CHADEMA wawaomba wana ukoo wa Mwl. Nyerere wasiwapokee ACT-Wazalendo

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,982
VIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo na Chama cha Demokrasia na Mendeleo (CHADEMA), nusura wakutane uso kwa uso nyumbani kwa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, walipokwenda kuzuru kaburi lake kwenye Kijiji cha Mwitongo, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara.

Msafara wa Naibu Katibu Mkuu CHADEMA Bara, Bw. John Mnyika, ndio ulioanza kuwasili kujijini hapo na baada ya kuzuru kaburi, waliondoka na baada ya muda mfupi ukawasili msafara wa ACT ukiongozwa na Kiongozi wa chama hicho, Bw. Zitto Kabwe.

Msafara wa ACT, ulifika kijijini hapo baada ya chama hicho kumaliza ziara ya kukitangaza, kukitambulisha chama na viongozi wake kwenye mikoa mbalimbali nchini.

Akizungumza mara baada ya kuwapokea viongozi wa ACT-Wazalendo, Mzee wa Ukoo wa Burito ambaye pia Mwenyekiti wa Wazee wa Butiama, Jack Nyamwaga, aliwaambia muda mfupi uliopita walikuwepo viongozi wa CHADEMA.

"Baada ya viongozi hao kufika hapa Mwitongo, walisema kuna viongozi wanakuja lakini tusiwape ushirikiano wakidai kama ni suala la kupinga ufisadi, CHADEMA wamelipigia kelele ili kumuenzi Mwalimu Nyerere.

"Kimsingi kila mtu anaruhusiwa kufika hapa Mwitongo katika kaburi la Mwalimu na sisi kama wanafamilia, tunampokea kila mtu lakini si kazi yetu kusema nani aje, nani asije," alisema.

Aliongeza kuwa, viongozi wengi wamekuwa wakimuenzi Mwalimu Nyerere kwa maneno si kwa vitendo...ACT mmeanza vizuri na mtamaliza vizuri, nawatakia kila la heri kama kweli mtamuenzi Mwalimu kwa vitendo," alisema Mzee Nyamwaga.

Kwa upande wake, Bw. Kabwe alisema wao watamuenzi Mwalimu kwa vitendo ndio maana wameweka msingi huo katika sera ya chama chao.

Alisema lengo la kumalizia ziara hiyo kwenye kaburi la Mwalimu Nyerere ni kutokana na kuuenzi mchango wake kwa Taifa na Watanzania ndio maana walianzia ziara yao mkoani Ruvuma ambapo ilikuwa ni kitovu cha vita ya maji maji.

"Tumefika hapa na viongozi wenzangu wa ACT kwa sababu ya kutambua mchango wa Mwalimu kwa Taifa...chama chetu kitayaenzi mambo yote ambayo Mwalimu alikuwa akiyataka na kuyapigania kwa vitendo na Katiba yetu inatamka hivyo," alisema Bw. Kabwe.

Chanzo:Gazeti la Majira.

===============================================
DSC_0466.JPG

DSC_0467.JPG

Andrew Nyerere ambaye Mtoto wa Hayati baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, akibadilishana kofia na kuteta jambo na Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe.
Andrew Nyerere alimpa Kofia ya CCM na Zitto Kabwe akampa kofia ya Chama cha ACT-Wazalendo na kuvaa wakati viongozi wa chama hicho walipofanya ziara kijijini Mwitongo Wilayani Butiama
11059486_922848151069216_4826621727278919500_n.jpg

Ujumbe wa ACT-Wazalendo wakiangalia Mawaziri wa Baraza la Mawaziri la mwisho la Mwalimu Nyerere. walipotembelea Makumbusho ya Baba wa Taifa Butiama jana
21720_922848427735855_8022850565462869756_n.jpg

Zitto Kabwe akimuonyesha Afande Sele picha ya Deng Xiaoping ambaye ni ‘baba wa mabadiliko ya kiuchumi ya China'. Hii ni baada ya kumjadili wakati wakiwa kwenye ziara kabla ya kufika Butiama.
 
