CHADEMA mnashaurika, shaurikeni na hili

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,306
25,928
Kwanza nikiri kufurahishwa na CHADEMA kupokea ushauri wangu pamoja na wa wana-JF wengine juu ya Uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki. Niliwashauri humu humu JF. Niliwashauri hivi: CHADEMA, pelekeni majina zaidi ya mawili Bungeni kumaliza utata EALA. Sasa mpo kwenye mchakato wa kupata majina ya nyongeza kwa ajili ya kuwasilisha tena Bungeni kwa upigaji wa kura. Ni jambo jema na ni hatua nzuri. Kwahilo, CHADEMA mnashaurika.

Sasa shaurikeni na jambo hili lenye pande mbili. Mosi, amueni kwa vitendo kujenga ofisi zenu (Ofisi Kuu na zile za kanda na kadhalika) zenye hadhi ya chama chenu. Endesheni hata harambee ya ujenzi wa ofisi zinazoakisi ukubwa, umaarufu na umuhimu wa chama chenu. Ofisi zenu za kwenye 'maflemu' zimepitwa na wakati. Ni wakati wa kuendana na hadhi yenu.

Pili, jiimarisheni katika ngazi za chini kuanzia shinani. Imarisheni chama chenu katika sehemu ambazo watu hawajui hata uwepo wa vyama vingi. Huko ndiko walipo wapiga kura. Huko ndiko wanakochaguliwa viongozi wanaojaza Bunge letu na kutuamulia mambo yetu. Huko ndiko wanakochaguliwa wanaojadili masuala ya kitaifa. Ngazi ya chini huamua muenekano wa ngazi za juu. Ndipo msingi hasa ulipo.
 
Kwanza nikiri kufurahishwa na CHADEMA kupokea ushauri wangu pamoja na wa wana-JF wengine juu ya Uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki. Niliwashauri hivi humu humu JF. Niliwashauri hivi: CHADEMA, pelekeni majina zaidi ya mawili Bungeni kumaliza utata EALA. Sasa mpo kwenye mchakato wa kupata majina ya nyongeza kwa ajili ya kuwasilisha tena Bungeni kwa upigaji wa kura. Ni jambo jema na ni hatua nzuri. Kwahilo, CHADEMA mnashaurika.

Sasa shaurikeni na jambo hili lenye pande mbili. Mosi, amueni kwa vitendo kujenga ofisi zenu (Ofisi Kuu na zile za kanda na kadhalika) zenye hadhi ya chama chenu. Endesheni hata harambee ya ujenzi wa ofisi zinazoakisi ukubwa, umaarufu na umuhimu wa chama chenu. Ofisi zenu za kwenye 'maflemu' zimepitwa na wakati. Ni wakati wa kuendana na hadhi yenu.

Pili, jiimarisheni katika ngazi za chini kuanzia shinani. Imarisheni chama chenu katika sehemu ambazo watu hawajui hata uwepo wa vyama vingi. Huko ndiko walipo wapiga kura. Huko ndiko wanakochaguliwa viongozi wanaojaza Bunege letu na kutuamulia mambo yetu. Huko ndiko wanakochaguliwa wanaojadili masuala ya kitaifa. Ngazi ya chini huamua muenekano wa ngazi za juu. Ndipo msingi hasa ulipo.
Kutwa kucha mawazo ya CDM yapo mahakamani, sidhani Kama ushauri wako utawafaa !
 
Chadema baada ya kugundua waliingizwa Mkenge na Tundu Lissu wameamua kufuata ushauri wa Spika wa Bunge kuitisha upya Mchakato wa Ubunge wa EA ngazi ya Chama japo hapo awali walijidai wasingetekeleza ushauri huo wa Spika

Hongereni Chadema kushaurika
 
Nafikiri watakuelewa! Ingawa sio lazima sana kama zilizopo zinakidhi mahitaji ya sasa!
Ingawa ni muhimu kuwa na ofisi nzuri
 
Back
Top Bottom