CHADEMA mtegoni!!!!

Hawa ccm na Zitto team wamemwaribia zaidi Zitto kwenye siasa na kumjenga zaidi Dr Slaa kwani siku za Leo watu wanachambua sana mambo maana najua kabisa kesho magazeti yote ya ccm na washirika wake eg mwananchi waripoti kuwafurahisha wafadhili lakini j3 CHADEMA watafafanua na tutaelewa ukombozi unaendelea.
 

Kuna kitu kimoja nakiona hapo mbeleni, sasa hivi ni Dr. Slaa anabebewa mabango kwa sababu wanaofanya hivyo(wanaotumwa) hawatapata au wameahidiwa kutopata madhara yoyote kwani Dr. hana dola. Kama ingekua ni waziri mkuu au Rais anafanyiwa hivyo ingekua ni shida. Ila wanawaonyesha watu wengine wengi zaidi waliochoshwa na umaskini, ahadi hewa za viongozi, elimu duni, njaa, nk. jinsi ya kufikisha ujumbe kwa watawala kwa njia hii mpya. Sasa hivi Rais na mawaziri wake wataona hicho kinachomtokea Slaa kinawatokea na wao tena kwa nguvu zaidi. Hofu yangu ni moja tu, "vitu vyenye ncha kali".
 
Hivi CDM walitegemea walipoeanda Kigoma walifikiri policcm watawalinda kwa dhati? Hili ni kosa lingine ambalo hawa jamaa wa CDM nawaona hawako serious. Kama mt anatoa vitisho mbele ya RPC na anaangaliwa tu unategemea nini hapo? Tangu lini mmeanza kuwaamini policcm nyie? Au mnajisahaulisha matukio?
 


Tunakushukuru kwa kuliona hili kwa kutumia akili yako na sio vinginevyo ,tulianza na Mungu tutamaliza na Mungu.Nnawashauri wanachama wengine wa ccm wawe wakweli kama ulivyokuwa mkweli hapa,Mungu akubariki sana.
 

.
Siasa za kupingana kwa hoja ndio tunu ya ulimwengu uliostaarabika. Ndio siasa zinazofanywa kwenye zile nchi tunazopeleka bakuli kuomba msaada. Unafikiri siasa za fujo na mabavu kama za Liberia ya Teyla zitamkomboa binadamu ama zitamwangamiza? Ona masikini wale vijana waliobeba mabango walichokuwa wamevaa miguuni. Nilipowaona hali zao nilitafuta mahali pa peke yangu nikawalilia. Nilitafakari na nisipata jibu, kwamba umeme unapandishwa hawaandamani, kodi za simu zinaasisiwa wala hawana habari jamo mwenye uwezo kwao anamiliki simu na uwezo wa kutumia vocha ya buku kwa huo mwezi unaotakiwa hana. Achalia mbali shule, dawa hosptalini nk ambazo hawana. Basi demokrasia imewaruhusu ili mufikishe mabango yenu na yamulikwe na media zote ujumbe ufike sasa mawe mnayorusha ya nini? Ndio tuseme hayo mawe yatamrudishia Zitto unaibu katibu aliyonyanganywa kwa mujibu wa taratibu na miongozo ya chama chake? Jingine ni kwamba chadema wana uwezo mkubwa wa kulinda mikutano yao kuliko hata wawezavyo kufanya polisi lakini wameliacha suala hili mikononi mwa polisi ili kulinda utengamano wa taifa. Lakini ikifika mahali ambapo tunaona watu wasiozidi kumi na tano wanawashinda polisi wenye silaha basi itabidi uzalendo utushinde na hivyo kutangaza uasi kwa taratibu za polisi kwa kuchukua jukumu la ulinzi sisi wenyewe. Dr Slaa kawaacha wenye mabango watoe dukuduku lao na huu ni ukomavu wa kidemokrasia ulio juu sana katika bara hili. Sii hata sisiem wanaothubutu kuruhusu bango limfikie mwenyekiti wao. Sasa tunasema kama hao wenye mabango hawawezi kuwa na siasa za kupingana kihoja basi raia tutahakikisha hata ruhusa ya kukanyaga uwanja wa mkutano hawaupati.
TANZANIA YA LEO DR SLAA NA CHADEMA WANATAJWA ULIKO BIDHAA YEYOTE ILIYOPO KATIKA MATUMIZI YA KILA SIKU YA BINADAMU.
.
 