Mdini na mkabila mkuu anaweza kumuenzi mwl Nyerere, hebu acheni utani na mizaha.

Nyerere angekuwa na mawazo kama yake ya mkoa flani unachangia kiasi kadhaa katika taifa, leo musoma ingekua hivi ilivyo kweli?
 
VIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo na Chama cha Demokrasia na Mendeleo (CHADEMA), nusura wakutane uso kwa uso nyumbani kwa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, walipokwenda kuzuru kaburi lake kwenye Kijiji cha Mwitongo, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara.

Msafara wa Naibu Katibu Mkuu CHADEMA Bara, Bw. John Mnyika, ndio ulioanza kuwasili kujijini hapo na baada ya kuzuru kaburi, waliondoka na baada ya muda mfupi ukawasili msafara wa ACT ukiongozwa na Kiongozi wa chama hicho, Bw. Zitto Kabwe.

Msafara wa ACT, ulifika kijijini hapo baada ya chama hichokumaliza ziara ya kukitangaza, kukitambulisha chama na viongozi wake kwenye mikoa mbalimbali nchini.

Akizungumza mara baada ya kuwapokea viongozi wa ACT-Wazalendo, Mzee wa Ukoo wa Burito ambaye pia Mwenyekiti wa Wazee wa Butiama, Jack Nyamwaga, aliwaambia muda mfupi uliopita walikuwepo viongozi wa CHADEMA.

"Baada ya viongozi hao kufika hapa Mwitongo, walisema kuna viongozi wanakuja lakini tusiwape ushirikiano wakidai kama ni suala la kupinga ufisadi, CHADEMA wamelipigia kelele ili kumuenzi Mwalimu Nyerere.

"Kimsingi kila mtu anaruhusiwa kufika hapa Mwitongo katika kaburi la Mwalimu na sisi kama wanafamilia, tunampokea kila mtu lakini si kazi yetu kusema nani aje, nani asije," alisema.

Aliongeza kuwa, viongozi wengi wamekuwa wakimuenzi Mwalimu Nyerere kwa maneno si kwa vitendo...ACT mmeanza vizuri na mtamaliza vizuri, nawatakia kila la heri kama kweli mtamuenzi Mwalimu kwa vitendo," alisema Mzee Nyamwaga.

Kwa upande wake, Bw. Kabwe alisema wao watamuenzi Mwalimu kwa vitendo ndio maana wameweka msingi huo katika sera ya chama chao.

Alisema lengo la kumalizia ziara hiyo kwenye kaburi la Mwalimu Nyerere ni kutokana na kuuenzi mchango wake kwa Taifa na Watanzania ndio maana walianzia ziara yao mkoani Ruvuma ambapo ilikuwa ni kitovu cha vita ya maji maji.

"Tumefika hapa na viongozi wenzangu wa ACT kwa sababu ya kutambua mchango wa Mwalimu kwa Taifa...chama chetu kitayaenzi mambo yote ambayo Mwalimu alikuwa akiyataka na kuyapigania kwa vitendo na Katiba yetu inatamka hivyo," alisema Bw. Kabwe.

Chanzo:Gazeti la Majira.

