Deogratius Mosha
Member
- Aug 3, 2012
- 25
- 3
uwe mstaarabu kisa cha kuniita gamba ni nini? wewe unayejiita cdm hata kadi huna hata katiba ya chama hujui inafanana je sisi kwa tarifa yako ndio waanzilishi wa chama na makala kama hizi ni changamoto kwa chama chetu sasa usipende kuexpose ujinga wako kwenye jukwaa hili!
Nashikwa na kigugumizi kuchangia mada hii, Hivi majaji wa Kesi ya LEMA na wale walioamua kezi za Igunga na Sumbawanga tofauti zao nini, CDM wakishinda, jaji mzuri, wakishindwa, jaji wa CCM. Haya mambo yanakuaje? si tuachane na haya mambo ya vyama vingi? Haya mambo ya wazungu bwana, Afrika tunadandia gari kwa mbele.
I read the topic submitted by the author, in between the lines, and therefore come up with the following opinions; as being among the citizens of Arusha urban, educated, patriotic and exceedingly in love with CHADEMA politics, i would like to inform Tanzanians, firstly, the CDM is a strongest opposition political party in Arusha region and the Northern zone in its generality, the reason of which it could not made the party being coward of not going to another by-election. Secondly, CHEDEMA, an accurate party, in its form and content, with intensive discussion and for the betterment of the marginalized Tanzanians, it could not just, think of a new by-election, but rather, think of very expensive and unnecessary costs the by-election will incur. Upholding the notion of unnecessary costs, the CDM party, has affirmative thought of referring the matter to the Court of Appeal of Tanzania, as to oversee the irregularities of the previous decisions made by the High Court Of Tanzania avoiding the what we so called "miscarriage of Justice" by seeing the provision of justice by the current final house of justice.
Haki gani wanaisimamia wakati wanawanyima wananchi wa jimbo la Arusha haki ya kuwakilishwa bungeni?
ulichokiandika hakifanani na mwana CDM, mwanachama asiyejua chama kinafanya nini?
Bahati yako nakusamehe kwa sababu umeCOPY na kuPASTE
Mkuu Osokoni,
1. Naona umeamua kuweka habari kutoka kwenye Nipashe pasipo mwisho wa habari yenyewe kuweka source. Hii imetufanya wengi wetu tudhanie kuwa ni wewe ndio uliyeiasisi na kuiweka na hivyo kupokea mashambulizi mengi. Tungeendelea kuamini hivyo kama isingewekwa habari yanyewe, tarehe ya kuandikwa na jina la Mwandishi. Hata hivyo, tutaichangia mada kama ilivyo.
2. Kwa waliokuwepo pale Viwanja vya NMC siku ile ya Jumamosi ya tarehe 08. 04. 2012, watakubaliana nami kuwa 'kipande nilichonukuu' ndiyo haswa msingi wa CHADEMA na Lema kukata rufaa. Wananchi wa Arusha mpaka Mh Mbowe alipooa kauli ile walikuwa na AMRI na NIA ya kuingia tena kwenye uchaguzi na walidhamiria kulinda kura zao (kutokana na uzoefu walioupata kutoka Arumeru Mashariki juma moja tu lililopita) . Lakini Mh. Mbowe alieleza kuwa, "kuyakubali maamuzi yale ya Mahakama na Kukubali Kuingia Kwenye Uchaguzi Mdogo, Hata Kama Una uhakika kwa Kushinda, utakuwa umemaanisha kuwa, unakubaliana na mwenendo mzima wa mashtaka na shauri lenyewe. Kwamba CHADEMA na Lema, ni chama cha kuwadhalilisha wanawake; na ni chama cha ubaguzi. Lakini pia, hukumu ile ya kibaguzi na kionevu, itatumika kama rejea ya mahakama (Judicial Precedence) katika kutolea maamuzi siku zijazo. Watoto wetu wataonewa na kugandamizwa. Wataporwa Haki zao. Kuikubali hukumu ile, kutamaanisha kuwa wananchi maskini wa kitanzania, wataenda tena kugharamia uchaguzi ule mdogo (sikumbuki vizuri, ila nadhani alisema ni 4bn). Hukumu ile, haisemi hatma ya Mh. Lema kama anaruhusiwa kugombea au la. Amepewa hukumu ya kosa ambalo si la kwake"