Mkuu umezungumza kila kitu lakini sijui ni wanachi wangapi wenye uelewa hasa pale wanapotumika kisiasa,wahenga walinena "Mchuma janga hula na wa kwao"vijana tujifunze sana namna ya kuishi.Serikali ya ccm imetusababishia maisha magumu sana kwa kipindi kirefu huu mfumo haufai tena kwa sababu umeshindwa kutekeleza kile ilichokiahidi.
 
Chadema kwa kupenda kisifiwa!!!! Wakosoe sasa hata kwa nia njema matusi utayaka!!!
 
Kwa hiki ulichokiandika kinaendana na ID yako ya trade name ya condom kwa hiyo hapo ulipo unatumika

Kamanda natumika kivipi? Wewe ndio unatumika na unashirikiana na MINI KABAANG!
 

Mkuu mi sina haja ya ku comment kwenye maneno yako yoote ispikuwa hio sentensi ya mwisho.
Kutajwa sana kwa chadema na dr slaa hakumaanishi chochote cha maana!
Hata wakati wa watu walipoanza kuhara ovyo. Kipindupindu kilikuwa kinatajwa kuliko kitu chochote Tanzania! Na kilipopita. Basi maisha yakarudi kama kawaida.
Kwa hivyo. Chadema ni kama mfano huo. Na hii balaa ikishatupwa jalalani 2015. Maisha yetu yatarudi shwaaari kama zamani.
Hatutosikia tena miripuko wala maaandamano yasio na kichwa wala kiuno.
Na hilo jina la Slaa litabaki kama la bulicheka. Kwenye vitabu vya hadithi za alinachana.

Cc Ritz
 
Last edited by a moderator:

.
Mkuu nakushukuru sana ila na wewe huoni wasi wasi wako upo hapo 2015? Kutajwa sana kwa chedema na Dr Slaa ni hofu ya 2015.
Chadema kwa sasa zikiitishwa chaguzi hata za vijijini inashinda bila hata kutumia nguvu kubwa. Hofu kuu ya system kwa sasa ni nani ndani ya sisiem mwenye uwezo wa kushindana na Dr Slaa? Hofu yao iko hapo. Ni kweli kwa mfano wako Kipindupindu ni ugonjwa hatari ambao katika jitihada za kuuzuia hutajwa sana laa sivyo utawamaliza watu wotu. Hali kadhalika chadema hutajwa sana kwa sababu ya hatari waliyoisababishia system. Wanafanya kila njia kuizuia kwani wasipofanya hivyo itashinda chaguzi zote kuanzia serikali za mitaa ubunge na urais.
Nami kwa upande wangu sioni kama wanaweza kuizuia chadema kuchukua nchi.
.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu kwanza naomba utambue kuwa mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa.
Na siasa ya Tz si lolote zaidi ya utapeli wa mchana!
Kitu Ninachosema ni kuwa CCM juu wa kasoro zake na juu ya shida zetu Watu tumeishi kwa amani miaka yote.

Toka chadema ianzishe hizo pirika zake za kuwania uongozi watanzania tumejengewa UADUI MKUBWA SANA!

Leo imekuwa wana CDM na wana CCM ni maadui kabisa! We unayaona mwenyewe humu jf!
Na husikii uadui huu kutoka vyama vingine kama ccm na cuf. Au ccm na nccr. N.k

Zile nchi ambazo watu wamechinjana na kuuwana wao kwa wao. Woote WALIANZA KAMA SISI!!
Ilikuwa uadui wa vyama au makundi. Mwishowe wakaingia ktk vita vya silaha!

We hebu fikiri ni watanzania wangapi wamepoteza maisha kwa sababu hizi za ushindani. Tena wa hivyo vyama viwili??

Mnataka yatokee mangapi mpaka muache hizo harakati zenu za kuwania uongozi kwa fujo?

Watu badala ya kuonyesha wananchi mazuri watakayo yafanya. Basi wao kazi yao ni kuonyesha MABAYA YA WAPINZANI WAO.

Msipo badilisha hii tabia. Basi mtakujastukia wananchi wamebeba mapanga wanauwana ovyo!
Shauri yenu.
 

Tupa tupa kaa hapohapo Lumumba kwanza ukiwa unaangalia namna vijana wa Lumumba kina Pius Msekwa, Kingunge, Samweli, Mangula nk wanavyopambana kukinusuru chama cha zamani
 

Sawa kabisa mkuu, hata mimi nilishawaambia waende kwenye nyumba za Ibada kuomba HAKI ZAO lkn hawakunisikia kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…