CHADEMA na CCM wanavyoiua Muganza - Chato

CHADEMA na CCM wanavyoiua Muganza - Chato

JamboJema

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2011
Posts
1,143
Reaction score
209
Kumekuwa na malumbano yasiyo na tija kati ya CCM na CHADEMA huko Muganza kiasi cha kuathiri kwa kiwango kikubwa mstakabali wa maendeleo ya wanamuganza. Ilikuwaje?.....Mwaka 2010 kabla ya uchaguzi mkuu WDC waliamua kujenga zahanati ya kijiji.

Wakati huo Diwani akiwa kutoka CCM. Mkakati wa ujenzi ukaanza na kuonekana kusimama kupisha uchaguzi. Baada ya uchaguzi, diwani wa CHADEMA akapatikana.....bahati mbaya[kama ndivyo ilivyo] wenyeviti wa vijiji wa Kata hii wote ni CCM. Mpango wa ujenzi wa zahanati 'ukagomewa' na waCCM hawa. Jitihada zote za diwani hazikuzaa matunda!

Mwaka jana, watoto waliomaliza darasa la saba na kuchaguliwa kuingia kidato cha kwanza katika kata hii yenye shule moja tu ya sekondari - Zakia Megji, wanazidi idada ya madarasa yaliyopo. Watoto 138 wanakosa vyumba vya kusomea. Hakika ni kama vyuma vinne vinavyopungua. WDC ikaamua madarasa yajengwe. Siasa za CHADEMA zikapita kwa wananchi kuwa ni kwa nini wachangie madarasa hali zahanati haijajengwa. Wananchi wakagoma kuchanga!

Muziki ni kuwa, wenyeviti wa vijiji (CCM) wamekubali kuchangisha ili madarasa yajengwe; wananchi wanazuiwa na CHADEMA kuwa kwa nini watekeleze mradi wa pili wakati wa kwanza(zahanati) haujatekelezwa. Wananchi wengi wanaona CHADEMA wako sahihi na matokeo yake si zahanati wala madarasa vinavyojengwa!

Imegeuzwa kuwa zahanati ni sera ya CHADEMA na shule ni sera ya CCM. Hii ndio siasa tunayoijenga watanzania!
 
hili ni tatizo la uelewa,mimi naunga mkono sera ya CDM kwasababu tunalipa kodi iwe moja kwa moja au VAT,hivyo serikali ijenge shule na zahanati kama haiwezi iondoke.
 
Ma Padlock anasemaje si ndiyo Mungu wenu huko shauri yenu si mlipenda kuchagua maga.mba?
 
Niko Muganza. Ni kweli yalikuwepo malumbano ya nini kitangulie kati ya zahanati au madarasa. Diwani wa CDM ameweka nguvu kwenye zahanati na sasa mkandarasi anajenga boma. Kuna milioni 20 ambazo zimechangwa na wananchi tayari kwa kazi hii. Fedha hii itatosha kufikisha jengo kwenye linta. Awali diwani wa CDM; Mh. MADUKA, aliweza kuchangisha kutoka kwa wananchi na kufanikiwa kujenga msingi na kumwaga jamvi lake. Kulingana na utaratibu uliopo sasa, nguvu za wananchi kwenye kujenga zahanati zinaishia kwenye linta. Baada ya hapo serikali ngazi ya halmashauri ya wilaya humalizia kwa pesa kutoka mpango wa MMAM. Kwa upande wa Muganza mratibu wa MMAM wilaya Ndg.Rutatondelwa na Eng. Rwegoshora wamefurahishwa na kasi ya uchangiaji huu na kuahidi kuruhusu fedha ya MMAM mara baada ya boma kuisha.

Kuhusu madarasa ni kweli upo uhaba wa vyumba kwa ajili ya wanafunzi. Wiki iliyopita Kijiji cha Kasenda wamempata mkandarasi ambaye ameanza kuchimba msingi leo. Aidha vijiji vya Katete na Rutunguru viko vimeita wazabuni wa kujenga madarasa moja moja kila kijiji. Jumatatu ni siku ya kufungua zabuni na kutoa kandarasi.

Kumekuwepo na hujuma kutoka CCM ili diwani ashindwe kutekeleza majukumu yake ili aonekane sawa na mtangulizi wake Mr. Jahazi. Lakini kutokana na utashi watu(peoples' power) katika mkutano uliofanyika katani, wananchi wote waliazimia Zahanati ianze wakitaja kuwa watoto wakifa kwa magonjwa madarasa hayatakuwa na maana kwao. Kimsingi diwani huyu ni hazina kwa CDM na ana uwezo mkubwa kiuongozi hasa katika kushawishi.

