaweza thibitisha madai yako au unaropoka tu usiyoyajua
Huko ugambani MBOWE kutokuwa na BEI anawakosesha AMANI kweli kweliWarekebishe yafuatayo kama kweli wana nia ya kuaminika kupewa nchi
1. Mwenyekiti achaguliwe mwingine maana Mbowe muda wake uliisha akabadili katiba kujiongezea muda
2. Uteuzi wa mgombea urais uwe huru na wa kidemokrasia, watu wahamasishwe kuchukua form za urais ili mgombea achguliwe kutoka katika orodha ya wagombea kadhaa, na siyo kumwekea Lowasa siti ya upendeleo
3. Waache kutetea watu waofukuzwa kwa ubadhilifu na warudi kwenye sera ya kupinga ufisadi
4. Wajikite katika kufanya siasa za ukweli na siyo za utapeli
Hapa Ndipo ninapo Mvulia Kofia Ndugu Lowassa. Huyu ni Bonge la Kiongozi, kwa Mipango yake na Mikakati yenye Dira hakika CHADEMA Kitafanya Kazi Nzuri sana.
Wajipange Vizuri katika Almashauri walizozipata, wawatumikie wananchi kwa ufanisi Mzuri na Maendeleo yaonekane yasiwe Midomoni, wapange kamati moja ya Kutoa Mrejesho kwa Wananchi kwa kazi walizozifanya na Mafanikio yaliyo waletea wananchi husika katika miji na Majiji wanayo yaongoza.
Chama kishuke sasa kwa wananchi, kiwe karibu na Wananchi kwa kuonyesha Dira kama Chama kinachotafuta kuongoza Dola.
Warekebishe yafuatayo kama kweli wana nia ya kuaminika kupewa nchi
1. Mwenyekiti achaguliwe mwingine maana Mbowe muda wake uliisha akabadili katiba kujiongezea muda
2. Uteuzi wa mgombea urais uwe huru na wa kidemokrasia, watu wahamasishwe kuchukua form za urais ili mgombea achguliwe kutoka katika orodha ya wagombea kadhaa, na siyo kumwekea Lowasa siti ya upendeleo
3. Waache kutetea watu waofukuzwa kwa ubadhilifu na warudi kwenye sera ya kupinga ufisadi
4. Wajikite katika kufanya siasa za ukweli na siyo za utapeli
Hapa Ndipo ninapo Mvulia Kofia Ndugu Lowassa. Huyu ni Bonge la Kiongozi, kwa Mipango yake na Mikakati yenye Dira hakika Chaadema Kitafanya Kazi Nzuri sana.
Wajipange Vizuri katika Almashauri walizozipata, wawatumikie wananchi kwa ufanisi Mzuri na Maendeleo yaonekane yasiwe Midomoni, wapange kamati moja ya Kutoa Mrejesho kwa Wananchi kwa kazi walizozifanya na Mafanikio yaliyo waletea wananchi husika katika miji na Majiji wanayo yaongoza.
Chama kishuke sasa kwa wananchi, kiwe karibu na Wananchi kwa kuonyesha Dira kama Chama kinachotafuta kuongoza Dola.
Tabia ya kudandia mafanikio ya watu ni ya huyo mzee EL, anaipenda sana. Wakati bado yupo serikalini lakini akiwa ameshajiuzulu uwaziri mkuu alidai kwamba yeye ni mmoja wa watu waliowezesha kupatikana tena kwa sehemu ya ziwa Nyasa ambayo ilikuwa inatambulika kama mali ya Malawi. Kazi nzito za kisheria walifanya wanasheria wengine lakini aalipoona mambo yameanza kukaa vizuri ndio akataka kujitangazia umaarufu usiomhusu. Huyo katibu mkuu mpya anaweza kuwa mbunifu na mtendaji lakini awe mwangalifu sana kwani CHADEMA wanayo sifa ya kuwa na michezo ya kupenda kuzungukana. Maadui wa huyo katibu mkuu hawako mbali nae, ni viongozi wa juu wa chama, iwapo ataanza kuwafunika kiutendaji.Lowasa anaingiaje hapo? Hii ni mipango ya Katibu Mkuu CHADEMA, Dr Mashinji. Na hizi kauli ndo zitakuwa zinamvunja moyo, mipango apange yeye sifa apewe mwingine.
Mimi siyo CCM, ila napenda upinzani unaoaminika, wenye nguvu, nia na dhamira ya kweli ya kuwakomboa watanzania. Lowasa haninyimi usingizi, maana najua yeye na genge lake la mafisadi (walio CCM na kwingineko) hawawezi tena kupata madaraka ya kufisadi rasilimali zetu.HAYO NI MAMBO YA CHADEMA WEWE WA CCM YANAKUHUSU NINI.
PILIPILI IPO SHAMBANI WEWE YAKUWASHIA NINI??????
NAONA LOWASA BADO KUMBE ANAWANYIMA USINGIZI MNAZIDI KUMUOTA TU.