CHADEMA Yaanza Kumeguka Kimkakati Mbezi Luis

CHADEMA Yaanza Kumeguka Kimkakati Mbezi Luis

1954tanu

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
1,038
Reaction score
487
Hali ya CHADEMA yaanza kuteteleka kata ya Mbezi baada ya mapandikizi ya CCM na ACT ndani ya CDM kuanza kubungua taratibu. Mamluki hao wakiongozwa na Makweta kufurukuta hadi kupata uenyekiti chama wa mtaa Makabe.

Nafasi ya mwenyekiti ameipata baada ya kuendesha na kupiga majungu yaliyomlazimisha mwenyekiti aliyekuwepo kujiuzulu ndugu Munuo.

Makweta na kundi lake wamefanikiwa kuuweka mfukoni uongozi wa chadema Kata ya Mbezi Luis na Jimbo la Ubungo. Uongozi wote wa Chadema Jimbo na kata kwa sasa wanacheza ngoma inayopigwa na Makweta.

Kwa sasa, katiba imekuwa ikivunjwa wazi wazi ili mradi Makweta na mamluki wenzake wafanikishe malengo yao. Lengo mojawapo,ni kuhakikisha wanapandikiza watu wao kwenye ngazi za juu za chama katka kata ya Mbezi Luis. Hadi sasa wamelazimisha uchaguzi ndani ya chama urudiwe kwa kujaza nafasi zote. Wamelazimisha kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi za wazi ngazi ya tawi na kuwaondoa hata viongozi waliopo na waliochaguliwa mwaka jana.

Jambo lisiloeleweka ni pale ambapo viongozi wa kata na jimbo wanaendesha chaguzi zilizoamriwa na Makweta; huku wakijua dhahiri kwamba baadhi ya nafasi zinazoitiwa uchaguzi zina viongozi wanaozishikilia tangu uchaguzi uliopita.
 
Hali ya CHADEMA yaanza kuteteleka kata ya Mbezi baada ya mapandikizi ya CCM na ACT ndani ya CDM kuanza kubungua taratibu. Mamluki hao wakiongozwa na Makweta (aliyejiunga na CDM akitokea CCM) kufurukuta hadi kupata uenyekiti chama wa mtaa Makabe.

Nafasi ya mwenyekiti ameipata baada ya kuendesha na kupiga majungu yaliyomlazimisha mwenyekiti aliyekuwepo kujiuzulu.

Makweta na kundi lake wamefanikiwa kuuweka mfukoni uongozi wa chadema Kata ya Mbezi Luis na Jimbo la Ubungo. Uongozi wote wa Chadema Jimbo na kata kwa sasa wanacheza ngoma inayopigwa na Makweta.

Kwa sasa, katiba imekuwa ikivunjwa wazi wazi ili mradi Makweta na mamluki wenzake wafanikishe malengo yao. Lengo mojawapo,ni kuhakikisha wanapandikiza watu wao kwenye ngazi za juu za chama katka kata ya Mbezi Luis. Hadi sasa wamelazimisha uchaguzi ndani ya chama urudiwe kwa kujaza nafasi zote. Wamelazimisha kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi za wazi na kuwaondoa hata viongozi waliopo na waliochaguliwa mwaka jana.

Jambo lisiloeleweka ni pale ambapo viongozi wa kata na jimbo wanaendesha chaguzi zilizoamriwa na Makweta; huku wakijua dhahiri kwamba baadhi ya nafasi zinazoitiwa uchaguzi zina viongozi wanaozishikilia tangu uchaguzi wa mwaka jana.

Lengo la kupandikiza mamluki likikamilika, mkakati ufuatao ni kumng'oa mwenyekiti wa serikali ya mtaa (kwa tiketi ya Chadema) mtaa wa Makabe. Mkakati huu ni kuhakikisha uchaguzi uchaguzi serikali ya mtaa unarudiwa ili CCM waushike mtaa tena.

Makweta na kundi lake,wamepanga kufanya mafarakano na mtifuano ndani ya chadema kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015 ili kuweka mazingira mazuri kwa mgombea udiwani kwa tiketi ya CCM kupita.. Kwa sasa kata ya Mbezi ina diwani kupitia CHADEMA mh.Kagale. Hilo ndilo lengo mahususi la Makweta na mamluki wenzake ndani ya CDM.

Makweta amekaa kimkakati ili kuweza kupata donge nono la fedha na cheo kikubwa ndani ya chama cha CCM.
Mi nadhani kama mwanaume ea ukweli huwezi lalamika kiasi hiki. Pambana . Achana na mambo ya kulialia kama mtoto mdogo
 
Hamna vikao halali vya kuyasemea haya?
 
Viongozi CDM mwogopeni sana huyo jamaa makweta namjua vzr sana huyo ataharibu chama huyo ni ccm.
 
CHADEMA ni taasisi imara sana kuliko zote nchini. Taarfa zako zitafanyiwa kazi na mwishowe haki itatendeka. Usiwe na wasi kijana ukweli utajulikana tu kama huyo mwenyekiti anamatatizo au nyinyi mnampiga majungu kwa maslahi yenu tu.
 
Makweta ameandaa watu wa kugombea na kushika nafasi zote za tawi. Nafasi zilizo wazi na zile zilizozibwa kwa uchaguzi wa kikatiba.
 
pasipo zzk chadema hoi,ajabu!

wajinga wote waseme ndio unasikia ccm ndioooooo haya walio sema ndio wameshinda katibu endelea hahahahaha kweli ibililo we ni tikiti maji mpaka leo unamuwaza zito muulize mwl.kaijage yupoo kimya sasa ambaye ni vuvuzela la zito
 
pasipo zzk chadema hoi,ajabu!
wakati wa Limbu ACT ilikuwa inavuma sana wakati wote lakini baada ya Zitto kupora madaraka ACT ilivuma kwa siku kumi tu na sasa imekufa! Kama Zitto ameshindwa kuongoza ACT na kupelekea chama hicho kufa ana madhara gani kufukuzwa CHADEMA?
 
wakati wa Limbu ACT ilikuwa inavuma sana wakati wote lakini baada ya Zitto kupora madaraka ACT ilivuma kwa siku kumi tu na sasa imekufa! Kama Zitto ameshindwa kuongoza ACT na kupelekea chama hicho kufa ana madhara gani kufukuzwa CHADEMA?

Nyi chadema mbona hatuwaelewi act ni ya limbu hapohapo mnasema zzk alianzisha chama akiwa ndani ya chadema sasa tushike lipi?
 
Back
Top Bottom