Diwani huyu wa Muganza (CDM) akishirikiana na madiwani wenzake 4 wa CDM wamekuwa mwiba mchungu hapa Chato kiasi cha kuifanya wilaya ya Chato sasa kuwa ngome ya CDM. Ikumbukwe Ndg. Ntinonu,aliyekuwa mwenyekiti wilaya ya Geita na kuhamia CDM hivi karibuni ameisambaratisha ngome ya CCM kwenye kata ya Katende-Chato(Alikozaliwa) akishirikiana na Kamanda Prof. Lucanima(yule aliyekuwa mhadhiri wa Mzumbe kabla ya kwenda kufundisha Columbia). Prof. Lucanima alikuwa mshindi wa pili kwenye kura za maoni za CCM 2010 nyuma ya Magufuli. Alivua gamba mwaka jana na kuhama na wanachama wengi wa CCM
 
Anaweza asigombee tena. Upepo ni mkali sana

upepo ni mkali mpaka kwa mzee wa Lubambagwe huyu huyu alepitishwa mara kadha bila kupingwa! basi mambo yanazidi kuharibika kwa ccm.wananchi wa mganza wamesha ziona mbivu na mbichi.Mwaka 2014 siyo mbali kwa ajili ya maendeleo yao kata,vijiji vyote na vitongoji vyote wekeni pipoziii pawa ili maendeleo ya nyoke bila mkwaruzo.
 
YETU MACHO...ILA PICHA NILILOLIONA MUGANZA SIO JEPESI KAMA Gosbert UNAVYOLIELEZA. HAKIKA NILIANZA KUCHUKUA UWEPO WA VYAMA VINGI KWANI MAMBO KIMANTIKI HAYAENDI!
 
YETU MACHO...ILA PICHA NILILOLIONA MUGANZA SIO JEPESI KAMA Gosbert UNAVYOLIELEZA. HAKIKA NILIANZA KUCHUKUA UWEPO WA VYAMA VINGI KWANI MAMBO KIMANTIKI HAYAENDI!

Mkuu JamboJema Naona maelezo ya Gosbert yana mashiko, sababu ya mambo kusuasua ni vidudumtu vya ccm. logicwise si busara kuanza kujenga vyumba vya madarasa wakati mradi wa ujenzi wa Zahanati haujaukamilisha. kamilisha zahanati haraka kisha anza kujenga vyumba vya madarasa. hawa ccm kazi yao propaganda, wanawakwamisha chadema ili watengeneze single kana kwamba wananchi hawana macho vile!!!
NDIYO MAANA WALE WA MASASI HAWAJUI CHUKI ILITOKEA WAPI HADI WANANCHI WENYE HASIRA KALI KUZICHOMA KWA MOTO NYUMBA ZAO WAO WANA CCM NA NI VIONGOZI WAANDAMIZI.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JamboJema Naona maelezo ya Gosbert yana mashiko, sababu ya mambo kusuasua ni vidudumtu vya ccm. logicwise si busara kuanza kujenga vyumba vya madarasa wakati mradi wa ujenzi wa Zahanati haujaukamilisha. kamilisha zahanati haraka kisha anza kujenga vyumba vya madarasa. hawa ccm kazi yao propaganda, wanawakwamisha chadema ili watengeneze single kana kwamba wananchi hawana macho vile!!!
NDIYO MAANA WALE WA MASASI HAWAJUI CHUKI ILITOKEA WAPI HADI WANANCHI WENYE HASIRA KALI KUZICHOMA KWA MOTO NYUMBA ZAO WAO WANA CCM NA NI VIONGOZI WAANDAMIZI.
YOTE SAWA ILA KUMBUKA WATOTO HADI SASA HAWAENDI SHULE WANASUBIRI MADARASA.....i THINK HATA KAMA KUNA U-CCM NA U-CDM WANGEPASWA KUWAANGALIA WATOTO HAWA KWANZA! nGUMI ZAO ZISIWAKOSESHE WATOTO HAWA HAKI YA KUSOMA. nDO ANGALIZO LANGU!
 
Kiufupi hapo ni kwamba wananchi hawako aggressive na maendeleo. Kinachowafanya wakubali kukatazwa kuchangi shule ni kwamba kwao wao hata shule isipokuwepo ni sawa. Wangekuwa wanajali wangemwambia huyo diwani aache kuwadanganya na wangechangia shule yao ijengwe.
Kwahiyo hapo wamekutana wananchi wasiojali maendeleo, diwani wa chadema asiyejadli maendeleo na viongozi wa vijiji wanaofikiria kisiasa zaidi.
 
Back
Top Bottom