CHADEMA waelezeni wananchi mema yenu na siyo kuwa mabingwa wa kukosoa tu

Ritz

JF-Expert Member
Jan 1, 2011
47,375
33,023
Wanabodi.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kunadi tuhuma badala ya kuwaeleza wananchi juu ya sera zao. CHADEMA inapaswa kuwaeleza watanzania itawafanyia nini wakipata fursa ya kushika dola.

Linalowasikitisha watu makini CHADEMA haiwaelezi wananchi chochote juu ya mema yao au zuri lolote walilonalo wakiwa kama chama cha upinzani. Kinyume chake CHADEMA wameanza kunadi tuhuma wakati Watanzania hawahitaji kujulishwa tuhuma.

Bahati nzuri hizo tuhuma zimewarudia wenyewe wameanza kulipuana wao kwa wao na kutuhumiana wenyewe kwa wenyewe, tayari Arusha, Karatu, Mwanza, Mbeya, Tanga, wameishatimuana. CHADEMA hawakutambua kwamba kwenye uchaguzi kilichokuwa kimewanyima kura ni kutowaeleza Watanzania juu ya mema yao kwamba watawafanyia mambo gani mazuri Tanzania yetu endapo watafanikiwa kuchukua dola.

CHADEMA hawakujua ajenda yao ya ufisadi na mafisadi imepokelewa vipi na wapigakura. Wakaamua kuendeleza vijembe vya uchaguzi huku wakiugeuza upinzani uwe sawa na ukaidi, ubishi, na kusigana ama kubishana na dola.

Kimsingi vyama vya siasa vinashindana na kuzidiana kwa sera na siyo kuzidiana tuhuma.
 
CHADEMA inafuata nyao za NCCR Mageuzi, hali inajionyesha huko tuendako utaibuka mgogoro mkubwa wa kusambaratisha chama hicho.
 
Wakuu huyu jamaa na Nape kazi yao ni moja tu nayo ni kuzua mijadala isiyo na tija ili watu waache kujadili hoja za msingi.

Kama vipi tuwapotezee tu.
 
Wanabodi.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeendelea kunadi tuhuma badala ya kuwaeleza wananchi juu ya sera zao. Chadema inapaswa kuwaeleza watanzania itawafanyia nini wakipata fursa ya kushika dola.

Linalowasikitisha watu makini Chadema haiwaelezi wananchi chochote juu ya mema yao au zuri lolote walilonalo wakiwa kama chama cha upinzani. Kinyume chake Chadema wameanza kunadi tuhuma wakati watanzania hawahitaji kujulishwa tuhuma.

Bahati nzuri hizo tuhuma zimewarudia wenyewe wameanza kulipuana wao kwa wao na kutuhumiana wenyewe kwa wenyewe, tayari Arusha, Karatu, Mwanza, Mbeya, Tanga, wameishatimuana. Chadema hawakutambua kwamba kwenye uchaguzi kilichokuwa kimewanyima kura ni kutowaeleza watanzania juu ya mema yao kwamba watawafanyia mambo gani mazuri Tanzania yetu endapo watafanikiwa kuchukua dola.

Chadema hawakujua ajenda yao ya ufisadi na mafisadi imepokelewa vipi na wapigakura. Wakaamua kuendeleza vijembe vya uchaguzi huku wakiugeuza upinzani uwe sawa na ukaidi, ubishi, na kusigana ama kubishana na dola.

Kimsingi vyama vya siasa vinashindana na kuzidiana kwa sera na siyo kuzidiana tuhuma.

Heshima kwako mkuu

1. Hakina haja ya kuwaeleza mema kwani wananchi si mataahira wasioweza kujua mema na mabaya ya Chadema.

2. Inatoa elimu ya uraia inayoonyesha mapungufu ya chama tawala na njia ya kuyakabili pamoja na vyama vingine tofauti na Chadema.

3. Nilidhani kukosolewa ni afya kwa demokrasia. Nichukue fursa hii kukipongeza chama dola kuzichukulia serious baadhi ya maeneo yanayokosolewa kama elimu, bidhaa za ujenzi na matumizi mabaya dola.