===============================================
DSC_0466.JPG

DSC_0467.JPG

Andrew Nyerere ambaye Mtoto wa Hayati baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, akibadilishana kofia na kuteta jambo na Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe.
Andrew Nyerere alimpa Kofia ya CCM na Zitto Kabwe akampa kofia ya Chama cha ACT-Wazalendo na kuvaa wakati viongozi wa chama hicho walipofanya ziara kijijini Mwitongo Wilayani Butiama
11059486_922848151069216_4826621727278919500_n.jpg

Ujumbe wa ACT-Wazalendo wakiangalia Mawaziri wa Baraza la Mawaziri la mwisho la Mwalimu Nyerere. walipotembelea Makumbusho ya Baba wa Taifa Butiama jana
21720_922848427735855_8022850565462869756_n.jpg

Zitto Kabwe akimuonyesha Afande Sele picha ya Deng Xiaoping ambaye ni ‘baba wa mabadiliko ya kiuchumi ya China'. Hii ni baada ya kumjadili wakati wakiwa kwenye ziara kabla ya kufika Butiama.​
Kama Mnyika kaongea maneno hayo kuwa eti "kuna wageni watakuja msiwapokee" ni kukosa akili kabisa kwa Mnyika
Na kwa kifupi ni kuchanganyikiwa.

Huwezi kumchagulia mtu rafiki na mbaya zaidi mtanzania anadiriki kumwambia mtanzania mwenzake kuwa usimpokee yulee, ambaye naye ni mtanzania.
Ningesema ni tabia ya kis.shenzi na kukosa ustaarabu lakini inabidi nijizuie.
Sasa baada ya kukabwa koo na upinzani ndani ya chama chao ndo tunaona the true colors of CHADEMA, ukabilia, ubaguzi na umimi.
Heko familia ya Mwalimu kwa kutoendekeza upuuzi huo.
 
Kama Mnyika kaongea maneno hayo kuwa eti "kuna wageni watakuja msiwapokee" ni kukosa akili kabisa kwa Mnyika
Na kwa kifupi ni kuchanganyikiwa.

Huwezi kumchagulia mtu rafiki na mbaya zaidi mtanzania anadiriki kumwambia mtanzania mwenzake kuwa usimpokee yulee, ambaye naye ni mtanzania.
Ningesema ni tabia ya kis.shenzi na kukosa ustaarabu lakini inabidi nijizuie.
Sasa baada ya kukabwa koo na uzinzani ndani ya chama chao ndo tunaona the true colors of CHADEMA, ukabilia, ubaguzi na umimi.
Heko familia ya Mwalimu kwa kutoendekeza upuuzi huo.
Ukisoma kauli ya Vincent Nyerere ni dhahiri gazeti la Majira limepotosha. Kwanza msemaji wa familia ya Nyerere si Jack Nyamwaga. Ni Chifu Wanzagi.
 
VIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo na Chama cha Demokrasia na Mendeleo (CHADEMA), nusura wakutane uso kwa uso nyumbani kwa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, walipokwenda kuzuru kaburi lake kwenye Kijiji cha Mwitongo, Wilaya ya Butiama, mkoani Mara.

Msafara wa Naibu Katibu Mkuu CHADEMA Bara, Bw. John Mnyika, ndio ulioanza kuwasili kujijini hapo na baada ya kuzuru kaburi, waliondoka na baada ya muda mfupi ukawasili msafara wa ACT ukiongozwa na Kiongozi wa chama hicho, Bw. Zitto Kabwe.

Msafara wa ACT, ulifika kijijini hapo baada ya chama hichokumaliza ziara ya kukitangaza, kukitambulisha chama na viongozi wake kwenye mikoa mbalimbali nchini.

Akizungumza mara baada ya kuwapokea viongozi wa ACT-Wazalendo, Mzee wa Ukoo wa Burito ambaye pia Mwenyekiti wa Wazee wa Butiama, Jack Nyamwaga, aliwaambia muda mfupi uliopita walikuwepo viongozi wa CHADEMA.

"Baada ya viongozi hao kufika hapa Mwitongo, walisema kuna viongozi wanakuja lakini tusiwape ushirikiano wakidai kama ni suala la kupinga ufisadi, CHADEMA wamelipigia kelele ili kumuenzi Mwalimu Nyerere.

"Kimsingi kila mtu anaruhusiwa kufika hapa Mwitongo katika kaburi la Mwalimu na sisi kama wanafamilia, tunampokea kila mtu lakini si kazi yetu kusema nani aje, nani asije," alisema.

