CHADEMA: Kuweni makini na jimbo la Segerea

CHADEMA: Kuweni makini na jimbo la Segerea

b2015

Member
Joined
Nov 14, 2013
Posts
42
Reaction score
22
Habari ambazo sijazidhibitisha ni kwamba mnataka kumsimamisha Makongoro Mahanga kugombea jimbo la Segerea nawapa taadhari huyu mtu hatumtaki na hatashinda so kuweni makini na uteuzi,mwaka 2010 pamoja na kuchakachua matokeo bado alisema kashinda kwa nguvu ya hela zake hicho kitu kimewakaa watu moyoni mpaka leo hivyo msijaribu kumrudisha jimbo litapotea
 
huyo ni mmoja wa watu 30+ ambao lowasa ameamuru wapewe nafasi, hakuna namna nyingne ni mahanga tu
 
Uu uhuni wa Cdm na Ukawa kuwapa new comer pruority badala ya waliojenga chama nadhani ni tatizo litalotusumbua mbeleni au kitambo kidogo
 
Makongoro Maanga hana mvuto tena segerea, yeye apewe kazi ya kuzunguka vijijini akawashauri ndugu zake waame ccm, Segerea hatumtaki
 
Ni kweli inabidi awekwe mtu anayekubalika kwa wananchi.....CCM watatuliza
 
iko wazi tukimsimamisha mtu ambae wananchi hawampendi na hajawafanyia chochote tutapoteza jimbo, viongozi teremkeni chini kwenye kata mjue ubaya wa mtu huyu atatupa ugumu kumuuza .

pia tusimpe kila kiongozi. anayekuja madaraka makubwa ya uwakilishi .
viongozi wa kanda tutendeeni haki msituwekee huyu hatutashinda. hakuna atakaye linda kura kwa huyu mahanga,ni sawa na kumpitisha mgombea wa ccm bila kupingwa.
 
kila mtu na umbea wake ...kura za maoni jimbo la segerea zilishafanyika...muache udaku subirini majina yatangazwe
 
Hakika wasi tuhalibie segerea yetu huyo mahanga hatu mtaki kabisa.hili jimbo sio Mali yake Muda aliyo kuwa Kama mbunge unatosha.ndio huyu huyu alikuwa Ana tuambia kuwa kapata ubunge Kwa hela yake na sio Kwa kura zetu.big noooooo
 
Mahanga mbali na kuwa hana MVUTO segerea lakn ni hazina katika kuisambaratisha CCM huko segerea. Hivyo ashiriki kikamilifu kwenye kampeni kwa yeyote atakayependekezwa na ukawa.....
 
Nasikia na mtu wa Lowassa na makubaliano ya kuja Chadema masharti lazima wampe nafasi ya kugombea Segerea.
 
Uu uhuni wa Cdm na Ukawa kuwapa new comer pruority badala ya waliojenga chama nadhani ni tatizo litalotusumbua mbeleni au kitambo kidogo

Hamkulijua hilo, endeleeni kuchekelea na kuropoka, mtafurahi tu muda si mrefu, mnafikiri siasa ni jazba?
 
Habari ambazo sijazidhibitisha ni kwamba mnataka kumsimamisha Makongoro Mahanga kugombea jimbo la Segerea nawapa taadhari huyu mtu hatumtaki na hatashinda so kuweni makini na uteuzi,mwaka 2010 pamoja na kuchakachua matokeo bado alisema kashinda kwa nguvu ya hela zake hicho kitu kimewakaa watu moyoni mpaka leo hivyo msijaribu kumrudisha jimbo litapotea

mahanga hawezi shinda nadhani wahusika wanalijua hilo,wakiziba masikio watausikia mziki wake October 26
 
Back
Top Bottom