3. Ukisoma makala hii tu kwa juu juu bila ya kumfahamu Mwandishi Mwenyewe wa Makala na aina ya uandishi wake utakuwa unakosea. Kwa wale ambao hawafahamu ni kuwa, uandishi wa habari wa Tanzania wa habari za kiuchunguzi/makala au michezo unafanana. Kwamba kuna waandishi wenye kambi ya Simba na Yanga. Na waandishi wa habari za Siasa, nao wako kwenye kambi hizo pia. CCM, CHADEMA, CUF n.k. Makala na habari za Muhibu Said tangu akiwa anaandikia gazeti la Mwananchi kama freelancer, zilikuwa zinaonyesha dhahiri upande aliopo. Na kwa muda wote, alikuwa akiripoti habari zilizohusu Chama Cha Wananchi (CUF). Alizunguka katika misafara yote ya Pr. Lipumba na hata lile tukio la yule mtoto inayesemekana kuiba sanduku la kura na kupigwa risasi na Mkurugenzi wa Temeke, ni yeye ndiye alikuwa anaripoti. Na hata alipojiunga na Nipashe, ameendelea kuandika, kwa asilimia kubwa, habari zinazomhusu Lipumba na chama cha CUF.
Hivyo, sikushangaa kusoma makala kama haya kutoka kwa mwandishi mwenye 'calibre' ya Muhibu. Ni nani amesahau namna Novatus Makunga (aliyewahi Kugombea Kura za Maoni Ubunge kupitia CCM) alivyokuwa anaripoti kampeni, upigaji kura na hata kuwasilisha matokeo ya awali katika uchaguzi mdogo wa Ubunge Arumeru Mashariki?
- Ni Makunga aliyekuwa kila akiripoti habari za Sioi, anaweka picha za kampeni za urais mwaka 2010 kuonyesha watazamaji wa ITV kuwa wale walikuwa ni wahudhuriaji wa mikutano ya kampeni wa Sioi.
- Ni Makunga ambaye wakati akiripoti kuhusu watu waliojitokeza kwenye kupiga kura, alieleza kuwa " waliojitokeza kwenye upigani wa kura ni wazee tu, na vijana hawakuwepo, tofauti na wakati wa mikutano ya kampeni walikuwa wengi", wakati mtangazaji mwenzake, Asraj Mvungi 'akielezea kuwa Vijana walijitokeza kwa wingi katika upigaji wa kura, kama ilivyokuwa katika mikutano ya kampeni'.
- Ni Novatus Makunga huyu huyu, miezi michache baadaye, aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai!
Kama Great Thinkers ( GT), inatupasa kuthink Critically.
I read the topic submitted by the author, in between the lines, and therefore come up with the following opinions; as being among the citizens of Arusha urban, educated, patriotic and exceedingly in love with CHADEMA politics, i would like to inform Tanzanians, firstly, the CDM is a strongest opposition political party in Arusha region and the Northern zone in its generality, the reason of which it could not made the party being coward of not going to another by-election. Secondly, CHEDEMA, an accurate party, in its form and content, with intensive discussion and for the betterment of the marginalized Tanzanians, it could not just, think of a new by-election, but rather, think of very expensive and unnecessary costs the by-election will incur. Upholding the notion of unnecessary costs, the CDM party, has affirmative thought of referring the matter to the Court of Appeal of Tanzania, as to oversee the irregularities of the previous decisions made by the High Court Of Tanzania avoiding the what we so called "miscarriage of Justice" by seeing the provision of justice by the current final house of justice.
Mkuu huwa nakuamini sana lakini mada yako ya leo umeteleza kidogo.CDM imekata rufaa kwa sababu hukumu inasema Lema haruhusiwi kugombea tena mpaka miaka 5 ipite...
Haki gani wanaisimamia wakati wanawanyima wananchi wa jimbo la Arusha haki ya kuwakilishwa bungeni?
kumbe unaweza kugundua itikadi na akili za mtu kutokana thread zake. Mia
kumbe unaweza kugundua itikadi na akili za mtu kutokana thread zake. Mia