Aliongeza kuwa, viongozi wengi wamekuwa wakimuenzi Mwalimu Nyerere kwa maneno si kwa vitendo...ACT mmeanza vizuri na mtamaliza vizuri, nawatakia kila la heri kama kweli mtamuenzi Mwalimu kwa vitendo," alisema Mzee Nyamwaga.

Kwa upande wake, Bw. Kabwe alisema wao watamuenzi Mwalimu kwa vitendo ndio maana wameweka msingi huo katika sera ya chama chao.

Alisema lengo la kumalizia ziara hiyo kwenye kaburi la Mwalimu Nyerere ni kutokana na kuuenzi mchango wake kwa Taifa na Watanzania ndio maana walianzia ziara yao mkoani Ruvuma ambapo ilikuwa ni kitovu cha vita ya maji maji.

"Tumefika hapa na viongozi wenzangu wa ACT kwa sababu ya kutambua mchango wa Mwalimu kwa Taifa...chama chetu kitayaenzi mambo yote ambayo Mwalimu alikuwa akiyataka na kuyapigania kwa vitendo na Katiba yetu inatamka hivyo," alisema Bw. Kabwe.

Chanzo:Gazeti la Majira.

===============================================
DSC_0466.JPG

DSC_0467.JPG

Andrew Nyerere ambaye Mtoto wa Hayati baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, akibadilishana kofia na kuteta jambo na Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe.
Andrew Nyerere alimpa Kofia ya CCM na Zitto Kabwe akampa kofia ya Chama cha ACT-Wazalendo na kuvaa wakati viongozi wa chama hicho walipofanya ziara kijijini Mwitongo Wilayani Butiama
11059486_922848151069216_4826621727278919500_n.jpg

Ujumbe wa ACT-Wazalendo wakiangalia Mawaziri wa Baraza la Mawaziri la mwisho la Mwalimu Nyerere. walipotembelea Makumbusho ya Baba wa Taifa Butiama jana
21720_922848427735855_8022850565462869756_n.jpg

Zitto Kabwe akimuonyesha Afande Sele picha ya Deng Xiaoping ambaye ni ‘baba wa mabadiliko ya kiuchumi ya China'. Hii ni baada ya kumjadili wakati wakiwa kwenye ziara kabla ya kufika Butiama.​
Huu ndio unafiki tunao usema. ZZK hawezi fika popote.
 
Ama hakika Zitto wewe ni kichwa you know where to strike suprise zako zitawachanganya wadau kwa muda mrefu sana.
 
Kama Mnyika kaongea maneno hayo kuwa eti "kuna wageni watakuja msiwapokee" ni kukosa akili kabisa kwa MnyikaNa kwa kifupi ni kuchanganyikiwa.Huwezi kumchagulia mtu rafiki na mbaya zaidi mtanzania anadiriki kumwambia mtanzania mwenzake kuwa usimpokee yulee, ambaye naye ni mtanzania.Ningesema ni tabia ya kis.shenzi na kukosa ustaarabu lakini inabidi nijizuie.Sasa baada ya kukabwa koo na upinzani ndani ya chama chao ndo tunaona the true colors of CHADEMA, ukabilia, ubaguzi na umimi.Heko familia ya Mwalimu kwa kutoendekeza upuuzi huo.
Mkuu, tupo kwenye ulimwengu wa siasa za kijinga sana kuwahi kutokea duniani. Gazeti la Majira ambalo ni moja ya magazeti ya propaganda ya ACT yamemnukuu vipi mtu ambaye sio msemaji wa familia? Na kama ACT wanajinasibu kumuenzi Mzee Nyerere kwanini huyo kila saa wamtumie kwa kuibabatizia Chadema mambo ya kipumbavu? Juliana Shonza aliyefukuzwa Chadema kama mbwa alipandisha uzi hapa kuhusu Chadema na Familia ya Nyererr, Andrew Nyerere akakanusha hapa, Juliana akapewa alichostahili. Sote tunajua Juliana na Nuru ya Chama ni 'marafiki'.Gazeti la Majira kama yalivyo Raia Tanzania na Mtanzania linalohaririwa na Denis Msaki na lenyewe linatumika kumbeba Zitto limeamua kuanzisha uzushi, ufitini, uzabizabina ambao umevuka mipaka.Kwa uwezo, busara, malezi aliyopewa na Chama, na kwa jinsi ACT isivyo threat kwa Chadema, John Mnyika hana na hatakuwa na sababu ya kuongea hayo 'aliyonukuliwa'. Mnyika is more smart than that. Level ya Mnyika imeipita kwa mbaaaaali sana level ya kina Mchange na mwal. Kaijage
 
Last edited by a moderator:
Siasa buana ..Kuna wakati fikra za Mwalimu hubezwa na kuitwa zimepitwa na wakati,, lakini cha ajabu kuna mambo mpaka sasa hayaendi bila hizo fikra zake.. Zidumu fikra za Hayati Baba wa Taifa.
 
Siasa buana ..Kuna wakati fikra za Mwalimu hubezwa na kuitwa zimepitwa na wakati,, lakini cha ajabu kuna mambo mpaka sasa hayaendi bila hizo fikra zake.. Zidumu fikra za Hayati Baba wa Taifa.

Walewale waliomtukana bungeni sasahivi wanapigana vikumbo kwa Nyerere!! Na kutaka wenzao wasipokelewe!!!
 
Kwa mwendo huu wa baadhi watz kuendelea shabikia watu wengine uku wanatambua kuwa maneno yao ni ufitini na uchonganishi ni dhairi kwamba watanzania bado hatuna uzarendo na hatujawa tayari kujitawala na kuiona nchi yetu ikisonga mbele kama baadhi ya mataifa tuliyokuwa nayo at the same level of development be4 1970 na kwa sasa wako mbali kuliko sisi na huko ndo viongoz wetu wanatembeza bakuri kuomba misahada.
Tunakalia Majungu matupu na hatuzungumzii ukosefu wa huduma bora za elimu,barabara,afya na chakula,tunabaki shabikia msaliti mkubwa wa maendeleo yetu zzK as Yudah eskalioti na ujinga na wajinga wenzake.Kwa tamaa ya madaraka ya kijana huyo tegemeeni ya xenophibia kati ya CHADEMA V/s ACT badala ya upinzani na Ccm.
 
Mbona steve nyerere hayupo?au sio mtoto wa mwalimu

Hakufuatwa mtu au watu pale, atakae kutwa huyohuyo, kubwa nikile kilicho fanya watu na chama kuwapo pale, mtu amemfuata mzazi wako nyumbani lazima akukute na wewe akiwa hana shida nawe, teve nyerere?
 
Hivi huko kwenye kaburi la Nyerere wanaenda kutambika ama?

Binafsi naona haina maana kutembelea kaburi la mtu ambaye hata kazi hujaweza kuzienzi na wala huna mpango huo...

Ni kama kaunafiki fulani hivi...

By the way hivi Invisible ile kampeni yako ya kuchunguza habari za kweli na uongo bado inaendelea?
 
Last edited by a moderator:
Mdini na mkabila mkuu anaweza kumuenzi mwl Nyerere, hebu acheni utani na mizaha.

Nyerere angekuwa na mawazo kama yake ya mkoa flani unachangia kiasi kadhaa katika taifa, leo musoma ingekua hivi ilivyo kweli?
Hoja yako ni nini?

Hutaki kusikia ukweli habari ya mchango wa kila mkoa katika kapu la taifa?

Unataka kusikia unafiki katika mantiki ya kuficha ukweli?
 
Back
Top Bottom