Hata Chadema itakaposhika madaraka 2015 kitakosolewa na wanachama wake bila chenga kikienda kinyume na matarajio ya Watanzania pamoja na magamba.
 
shida ya CHADEMA ni kwamba hata maandamano yao lazima watu waumie ni kwa nini? tujiulize wadanganyika ni kweli CHADEMA itakufa kama ilivyokufa NCCR hizo ni nguvu za soda tu tuone mwisho
 
CHADEMA inafuata nyao za NCCR Mageuzi, hali inajionyesha huko tuendako utaibuka mgogoro mkubwa wa kusambaratisha chama hicho.
Kama mnategemea CHADEMA kife hapo mna kazi maana ndiyo kwanza kinaendelea kuchanua.

Ombea adui yako aishi maisha marefu aone mafanikio yako au na wewe umekata tamaa ya kuwa hutaona mafanikio chanya ya CCM hata iweje ndyo mnasubiria CHADEMA kife kisione aibu yenu?
 
Wanabodi.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeendelea kunadi tuhuma
badala ya kuwaeleza wananchi juu ya sera zao. Chadema inapaswa kuwaeleza
watanzania itawafanyia nini wakipata fursa ya kushika dola.

Linalowasikitisha watu makini Chadema haiwaelezi wananchi chochote juu
ya mema yao au zuri lolote walilonalo wakiwa kama chama cha upinzani.
Kinyume chake Chadema wameanza kunadi tuhuma wakati watanzania
hawahitaji kujulishwa tuhuma.

Bahati nzuri hizo tuhuma zimewarudia wenyewe wameanza kulipuana wao kwa
wao na kutuhumiana wenyewe kwa wenyewe, tayari Arusha, Karatu, Mwanza,
Mbeya, Tanga, wameishatimuana. Chadema hawakutambua kwamba kwenye
uchaguzi kilichokuwa kimewanyima kura ni kutowaeleza watanzania juu ya
mema yao kwamba watawafanyia mambo gani mazuri Tanzania yetu endapo
watafanikiwa kuchukua dola.

Chadema hawakujua ajenda yao ya ufisadi na mafisadi imepokelewa vipi na
wapigakura. Wakaamua kuendeleza vijembe vya uchaguzi huku wakiugeuza
upinzani uwe sawa na ukaidi, ubishi, na kusigana ama kubishana na dola.

Kimsingi vyama vya siasa vinashindana na kuzidiana kwa sera na siyo
kuzidiana tuhuma.

Ni bora mtu akutukane kwa kukuambia "una akili za kitoto", kuliko kukwambia "una akili kama wanachama wa ccm"...
 
shida ya chadema ni kwamba hata maandamano yao lazima watu waumie ni kwa nini? tujiulize wadanganyika ni kweli chadema itakufa kama ilivyokufa NCCR hizo ni nguvu za soda tu tuone mwisho
haaah! Inamaana hukumwelewa jk kwenye hotuba yake pale kizota, au we ni mgeni hapa tz
 
Ritz,

Kuna jambo gani jema zaidi ya mtu kukuambia mwizi wako ni nani, na anaiba nini? Just think about it!
 
Kama mnategemea chadema kife hapo mna kazi maana ndiyo kwanza kinaendelea kuchanua. Omba adui yako aishi maisha marefu aone mafanikio yako au na wewe umekata tamaa ya kuwa hutaona mafanikio chanya ya ccm hata iweje ndyo mnasubiria chadema kife kisione aibu yenu?

Mgogoro mwingine tunasubiri kule Tarime kati ya Mwita Waitara na John Heche.

Waitara anasema kutokana na kura alizopata mwaka 2010 tayari anao mtaji wake wa kisiasa na Heche naye kwa kubebwa na Makao Makuu anataka naye kugombea ubunge Tarime.
 
Naona umeibuka na ya kufungia mwaka mkuu Ritz.Najua kipindi hiki cha sikukuu kinahitaji pesa nyingi kidogo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom