CHADEMA: Turudishie Hadhi ya Chama Chetu

Ufipa-Kinondoni

JF-Expert Member
Jan 3, 2012
4,582
2,783
Ni lazima tuseme na hakuna wa kutunyamazisha.
[Na ahidi tarehe ya kuja kwa Lowassa CHADEMA kuleta andiko la Malengo makuu ya SUMAYE na LOWASSA].


Ni kama chama kimekosa mwelekeo, kinawayawaya. Kinaendeshwa na kila anayejisikia. Hakuna mipango, hakuna msimamizi wa mipango na hakuna vikao vya kimaamuzi. Ni wakati wa kusema tunahitaji chama kirudi kwenye msingi yake. Msemaji wa chama yupo?

Nimeona sahizi tumegraduate na kuwa chama cha siasa. Wawakilishi wetu wameambiwa, waanze kufanya kazi na waache siasa na kuzuia kazi za serikali. Hili nakubaliana nalo. Ila naona linapingana na kauli ya Mbowe ya Madiwani kutoshirikiana na serikali. Na ndo ile imetokea kwa Meya wa Kinondoni akitekeleza agizo la chama. Leo ataficha wapi uso wake baada ya kupata agizo jipya??? .

Sijajua viongozi wa ngazi za chini za chama na mabaraza yake yanafanyia kazi kauli za nani.
Mbowe anasema, Lowassa anasema!!!!!

Nani kiongozi wetu hapa Ufipa? Nani msemaji wetu hapo? Matamko na maelekezo ya kuendesha chama yanatoka kwa nani? Hakika miluzi mingi humpoteza mbwa. Ndo kinachotokea. Tunahitaji msimamo wa chama kabla muda haujaisha wa kuponya vidonda vikubwa zaidi.

Mwenyekiti upo? Katibu upo? Au ndo kauli na ubashiri wa Lowassa kuchukua chama umetimia?

Kwa leo nitaishia hapa.
 
Bora muongee wenyewe from within labda mtaelewana. Sisi wengine tunaposhauri from a neutral angle bila kuwa na any conflict of interest tunaishia kushambuliwa na wanaojiita wafia chama. Kitu wanachosahau ni kwamba sio kila mwenye wazo tofauti anakuwa adui wa chama.

Party members na viongozi lazima wajifunze kukubali constructive criticism.

Kwa kifupi na bila kuficha ukweli ni kwamba Chadema kimepoteza muelekeo kwasasa. Chadema ya siku za nyuma tuliyoiona ni mkombozi wa wanyonge na mbadala sahihi wa CCM haipo tena.

But there is still room and potentials za kujitathmini, kuji-strategize na kubadilika objectively ili kuendana na mahitaji ya wakati huu. Concrete revisited plans with solid way forward and ultimate party transformation is inevitable!! Business as usual inaua chama!!
 
jaman hivi hiyo chadema mmelazimishwa? si huwa mnadai eti mnaakili mno ,endeleeni tu mie sio tofauti ya cdm na ccm, labda tu ni kwakua ccm ipo madarakani tu. Yale yanayofanywa ccm na cdm vile,
m/kt bila kupingwa
makundi
Hofu ya kumhoji mwenyekiti
Hamueleweki kisera na kiitikadi
Rushwa katika michakato ya uchaguzi
vyeo vya urafiki na kufamiana
Elimu kutopewa kipaumbele etc
Twende siku moja tutafika.
 
Hakuna anayelazimishwa ila kila haki za wanachama ziheshimiwe. Maana bila wanachama ina maana hakuna chama.
jaman hivi hiyo chadema mmelazimishwa? si huwa mnadai eti mnaakili mno ,endeleeni tu mie sio tofauti ya cdm na ccm, labda tu ni kwakua ccm ipo madarakani tu. Yale yanayofanywa ccm na cdm vile,
m/kt bila kupingwa
makundi
Hofu ya kumhoji mwenyekiti
Hamueleweki kisera na kiitikadi
Rushwa katika michakato ya uchaguzi
vyeo vya urafiki na kufamiana
Elimu kutopewa kipaumbele etc
Twende siku moja tutafika.
 
chama chako wewe na nani? hicho mbona wenyewe wanafahamika? jikusanyeni na mkaanzishe chenu. si mnaona zito anavyopeta na chake? mbunge yeye peke yake. kiongozi mkuu yeye mwenyewe. raha tupu yaani.
 
Na wewe!! Sasa chama bila wanachama unaona nini.
chama chako wewe na nani? hicho mbona wenyewe wanafahamika? jikusanyeni na mkaanzishe chenu. si mnaona zito anavyopeta na chake? mbunge yeye peke yake. kiongozi mkuu yeye mwenyewe. raha tupu yaani.
 
Back
Top Bottom